Je, Utaanzisha Funzo la Biblia Mwezi wa Oktoba?
1 Toleo la mwezi wa Oktoba ni magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ili kufuatia upendezi, tunatiwa moyo kutoa trakti Je, Ungependa Kujua Ukweli? na tujitahidi kuanzisha funzo la Biblia. Tunaweza kufanya hivyo jinsi gani tunapofanya ziara ya kurudia?
2 Jinsi ya Kutumia Trakti Hiyo: Tunaweza kusema: “Magazeti niliyokuachia yanawatia moyo watu wa tabaka na dini zote kuichunguza Biblia. [Mpe mwenye nyumba trakti Kujua Ukweli, na umwonyeshe maswali yaliyo kwenye ukurasa wa kwanza.] Haya ni baadhi ya maswali yenye kutatanisha ambayo Biblia hujibu kwa njia yenye kuridhisha. Je, umewahi kuuliza swali lolote kati ya maswali haya?” Baada ya mwenye nyumba kujibu, pitieni jibu la swali lake kwenye trakti hiyo, na msome moja ya maandiko yaliyoonyeshwa. Kisha umweleze kwamba huo ni mfano tu wa mambo ambayo Biblia hufundisha, halafu umpe kitabu Biblia Inafundisha. Baada ya kumpa kitabu, tunaweza kuzungumzia mafungu ya kwanza ya sura atakayochagua. Au tunaweza kuamua kufungua ukurasa ulio na habari zaidi kuhusu mambo tuliyozungumzia katika trakti. Tunaweza kutumia marejeo yafuatayo:
● Je, kweli Mungu anatujali? (uku. 9-11, fu. 6-10)
● Je, vita na kuteseka kutakwisha? (uku. 12, fu. 12-13)
● Ni nini kinachotupata tunapokufa? (uku. 59-60, fu. 7-8)
● Je, kuna tumaini lolote kwa wafu? (uku. 71, fu. 13-15)
● Nisali kwa njia gani ili Mungu anisikilize? (uku. 166-167, fu. 5-8)
● Nifanye nini ili nipate furaha maishani? (uku. 9, fu. 4-5)
3 Ikiwa hali hazituruhusu kuanzisha funzo kwa kutumia kitabu Biblia Inafundisha tunapomrudia mtu kwa mara ya kwanza, tunaweza kufanya mipango ili turudi na kuendeleza mazungumzo yetu. Na ikitegemea upendezi wa mtu huyo, huenda tukaamua kumtembelea mara kadhaa na kuzungumzia maswali mbalimbali kabla ya kutoa kitabu. Na tuitumie vizuri trakti hiyo nzuri katika mwezi wa Oktoba kuanzisha funzo la Biblia na kuwasaidia watu wenye mioyo minyoofu ‘kuijua kweli.’—Yoh. 8:31, 32.
[Maswali ya Funzo]
1. Tutatoa toleo gani mwezi wa Oktoba?
2. Tunaweza kutumiaje trakti Kujua Ukweli kuanzisha funzo la Biblia tunapomrudia mtu tuliyemwachia magazeti?
3. Tunaweza kubadilije njia yetu ya kuhubiri ikitegemea hali mbalimbali za watu?