Mikutano Ya Utumishi Kwa Januari
Juma Linaloanza Januari 4
Dak. 15: Matangazo ya kwenu na matangazo yafaayo kutoka Huduma ya Ufalme Yetu. Watie moyo wahubiri wafanye mipango sasa ya kufanya upainia msaidizi katika Machi na Aprili. Familia na wahubiri wachanga watakaokuwa likizoni katika Machi na Aprili wanatiwa moyo waone ni mipango ipi wanaoweza kufanya ili kushiriki zaidi hudumani. Waweza kutumia baadhi ya mawazo kutoka kwa makala “Umepangia Nini Machi na Aprili?” kutoka Huduma ya Ufalme Yetu ya Januari 1991 ili kuwatia moyo akina ndugu waanze kutayarisha sasa kwa ajili ya majira ya Ukumbusho.
Dak. 15: “Wachukuaji Nuru Katika Ujirani.” Kazia njia ambazo matoleo mapya yaweza kutumiwa katika eneo la kwenu.
Dak. 15: Hotuba juu ya “Biblia” yenye kutegemea kitabu Kutoa Sababu, kurasa 40-6. Kazia faida tunazopata kibinafsi kwa kutumia kanuni za Biblia maishani mwetu.
Wimbo 139 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 11
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Eleza mipango kwa ajili ya utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 20: “Hubiri Njia ya Mungu ya Kuleta Amani na Usalama.” Makala hiyo ipitiwe kwa maswali na majibu. Watie moyo wahubiri watumie trakti katika utumishi wa shambani. Baada ya kuzungumzia fungu la 3, mhubiri aliyejitayarisha vizuri atoe wonyesha wa jinsi funzo la Biblia liwezavyo kuanzishwa ama kwenye ziara ya kwanza ama kwenye ziara ya kurudia, kwa kutumia trakti Je! Ulimwengu Huu Utaokoka? Mhubiri: “Habari za asubuhi. Tunaongea na watu leo juu ya hali ya maisha. Je! wewe unatosheka na yale unayoona yakitukia katika maisha ya watu leo?” Mwenye nyumba: “Kwa kweli sivyo.” Mhubiri: “Je! wafikiri hali itakuwa bora zaidi?” Mwenye nyumba: “Sijui.” Mhubiri atoa trakti na kusema hivi: “Wengine hufikiri kwamba yale yanayotokea ni utimizo wa unabii wa Biblia na kwamba mwisho wa ulimwengu uko karibu. Wewe unaonaje?” Mwenye nyumba: “Sijui. Nadhani inawezekana.” Kisha mhubiri anarejezea trakti na kueleza kwamba mwisho wa ulimwengu haumaanishi mwisho wa mbingu na dunia halisi. Mhubiri apangia ziara nyingine ili kuchunguza uthibitisho wa Biblia kwamba mwisho wa mfumo uliopo uko karibu.
Dak. 15: Kujiepusha na Matatizo ya Utiaji Damu Mishipani—Wakati wa Kufanya Upya Mwelekezo Wetu wa Mapema Kuhusu Tiba. Mzee anayeshughulikia sehemu hii aelekeza kadi mpya zigawanywe kwa wahubiri waliobatizwa na azungumzia kwa uangalifu, barua ya Oktoba 15, 1991, inayoeleza matumizi ya kadi hizo. Katika kujitayarisha, pitia kwa ukamili barua ya Sosaiti ya Januari 1, 1990. Wale wanaotia sahihi kuwa mashahidi wanapaswa kwa kweli kumwona mwenye kadi akitia sahihi hati hiyo. Watie moyo wote wakamilishe kadi mpya kabla ya kuondoka Jumba la Ufalme. Wahubiri waliobatizwa hawapaswi kamwe kuondoka nyumbani bila kadi yao ya Mwelekezo wa Mapema Kuhusu Tiba/Ondoleo la Hatia. Watoto wadogo wasiobatizwa wenye mzazi aliye Shahidi wanapaswa kuibeba sikuzote Kadi ya Utambulishi. Uchunguzi mmoja wa hivi majuzi kwenye mkutano mmoja wa kundi ulionyesha kwamba mmoja kati ya kila wahubiri watano hakuwa na kadi yake, na hakuna watoto waliokuwa na Kadi ya Utambulishi zao. Kwa kumalizia, soma na kufanyia matumizi Mithali 22:3.
Wimbo 151 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 18
Dak. 10: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi. Soma ripoti ya hesabu na shukrani za Sosaiti kwa upaji. Pongeza kundi kwa ajili ya utegemezo mwaminifu-mshikamanifu wa kifedha wa kundi la kwenu na wa kazi ya Sosaiti ya ulimwenguni pote.
Dak. 20: “Kutumia kwa Hekima Vyombo vya Muhimu.” Baada ya utangulizi mfupi ukitolewa na mwenyekiti, kutakuwa maonyesho mawili yanayotegemea habari inayoelezwa katika mafungu 2 hadi 5. Mwishoni mwa wonyesho wa kwanza, mwenye nyumba akubali magazeti mawili. Mhubiri aahidi kurudi ili kujibu swali, Kwa nini Mungu huruhusu kuteseka? Mwishoni mwa wonyesho wa pili, funzo la Biblia nyumbani laanzishwa kwa kutumia trakti inayofaa. Watie moyo wote wawahusishe wenye nyumba katika mazungumzo ya Kimaandiko wanaposhiriki katika utumishi wa shambani mwisho-juma huu.
Dak. 15: Sababu Kwa Nini Wakristo Hujiepusha Na Damu. Hotuba ikitolewa na mzee yenye kutegemea fasili na vichwa vidogo vitatu vya kwanza chini ya kichwa “Damu” katika kitabu Kutoa Sababu, kurasa 50-1.
Wimbo 177 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Januari 25
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzia mambo makuu kutoka makala “Pendeleo Zuri la Utumishi.” Jinsi wakati uruhusuvyo, hoji mhubiri aliye na njia iliyo imara ya kupelekea watu magazeti kwa ukawaidia. Aliianzishaje? Nayo imemsaidiaje akuze kupendezwa au kutambua kwa wazi kadiri ya kupendezwa upande wa mwenye nyumba?
Dak. 15: “Je! Waweza Kumtumikia Yehova Ukiwa Painia?” Mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Hoji kijana ambaye ni painia wa kawaida au mhubiri aliyefanya upainia akiwa kijana. Kazia jinsi wazazi na wengine wanavyoweza kutia moyo vijana wafikie lengo lao la kufanya upainia. Wavutie wote kwa uchangamfu wafikirie kwa uzito uwezo wao mbalimbali wa kushiriki katika utumishi wa wakati wote. Panga sasa ili kufanya upainia msaidizi katika Aprili.
Dak. 20: “Jenga Kupendezwa kwa Kufanya Ziara za Kurudia Zenye Matokeo.” Hotuba fupi yenye kufuatwa na wonyesho wa mazungumzo yaliyotolewa katika fungu la 3. Jinsi wakati uruhusuvyo, sehemu fulani kuu za utoaji, kama vile utangulizi au hatua ya kuelekeza kwenye andiko, vyaweza kurudiwa.
Wimbo 160 na sala ya kumalizia.