KUMBUKUMBU LA TORATI
1 Haya ndiyo maneno yenye Musa aliambia Israeli wote katika eneo la Yordani katika jangwa, katika maeneo tambarare ya jangwa mbele ya Sufi, katikati ya Parani, Tofeli, Labani, Haseroti, na Dizahabu. 2 Ni safari ya siku kumi na moja (11) kutoka Horebu mupaka Kadesh-barnea+ kupitia njia ya Mulima Seiri. 3 Katika mwaka wa makumi ine (40),+ mwezi wa kumi na moja (11), siku ya kwanza ya mwezi huo, Musa akasema na Waisraeli* kulingana na mambo yote yenye Yehova alikuwa amemuagiza awaambie. 4 Hii ilikuwa kisha yeye kumushinda Sihoni+ mufalme wa Waamori, mwenye alikuwa anakaa Heshboni, na Ogu+ mufalme wa Bashani, mwenye alikuwa anakaa Ashtaroti, kule Edrei.+ 5 Katika eneo la Yordani katika inchi ya Moabu, Musa akaanza kufasiria Sheria hii,+ na kusema:
6 “Yehova Mungu wetu alituambia kule Horebu, ‘Mumekaa wakati murefu sana katika eneo hili lenye milima.+ 7 Mugeuke na kuenda katika eneo lenye milima la Waamori+ na kuelekea majirani wao wote kule Araba,+ eneo la milima, Shefela, Negebu, na eneo la pembeni ya bahari,+ inchi ya Wakanaani, na Lebanoni,*+ mupaka kwenye ule muto mukubwa, muto Efrati.+ 8 Angalia, nimeweka inchi hii mbele yenu. Muingie na kuriti inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia baba zenu, Abrahamu, Isaka,+ na Yakobo,+ wao pamoja na uzao wao* kisha wao.’+
9 “Na niliwaambia ninyi wakati huo, ‘Siwezi kuwabeba peke yangu.+ 10 Yehova Mungu wenu amewafanya muongezeke, na ninyi leo muko wengi kama nyota za mbinguni.+ 11 Yehova Mungu wa mababu zenu awafanye muongezeke+ mara elfu moja (1 000) kuliko namna muko sasa, na awabariki kama vile amewaahidi.+ 12 Namna gani mimi peke yangu ninaweza kubeba uzito wenu na mizigo yenu na ugomvi wenu?+ 13 Muchague wanaume wenye hekima, busara, na wenye uzoefu katika makabila yenu, na mimi nitawaweka kuwa vichwa juu yenu.’+ 14 Mukanijibu, ‘Jambo lenye ulituambia tufanye ni la muzuri.’ 15 Kwa hiyo nikachukua vichwa vya makabila yenu, wanaume wenye hekima na uzoefu, na nikawaweka kuwa vichwa juu yenu, wakubwa wa maelfu, wakubwa wa mamia, wakubwa wa makumi tano, wakubwa wa makumi, na maofisa wa makabila yenu.+
16 “Wakati huo niliwaagiza waamuzi wenu, ‘Wakati munasikia kesi ya hukumu kati ya ndugu zenu, munapaswa kuhukumu kwa haki+ kati ya mutu na ndugu yake ao mukaaji mugeni.+ 17 Hamupaswe kuhukumu kwa upendeleo.+ Munapaswa kusikia mudogo kama vile munasikia mukubwa.+ Musiogopeshwe na wanadamu,+ kwa sababu hukumu ni ya Mungu;+ na kama kesi ya hukumu iko nguvu sana kwenu, muilete kwangu, na nitaisikia.’+ 18 Wakati huo niliwapatia maagizo juu ya mambo yote yenye munapaswa kufanya.
19 “Kisha tukaondoka Horebu na kupita katika lile jangwa lote kubwa na lenye kuogopesha+ lenye muliona katika njia ya kuenda kwenye eneo lenye milima la Waamori,+ kama vile Yehova Mungu wetu alikuwa ametuamuru, na mwishowe tukafika Kadesh-barnea.+ 20 Halafu nikawaambia, ‘Mumefika kwenye eneo lenye milima la Waamori, lenye Yehova Mungu wetu anatupatia. 21 Angalia, Yehova Mungu wako amekupatia inchi hii. Panda, uiriti, kama vile Yehova, Mungu wa mababu zako amekuambia.+ Usiogope wala usikuwe na hofu.’
22 “Lakini, ninyi wote mulinikaribia na kusema, ‘Tutume wanaume watutangulie ili kupeleleza inchi kwa ajili yetu na watuletee habari kuhusu njia yenye tunapaswa kufuata na ni miji ya namna gani tutakuta.’+ 23 Pendekezo hilo lilionekana kuwa la muzuri kwangu, kwa hiyo nikachagua wanaume kumi na mbili (12) katikati ya wanaume wenu, mwanaume mumoja kwa ajili ya kila kabila.+ 24 Wakaondoka na kupanda kwenye eneo lenye milima,+ na wakafika kwenye Bonde* la Eshkoli na kupeleleza inchi. 25 Wakakamata matunda fulani ya inchi hiyo na kutuletea, na wakatuletea habari hii, ‘Inchi yenye Yehova Mungu wetu anatupatia ni ya muzuri.’+ 26 Lakini mulikataa kupanda, na mukaasi agizo la Yehova Mungu wenu.+ 27 Muliendelea kunungunika katika mahema yenu na mulikuwa munasema, ‘Yehova alituchukia ndiyo sababu alitutosha katika inchi ya Misri ili atutie katika mikono ya Waamori kusudi watumalize. 28 Tunaenda mahali pa namna gani? Ndugu zetu walituvunja moyo*+ kwa kusema, “Watu hao wako na nguvu na ni warefu kuliko sisi, na miji yao ni mikubwa na yenye ngome mupaka mbinguni,*+ na tuliona wana wa Anaki+ kule.”’
29 “Kwa hiyo nikawaambia, ‘Musikuwe na hofu wala musiogope kwa sababu yao.+ 30 Yehova Mungu wenu atawatangulia na kuwapigania,+ kama vile alifanya kule Misri mbele ya macho yenu wenyewe.+ 31 Na uliona katika jangwa namna Yehova Mungu wako alikubeba kama vile mutu anabeba mwana wake, kila mahali kwenye mulienda mupaka wakati mulifika mahali hapa.’ 32 Lakini ijapokuwa mambo hayo yote, hamukukuwa na imani katika Yehova Mungu wenu,+ 33 mwenye alikuwa anawatangulia katika njia, ili apeleleze mahali kwenye mutapiga kambi. Alitokea kwa moto wakati wa usiku na kwa wingu wakati wa muchana ili awaonyeshe njia yenye munapaswa kufuata.+
34 “Wakati huo wote Yehova alisikia mambo yenye mulikuwa munasema, na akakasirika na kuapa kwa uzito,+ 35 ‘Hakuna mutu hata mumoja wa kizazi hiki kiovu mwenye ataona inchi ya muzuri yenye niliapa kwamba nitapatia baba zenu,+ 36 isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune. Yeye ataiona, na nitamupatia yeye na wana wake inchi hiyo yenye alitembea juu yake, kwa sababu amemufuata Yehova kwa moyo wote.*+ 37 (Yehova alinikasirikia mimi pia kwa sababu yenu, na alisema, “Wewe pia hautaingia ndani.+ 38 Yoshua mwana wa Nuni, mwenye anasimama mbele yako,+ ndiye ataingia katika inchi hiyo.+ Umutie nguvu,*+ kwa maana atafanya Israeli ariti inchi hiyo.”) 39 Zaidi ya hayo, watoto wenu wenye mulisema watakuwa vitu vyenye vinanyanganywa katika vita+ na wana wenu wenye leo hawajue jambo la muzuri ao la mubaya, hao ndio wataingia, na nitawapatia inchi hiyo ili wairiti.+ 40 Lakini ninyi, mugeuke na kuenda katika jangwa kupitia njia ya Bahari Nyekundu.’+
41 “Basi muliniambia, ‘Tumemutendea Yehova zambi. Sasa tutapanda na kupigana, kama vile Yehova Mungu wetu ametuamuru!’ Kwa hiyo kila mumoja wenu akavaa silaha zake za vita, na mulifikiri itakuwa mwepesi kupanda katika mulima.+ 42 Lakini Yehova akaniambia, ‘Uwaambie: “Musipande na kupigana, kwa sababu sitakuwa pamoja na ninyi.+ Mukienda, mutashindwa na maadui wenu.”’ 43 Kwa hiyo nikaongea na ninyi, lakini hamukusikiliza. Lakini, muliasi agizo la Yehova na mukajaribu kwa kimbelembele kupanda katika mulima. 44 Kisha Waamori wenye walikuwa wanakaa kwenye mulima huo wakatoka ili kukutana na ninyi na wakawakimbiza ninyi kama vile nyuki wanafanya, na wakawasambaza ninyi kuanzia Seiri mupaka Horma. 45 Kwa hiyo mukarudia na kuanza kulia mbele ya Yehova, lakini Yehova hakuwasikiliza wala kuwakazia uangalifu. 46 Ndiyo sababu muliendelea kukaa Kadeshi wakati wote wenye mulikaa kule.
2 “Kisha tukageuka na kuenda katika jangwa kupitia njia ya Bahari Nyekundu, kama vile Yehova alikuwa ameniambia,+ na tulizunguka-zunguka Mulima Seiri kwa siku nyingi. 2 Mwishowe Yehova akaniambia, 3 ‘Mumezunguka-zunguka mulima huu wakati murefu sana. Sasa mugeuke kuelekea kaskazini. 4 Na uamuru watu hivi: “Mutapita karibu na mupaka wa ndugu zenu, wazao wa Esau,+ wenye wanakaa Seiri,+ na watawaogopa ninyi,+ na munapaswa kuwa waangalifu sana. 5 Musijiingize katika uadui pamoja nao,* kwa sababu sitawapatia sehemu yoyote ya inchi yao, hata mahali pa alama ya muguu, kwa sababu nimemupatia Esau Mulima Seiri kuwa eneo lake.+ 6 Munapaswa kuwapatia feza kwa ajili ya chakula chenye mutakula, na munapaswa kulipia maji yenye mutakunywa.+ 7 Kwa maana Yehova Mungu wako amekubariki katika mambo yote yenye umefanya. Anajua muzuri kabisa safari yako katika jangwa hili kubwa. Yehova Mungu wako amekuwa pamoja na wewe miaka hii makumi ine (40), na haujakosa kitu.”’+ 8 Kwa hiyo tulipita karibu na ndugu zetu, wazao wa Esau,+ wenye wanakaa Seiri, tukaepuka njia ya Araba, kutoka Elati na kutoka Esion-geberi.+
“Kisha tukageuka na kupitia njia ya jangwa la Moabu.+ 9 Halafu Yehova akaniambia, ‘Usijiingize katika uadui wala kupigana vita na Moabu, kwa sababu sitakupatia sehemu yoyote ya inchi yao kuwa eneo lako kwa sababu nimepatia wazao wa Loti inchi ya Ari kuwa eneo lao.+ 10 (Waemi+ waliishi kule zamani, walikuwa watu wenye nguvu na wengi sana na warefu kama Waanaki. 11 Warefaimu+ pia walionwa kama Waanaki,+ na Wamoabu walikuwa wanawaita Waemi. 12 Zamani, Wahori+ waliishi Seiri, lakini wazao wa Esau walikamata inchi yao na kuwaharibu na kukaa mahali pao,+ kama vile Israeli atafanya katika inchi yenye ni eneo lao, yenye hakika Yehova atawapatia.) 13 Sasa muende na muvuke Bonde* la Zeredi.’ Kwa hiyo tukavuka Bonde* la Zeredi.+ 14 Tulitembea miaka makumi tatu na munane (38) kutoka Kadesh-barnea mupaka wakati tulivuka Bonde* la Zeredi, mupaka wakati kizazi chote cha wanaume wa vita kiliangamia katika kambi, kama vile Yehova alikuwa amewaapia.+ 15 Mukono wa Yehova ulikuwa juu yao ili kuwaangamiza katika kambi mupaka wakati walikuwa wamemalizika.+
16 “Wakati tu wanaume wote wa vita walikuwa wamekufa na kumalizika kati ya watu,+ 17 Yehova akasema tena na mimi, na kuniambia, 18 ‘Leo utapita karibu na eneo la Moabu, ni kusema, Ari. 19 Wakati utafika karibu na Waamoni, usiwashambulie wala kuwachokoza, kwa sababu sitakupatia sehemu yoyote ya inchi ya Waamoni kuwa eneo lako, kwa maana nimeipatia wazao wa Loti kuwa eneo lao.+ 20 Inchi hiyo pia ilionwa kuwa inchi ya Warefaimu.+ (Warefaimu waliishi kule zamani, na Waamoni walikuwa wanawaita Wazamzumi. 21 Walikuwa watu wenye nguvu na wengi sana na warefu kama Waanaki;+ lakini Yehova aliwaharibu mbele ya Waamoni, na Waamoni wakawafukuza na kuishi mahali pao. 22 Ni vile alifanya kwa ajili ya wazao wa Esau, wenye sasa wanakaa Seiri,+ wakati aliharibu Wahori+ kutoka mbele yao, ili wakamate inchi yao na kukaa mahali pao mupaka leo. 23 Na kuhusu Waavi, walikuwa wanaishi katika makao kufikia Gaza,+ mupaka wakati Wakaftori,+ wenye walitoka Kaftori,* waliwaharibu na kukaa mahali pao.)
24 “‘Musimame, na kuvuka Bonde la Arnoni.*+ Angalia, nimemutia katika mukono wako Sihoni+ Mwamori, mufalme wa Heshboni. Kwa hiyo anza kukamata inchi yake, na upigane vita naye. 25 Leo nitaanza kufanya watu wote wenye kuwa chini ya mbingu wenye wanasikia habari zako wakuhofu na kukuogopa wewe. Watakuwa na wasiwasi na watatetemeka* kwa sababu yako.’+
26 “Kisha nilituma wajumbe kutoka katika jangwa la Kedemoti,+ mupaka kwa Mufalme Sihoni wa Heshboni, wakiwa na maneno haya ya amani,+ 27 ‘Uniruhusu nipite katika inchi yako. Nitatembea katika barabara tu na sitageuka kuenda kuume wala kushoto.+ 28 Nitakula tu chakula na kunywa tu maji yenye utanipatia ninunue. Uniruhusu tu nipite kwa miguu, 29 —ni vile wazao wa Esau wenye wanakaa Seiri na Wamoabu wenye wanakaa Ari walinifanyia—mupaka wakati nitakuwa nimevuka Yordani na kuingia katika inchi yenye Yehova Mungu wetu anatupatia sisi.’ 30 Lakini Mufalme Sihoni wa Heshboni hakuturuhusu tupite, kwa sababu Yehova Mungu wako aliacha roho yake ikuwe na kiburi+ na moyo wake ukuwe mugumu, ili amutie katika mukono wako kama vile hali iko leo.+
31 “Kisha Yehova akaniambia, ‘Angalia, tayari nimeanza kutia katika mukono wako Sihoni pamoja na inchi yake. Anza kukamata inchi yake.’+ 32 Wakati Sihoni alitoka na watu wake wote ili kupigana na sisi kule Yahazi,+ 33 Yehova Mungu wetu alimutia katika mukono wetu, kwa hiyo tukamushinda yeye, wana wake, na watu wake wote. 34 Tulikamata miji yake yote wakati huo na kuharibu kila muji, pamoja na wanaume, wanamuke, na watoto. Hatukuacha mutu yeyote aponyoke.+ 35 Tulinyanganya tu mifugo kwa ajili yetu pamoja na vitu vya miji yenye tulikuwa tumekamata. 36 Kuanzia Aroeri,+ muji wenye kuwa pembeni ya Bonde la Arnoni* (pamoja na muji wenye kuwa katika bonde), mupaka Gileadi, hakuna muji wenye hatukuweza kufikia. Yehova Mungu wetu aliitia yote katika mukono wetu.+ 37 Lakini, haukukaribia inchi ya Waamoni,+ eneo lote la pembeni ya Bonde* la Yaboki+ na miji ya eneo lenye milima, wala eneo lingine lolote lenye lilikatazwa na Yehova Mungu wetu.
3 “Kisha tuligeuka na kupanda kupitia Njia ya Bashani. Na Ogu, mufalme wa Bashani, akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana na sisi kule Edrei.+ 2 Kwa hiyo Yehova akaniambia, ‘Usimuogope, kwa maana nitamutia yeye na watu wake wote na inchi yake katika mukono wako, na utamutendea kama vile ulimutendea Sihoni mufalme wa Waamori, mwenye aliishi Heshboni.’ 3 Kwa hiyo Yehova Mungu wetu akamutia pia Mufalme Ogu wa Bashani pamoja na watu wake wote katika mukono wetu, na tukaendelea kumupiga na tukamuua mupaka hapakukuwa mutu katikati ya watu wake mwenye aliokoka. 4 Kisha tukakamata miji yake yote. Hakuna muji wao hata mumoja wenye hatukuwanyanganya—miji makumi sita (60), eneo lote la Argobu, ufalme wa Ogu katika Bashani.+ 5 Miji hiyo yote ilikuwa yenye ngome kwa sababu ya kuta za murefu, milango mikubwa, na mapingo,* na pia miji mingi sana ya mashambani. 6 Lakini, tuliwaharibu,+ kama vile tulikuwa tumemutendea Mufalme Sihoni wa Heshboni, tuliharibu kila muji, pamoja na wanaume, wanamuke, na watoto.+ 7 Na tukajikamatia mifugo yote na vitu vya miji hiyo.
8 “Wakati huo tulikamata inchi ya wafalme wawili wa Waamori+ wenye walikuwa katika eneo la Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni* mupaka Mulima Hermoni+ 9 (Wasidoni walikuwa wanaita mulima huo Sirioni na Waamori walikuwa wanauita Seniri), 10 miji yote ya eneo tambarare la juu, Gileadi yote, na Bashani yote mupaka Saleka na Edrei,+ miji ya ufalme wa Ogu katika Bashani. 11 Kwa maana Mufalme Ogu wa Bashani ndiye Murefaimu pekee mwenye alikuwa amebakia. Sanduku lake lilitengenezwa na chuma,* na lingali katika muji wa Waamoni wa Raba. Liko na urefu wa mikono* kenda (9) na upana wa mikono ine (4), kwa kipimo cha kawaida cha mukono. 12 Wakati huo tulikamata inchi hii: kuanzia Aroeri,+ muji wenye kuwa karibu na Bonde la Arnoni,* na nusu ya eneo lenye milima la Gileadi, na miji yake nimeipatia Warubeni na Wagadi.+ 13 Na nusu ya kabila la Manase+ nimeipatia sehemu yenye kubakia ya Gileadi na eneo lote la Bashani la ufalme wa Ogu. Eneo lote la Argobu, la Bashani, lilijulikana kuwa inchi ya Warefaimu.
14 “Yairi+ mwana wa Manase alikamata eneo lote la Argobu+ kufikia kwenye mupaka wa Wageshuri na Wamaakati+ na akaita vijiji hivyo vya Bashani kwa jina lake mwenyewe, Hawot-yairi,*+ mupaka leo. 15 Na Makiri+ nimemupatia Gileadi. 16 Na Warubeni na Wagadi+ nimewapatia kuanzia Gileadi mupaka kwenye Bonde la Arnoni,* katikati ya bonde ndio mupaka, kufikia Yaboki, bonde lenye ni mupaka wa Waamoni, 17 na Araba na Yordani na ule mupaka, kuanzia Kinereti kufikia kwenye Bahari ya Araba, Bahari ya Chumvi,* kwenye sehemu ya chini ya miteremuko ya Pisga kuelekea upande wa mashariki.+
18 “Kisha nikawaamuru hivi: ‘Yehova Mungu wenu amewapatia inchi hii ili ikuwe yenu. Wanaume wenu wote hodari watakamata silaha na kuvuka mbele ya ndugu zenu, Waisraeli.+ 19 Ni bibi zenu, watoto wenu, na mifugo yenu tu (ninajua muzuri kwamba muko na mifugo mingi sana) ndio wataendelea kukaa katika miji yenye nimewapatia, 20 mupaka wakati Yehova atapatia ndugu zenu pumuziko, kama vile anawafanyia ninyi, nao pia wakuwe wamekamata inchi yenye Yehova Mungu wenu atawapatia ngambo ya Yordani. Kisha mutarudia, kila mumoja kwenye eneo lake lenye nimewapatia.’+
21 “Wakati huo nilimuamuru Yoshua hivi:+ ‘Umeona na macho yako mwenyewe mambo yenye Yehova Mungu wako ametendea wafalme hao wawili. Ni vile Yehova atatendea falme zote kule kwenye utavuka kuenda.+ 22 Musiwaogope, kwa maana Yehova Mungu wenu ndiye anawapigania ninyi.’+
23 “Wakati huo nilimulilia Yehova, na kusema, 24 ‘Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, umeanza kumuonyesha mutumishi wako ukubwa wako na mukono wako wenye nguvu,+ kwa maana ni mungu gani katika mbingu ao juu ya dunia mwenye anatenda matendo yenye nguvu kama wewe?+ 25 Tafazali uniruhusu nivuke na kuona inchi ya muzuri yenye kuwa ngambo ya Yordani, eneo hili la muzuri lenye milima na Lebanoni.’+ 26 Lakini bado Yehova alikuwa amenikasirikia sana kwa sababu yenu,+ na hakutaka kunisikiliza. Tofauti na hilo, Yehova aliniambia, ‘Achia pale! Usiniambie tena juu ya jambo hili. 27 Panda kwenye kichwa cha Pisga,+ na uangalie mangaribi na kaskazini na kusini na mashariki na uone inchi hiyo na macho yako, kwa maana hautavuka hii Yordani.+ 28 Umuweke Yoshua+ katika madaraka yake na umutie moyo na kumutia nguvu, kwa sababu yeye ndiye atavuka+ mbele ya watu hawa na yeye ndiye atawafanya wariti inchi yenye utaona.’ 29 Mambo hayo yote yalitendeka wakati tulikuwa tunakaa katika bonde mbele ya Bet-peori.+
4 “Sasa, Ee Israeli, sikiliza masharti na maamuzi ya hukumu yenye ninawafundisha kushika, ili muishi+ na kuingia na kuriti inchi yenye Yehova, Mungu wa mababu zenu, anawapatia ninyi. 2 Hamupaswe kuongeza kitu kwenye neno lenye ninawaamuru, wala hamupaswe kuondoa kitu kwenye neno hilo,+ ili mushike amri za Yehova Mungu wenu zenye ninawaamuru ninyi.
3 “Macho yenu wenyewe yameona mambo yenye Yehova alitenda katika jambo la Baali wa Peori; Yehova Mungu wenu aliharibu kila mutu katikati yenu mwenye alimufuata Baali wa Peori.+ 4 Lakini ninyi wenye munashikamana kabisa na Yehova Mungu wenu, ninyi wote muko wazima leo. 5 Angalia, nimewafundisha masharti na maamuzi ya hukumu,+ kama vile Yehova Mungu wangu ameniamuru, ili muyashike katika inchi yenye mutariti. 6 Munapaswa kuyafuata kwa uangalifu,+ kwa sababu hilo litaonyesha kwamba muko na hekima+ na uelewaji+ mbele ya vikundi vya watu vyenye vitasikia kuhusu masharti haya yote, na watasema, ‘Kwa kweli taifa hili kubwa ni taifa la watu wenye hekima na uelewaji.’+ 7 Kwa maana ni taifa gani kubwa lenye miungu yake iko karibu nalo kama vile Yehova Mungu wetu iko* karibu na sisi kila wakati wenye tunamuitia?+ 8 Na ni taifa gani kubwa lenye liko na masharti na maamuzi ya hukumu yenye haki kama Sheria hii yote yenye ninatia mbele yenu leo?+
9 “Lakini tu ukuwe muangalifu na ujiangalie sana,* ili usisahau mambo yenye macho yako yameona na ili yasitoke katika moyo wako siku zote za maisha yako. Unapaswa pia kuyajulisha wana wako na wajukuu wako.+ 10 Siku yenye ulisimama mbele ya Yehova Mungu wako kule Horebu, Yehova aliniambia, ‘Kusanya watu pamoja mbele yangu ili niwafanye wasikie maneno yangu,+ kusudi wajifunze kuniogopa+ siku zote zenye wataishi juu ya udongo na kusudi wafundishe wana wao.’+
11 “Kwa hiyo mulikaribia na kusimama kwenye sehemu ya chini ya mulima, na mulima huo ulikuwa unawaka moto mupaka kwenye mbingu zenyewe;* kulikuwa giza, wingu, weusi muzito.+ 12 Na Yehova akaanza kusema na ninyi kutoka katika moto.+ Mulisikia sauti ya maneno, lakini hamukuona umbo lolote+—kulikuwa sauti tu.+ 13 Na akawatangazia agano lake,+ lenye aliwaamuru mushike—zile Amri Kumi (10).*+ Kisha, akaziandika kwenye mabamba mbili ya majiwe.+ 14 Wakati huo Yehova aliniamuru niwafundishe masharti na maamuzi ya hukumu yenye munapaswa kushika katika inchi yenye mutaingia ili kuiriti.
15 “Kwa hiyo, mujiangalie sana*—kwa sababu hamukuona umbo lolote siku yenye Yehova alisema na ninyi kule Horebu kutoka katikati ya moto— 16 ili musitende kwa upotovu kwa kujitengenezea sanamu ya kuchongwa yenye umbo ya mufano wowote, mufano wa mwanaume ao mwanamuke,+ 17 mufano wa munyama yeyote wa dunia ao mufano wa ndege yeyote mwenye anaruka katika anga,+ 18 mufano wa kitu chochote chenye kinatambaa juu ya udongo ao mufano wa samaki yeyote mwenye kuwa ndani ya maji chini ya dunia.+ 19 Na wakati unainua macho yako kuangalia mbinguni na kuona jua na mwezi na nyota—jeshi lote la mbinguni—usishawishiwe na kuviinamia na kuvitumikia.+ Yehova Mungu wako amevipatia vikundi vyote vya watu vyenye kuwa chini ya mbingu zote. 20 Lakini ninyi ndio watu wenye Yehova alichukua na kuwatosha katika tanuru ya kuyeyushia chuma, katika Misri, ili mukuwe watu wenye ni mali yake mwenyewe,*+ kama vile muko leo.
21 “Yehova alinikasirikia kwa sababu yenu,+ na akaapa kwamba sitavuka Yordani ao kuingia katika inchi ya muzuri yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti.+ 22 Kwa maana nitakufa katika inchi hii; sitavuka Yordani,+ lakini ninyi mutavuka na kuriti inchi hiyo ya muzuri. 23 Mukuwe waangalifu ili musisahau agano la Yehova Mungu wenu lenye alifanya pamoja na ninyi,+ na musijitengenezee sanamu ya kuchongwa, umbo ya kitu chochote chenye Yehova Mungu wako alikukataza.+ 24 Kwa maana Yehova Mungu wako ni moto wenye kuteketeza,+ Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu.+
25 “Kama unazaa wana na wajukuu na kama mumeishi wakati murefu katika inchi na munatenda kwa uharibifu na kutengeneza sanamu ya kuchongwa+ ya aina yoyote na munatenda uovu mbele ya macho ya Yehova Mungu wako na hivyo kumukasirisha,+ 26 ninachukua mbingu na dunia kuwa mashahidi juu yenu leo kwamba hakika mutaharibiwa haraka katika inchi yenye munavuka Yordani ili kuiriti. Hamutaishi wakati murefu katika inchi hiyo, lakini mutaharibiwa kabisa.+ 27 Yehova atawasambaza kati ya vikundi vya watu,+ na ni watu kidogo tu kati yenu ndio wataokoka+ kati ya mataifa kwenye Yehova atakuwa amewafukuzia. 28 Kule mutalazimika kutumikia miungu ya miti na ya majiwe yenye ilitengenezwa na mikono ya wanadamu,+ miungu yenye haiwezi kuona wala kusikia wala kula wala kunusa.
29 “Kama munatafuta Yehova Mungu wako mukiwa kule, hakika mutamupata,+ kama unamutafuta kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote.+ 30 Wakati utakuwa katika mateso makubwa na mambo hayo yote yakuwe yamekupata katika siku zenye kuja, basi utamurudilia Yehova Mungu wako na kusikiliza sauti yake.+ 31 Kwa maana Yehova Mungu wako ni Mungu mwenye rehema.+ Hatakuacha wala kukuharibu wala kusahau agano lenye aliapia mababu zako.+
32 “Sasa, uliza, kuhusu siku za zamani mbele ya wakati wako, kuanzia siku yenye Mungu aliumba mwanadamu juu ya dunia; tafuta kuanzia mwisho mumoja wa mbingu mupaka mwisho mwingine wa mbingu. Je, kuko jambo lolote kubwa kama hili lenye limekwisha kutokea ao kuko jambo lolote kama hili lenye limekwisha kusikiwa?+ 33 Je, kuko taifa lingine lolote lenye limekwisha kusikia sauti ya Mungu ikisema kutoka katika moto kama vile wewe uliisikia na kuendelea kuishi?+ 34 Ao je, Mungu amekwisha kujaribu kujichukulia taifa katikati ya taifa lingine kwa hukumu,* kwa alama, kwa miujiza,+ kwa vita,+ kwa mukono wenye nguvu,+ kwa mukono wenye kunyooshwa, na kwa matendo ya kuogopesha sana,+ kama vile Yehova Mungu wenu aliwafanyia kule Misri mbele ya macho yenu wenyewe? 35 Ninyi wenyewe mumeonyeshwa mambo hayo ili mujue kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli;+ hakuna mwingine isipokuwa yeye.+ 36 Alikufanya usikie sauti yake kutoka mbinguni ili akurekebishe, na katika dunia alikufanya uone moto wake mukubwa, na maneno yake uliyasikia kutoka katika moto.+
37 “Kwa sababu alipenda mababu zako na amechagua uzao wao* kisha wao,+ ulitoshwa Misri kwa nguvu zake kubwa mbele ya macho yake. 38 Alifukuza mbele yako mataifa makubwa sana na yenye nguvu sana kuliko wewe, ili akuingize na kukupatia inchi yao kuwa uriti, kama vile hali iko leo.+ 39 Kwa hiyo, siku ya leo, ujue na utie katika moyo wako kwamba Yehova ndiye Mungu wa kweli juu mbinguni na chini duniani.+ Hakuna mwingine.+ 40 Unapaswa kushika masharti yake na amri zake zenye ninakuamuru leo, ili mambo yakuendee muzuri wewe na wana wako kisha wewe, kusudi ubakie wakati murefu katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia.”+
41 Wakati huo Musa alitia pembeni miji tatu (3) upande wa mashariki wa Yordani.+ 42 Kama muuaji yeyote anaua mwanadamu mwenzake bila kukusudia na hakumuchukia zamani,+ anapaswa kukimbilia katika muji mumoja kati ya miji hiyo na kuishi.+ 43 Miji hiyo ni Beseri+ katika jangwa kwenye eneo tambarare la juu kwa ajili ya Warubeni, Ramoti+ katika Gileadi kwa ajili ya Wagadi, na Golani+ katika Bashani kwa ajili ya Wamanase.+
44 Sasa hiyo ndiyo Sheria+ yenye Musa alitia mbele ya watu wa Israeli. 45 Hivi ni vikumbusho, masharti, na maamuzi ya hukumu yenye Musa alipatia Waisraeli kisha wao kutoka Misri,+ 46 katika eneo la Yordani, katika bonde lenye kuwa ngambo ingine ya Bet-peori,+ katika inchi ya Mufalme Sihoni wa Waamori, mwenye alikuwa anakaa Heshboni,+ mwenye Musa na Waisraeli walimushinda kisha kutoka Misri.+ 47 Na wakakamata inchi yake na inchi ya Mufalme Ogu+ wa Bashani, wafalme wawili wa Waamori wenye walikuwa katika eneo la upande wa mashariki wa Yordani, 48 kuanzia Aroeri,+ yenye kuwa kwenye mupaka wa Bonde la Arnoni,* kufikia kwenye Mulima Sioni, ni kusema, Hermoni,+ 49 na Araba yote katika eneo la mashariki ya Yordani, mupaka Bahari ya Araba,* kwenye sehemu ya chini ya miteremuko ya Pisga.+
5 Kisha Musa akaita Israeli wote na kuwaambia: “Sikia, Ee Israeli, masharti na maamuzi ya hukumu yenye ninakutangazia leo, na unapaswa kujifunza na kushika kwa uangalifu masharti na maamuzi hayo ya hukumu. 2 Yehova Mungu wetu alifanya agano pamoja na sisi katika Horebu.+ 3 Yehova hakufanya agano hilo pamoja na mababu zetu, lakini pamoja na sisi, sisi wote wenye kuwa wazima hapa leo. 4 Yehova alisema na ninyi uso kwa uso katika mulima, kutoka katika moto.+ 5 Nilisimama katikati yenu na Yehova wakati huo+ ili niwaambie neno la Yehova, kwa maana muliogopa kwa sababu ya moto na hamukupanda katika mulima.+ Alisema:
6 “‘Mimi ni Yehova Mungu wako, mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa.+ 7 Haupaswe hata kidogo kuwa na miungu mingine isipokuwa mimi.*+
8 “‘Haupaswe kujifanyia sanamu ya kuchongwa+ wala umbo ya* kitu chochote chenye kuwa juu mbinguni ao chenye kuwa hapa chini juu ya dunia ao chenye kuwa ndani ya maji chini ya dunia. 9 Haupaswe kuviinamia wala kushawishiwa kuvitumikia,+ kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu,+ mwenye analeta azabu juu ya wana kwa sababu ya kosa la baba, juu ya kizazi cha tatu (3) na juu ya kizazi cha ine (4) cha wale wenye kunichukia,+ 10 lakini mwenye kuonyesha upendo mushikamanifu* kwa kizazi cha elfu (1 000) cha wale wenye kunipenda na kushika amri zangu.
11 “‘Haupaswe kutumia jina la Yehova Mungu wako kwa njia yenye haifae,+ kwa maana Yehova hatakosa kumupatia azabu mutu yeyote mwenye anatumia jina lake kwa njia yenye haifae.+
12 “‘Shika siku ya Sabato ili uione kuwa takatifu, kama vile Yehova Mungu wako alikuamuru.+ 13 Utatumika na kufanya kazi zako zote kwa siku sita (6),+ 14 lakini siku ya saba (7) ni sabato kwa ajili ya Yehova Mungu wako.+ Haupaswe kufanya kazi yoyote,+ wewe, wala mutoto wako mwanaume wala mutoto wako mwanamuke wala mutumwa wako mwanaume wala mutumwa wako mwanamuke wala ngombe-dume wako wala punda wako wala munyama yeyote katikati ya wanyama wako wa kufugwa wala mukaaji mugeni mwenye kuwa katika miji yako,*+ ili mutumwa wako mwanaume na mutumwa wako mwanamuke wapumuzike kama wewe.+ 15 Kumbuka kwamba ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri na kwamba Yehova Mungu wako alikutosha kule kwa mukono wenye nguvu na mukono wenye kunyooshwa.+ Ndiyo sababu Yehova Mungu wako alikuamuru ushike siku ya Sabato.
16 “‘Heshimia baba yako na mama yako,+ kama vile Yehova Mungu wako amekuamuru, ili uishi wakati murefu na kufanikiwa* katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia.+
17 “‘Haupaswe kuua.+
18 “‘Wala haupaswe kufanya uzinifu.+
19 “‘Wala haupaswe kuiba.+
20 “‘Wala haupaswe kutoa ushahidi wa uongo juu ya mwenzako.+
21 “‘Wala haupaswe kutamani bibi ya mwenzako.+ Wala haupaswe kutamani kwa uchoyo nyumba ya mwenzako wala shamba lake wala mutumwa wake mwanaume wala mutumwa wake mwanamuke wala ngombe-dume wake wala punda wake wala kitu chochote cha mwenzako.’+
22 “Yehova aliambia kutaniko lenu lote amri* hizo kwenye mulima, kutoka katika moto, wingu, na giza nzito,+ kwa sauti kubwa, na hakuongeza jambo lolote; kisha akaziandika kwenye mabamba mbili ya majiwe na kunipatia.+
23 “Lakini wakati tu mulisikia sauti kutoka katika lile giza, wakati mulima ulikuwa unawaka moto,+ vichwa vyote vya makabila yenu na wazee wakanikaribia. 24 Kisha mukasema, ‘Angalia, Yehova Mungu wetu ametuonyesha utukufu wake na ukubwa wake, na tumesikia sauti yake kutoka katika moto.+ Leo tumeona kwamba Mungu anaweza kuongea na mwanadamu na mwanadamu huyo anaweza kuendelea kuishi.+ 25 Sasa, sababu gani tukufe? Kwa maana moto huu mukubwa unaweza kututeketeza. Kama tunaendelea kusikia sauti ya Yehova Mungu wetu, hakika tutakufa. 26 Kwa maana ni nani kati ya miili yote* mwenye amesikia sauti ya Mungu mwenye kuishi ikiongea kutoka katika moto kama vile tulisikia na bado anaendelea kuishi? 27 Wewe mwenyewe unapaswa kuenda karibu ili usikie mambo yote yenye Yehova Mungu wetu atasema, na ni wewe utatuambia mambo yote yenye Yehova Mungu wetu anakuambia, na sisi tutasikiliza na kuyatenda.’+
28 “Kwa hiyo Yehova alisikia maneno yenye muliniambia, na Yehova akaniambia, ‘Nimesikia maneno yenye watu hawa wamekuambia. Mambo yote yenye wamesema ni sawa.+ 29 Kama tu wangekuwa sikuzote na moyo wenye muelekeo wa kuniogopa+ na kushika amri zangu zote,+ basi mambo yangewaendea muzuri wao na wana wao milele!+ 30 Uende uwaambie: “Murudie kwenye mahema yenu.” 31 Lakini unapaswa kubakia hapa pamoja na mimi, na uache nikuambie amri zote, masharti, na maamuzi ya hukumu yenye unapaswa kuwafundisha na yenye wanapaswa kushika katika inchi yenye ninawapatia ili wairiti.’ 32 Sasa ninyi watu munapaswa kuwa waangalifu kufanya kama vile Yehova Mungu wenu amewaamuru.+ Musigeuke kuenda kuume wala kushoto.+ 33 Munapaswa kutembea katika njia yote yenye Yehova Mungu wenu amewaamuru,+ ili muishi na kufanikiwa na kurefusha siku zenu katika inchi yenye mutariti.+
6 “Sasa hizi ni amri, masharti, na maamuzi ya hukumu yenye Yehova Mungu wenu ametoa ili kuwafundisha, ili muvishike wakati munavuka kuingia katika inchi yenye mutariti, 2 ili umuogope Yehova Mungu wako na kushika sheria zake zote na amri zake zenye ninakuamuru—wewe na mwana wako na mujukuu wako+—siku zote za maisha yako, ili uishi wakati murefu.+ 3 Na unapaswa kusikiliza, Ee Israeli, na kuzishika kwa uangalifu, ili ufanikiwe na mukuwe wengi sana katika inchi yenye kutiririka maziwa na asali, kama vile Yehova, Mungu wa mababu zako, amekuahidi.
4 “Sikiliza, Ee Israeli: Yehova Mungu wetu ni Yehova mumoja.+ 5 Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote+ na kwa nguvu zako zote.*+ 6 Maneno haya yenye ninakuamuru leo yanapaswa kuwa kwenye moyo wako, 7 na unapaswa kuyakazia katika* wana wako+ na kuongea kuyahusu wakati unakaa katika nyumba yako na wakati unatembea katika barabara na wakati unalala na wakati unaamuka.+ 8 Uyafunge kuwa kikumbusho kwenye mukono wako, na yanapaswa kuwa kama utepe wa kichwa kwenye paji la uso wako.*+ 9 Uyaandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na kwenye milango yako mikubwa.
10 “Wakati Yehova Mungu wako atakuingiza katika inchi yenye aliapia mababu zako Abrahamu, Isaka, na Yakobo kwamba atakupatia+—miji mikubwa na yenye kupendeza yenye haukujenga,+ 11 nyumba zenye kujaa vitu vya muzuri vya namna mbalimbali vyenye haukufanya kazi ili kuvipata, matangi yenye haukuchimba, na mashamba ya mizabibu na mizeituni yenye haukupanda—na wakati utakuwa umekula na kushiba,+ 12 ukuwe muangalifu ili usimusahau Yehova,+ mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. 13 Unapaswa kumuogopa Yehova Mungu wako,+ na unapaswa kumutumikia,+ na unapaswa kuapa kwa jina lake.+ 14 Hamupaswe kufuata miungu mingine, miungu yoyote ya vikundi vya watu vyenye kuwazunguka pande zote,+ 15 kwa maana Yehova Mungu wako mwenye kuwa katikati yako ni Mungu mwenye anataka watu washikamane na yeye tu.+ Kama haufanye vile, kasirani ya Yehova Mungu wako itawaka juu yako+ na atakuharibu usikuwe tena juu ya uso wa dunia.+
16 “Hamupaswe kumujaribu Yehova Mungu wenu+ kama vile mulimujaribu kule Masa.+ 17 Munapaswa kushika kwa bidii amri za Yehova Mungu wenu na vikumbusho vyake na masharti yake yenye amewaamuru mushike. 18 Unapaswa kufanya mambo yenye kuwa sawa na ya muzuri mbele ya macho ya Yehova, ili ufanikiwe na ili uingie na kuriti inchi ya muzuri yenye Yehova aliapia mababu zako,+ 19 kwa kufukuza maadui wako wote mbele yako, kama vile Yehova ameahidi.+
20 “Wakati wenye kuja, wakati mwana wako atakuuliza, ‘Ni nini maana ya vikumbusho, masharti, na maamuzi ya hukumu yenye Yehova Mungu wetu amewaamuru?’ 21 basi utamuambia mwana wako, ‘Tulikuwa watumwa wa Farao katika Misri, lakini Yehova alitutosha Misri kwa mukono wenye nguvu. 22 Kwa hiyo mbele ya macho yetu Yehova aliendelea kutuma alama na miujiza, mikubwa na yenye kuleta uharibifu, juu ya Misri,+ juu ya Farao, na juu ya nyumba yake yote.+ 23 Na alitutosha kule ili atulete hapa na kutupatia inchi yenye alikuwa ameapia mababu zetu.+ 24 Kisha Yehova akatuamuru tufuate masharti hayo yote na kumuogopa Yehova Mungu wetu kwa faida yetu ya kudumu,+ ili tuendelee kuishi,+ kama vile tuko leo. 25 Na hilo litamaanisha haki kwa ajili yetu ikiwa tunashika kwa uangalifu amri hizo zote ili kumutii* Yehova Mungu wetu, kama vile ametuamuru.’+
7 “Wakati Yehova Mungu wako atakuingiza katika inchi yenye unakaribia kuingia na kuriti,+ ataondoa pia mataifa yenye watu wengi mbele yako:+ Wahiti, Wagirgashi, Waamori,+ Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ mataifa saba (7) yenye watu wengi zaidi na yenye nguvu kuliko wewe.+ 2 Yehova Mungu wako atawatia katika mukono wako, na utawashinda.+ Unapaswa kuwaharibu kabisa.+ Haupaswe kufanya agano lolote pamoja nao wala kuwaonyesha wema wowote.+ 3 Haupaswe kufanya mapatano yoyote ya ndoa pamoja* nao. Watoto wako wanamuke usiwapatie watoto wao wanaume wala usikamate watoto wao wanamuke kwa ajili ya watoto wako wanaume.+ 4 Kwa maana watageuza watoto wenu wanaume waache kunifuata ili kutumikia miungu mingine;+ kisha kasirani ya Yehova itawaka juu yenu, na atawaharibu haraka.+
5 “Lakini, ni hivi mutawatendea: Mubomoe mazabahu zao, muvunje nguzo zao takatifu,+ mukate miti yao mitakatifu,*+ na kuteketeza kwa moto sanamu zao za kuchongwa.+ 6 Kwa maana wewe ni kikundi cha watu watakatifu kwa ajili ya Yehova Mungu wako, na Yehova Mungu wako amekuchagua kuwa kikundi chake cha watu, mali yake ya pekee,* katikati ya vikundi vyote vya watu vyenye kuwa juu ya uso wa dunia.+
7 “Yehova hakuwaonyesha upendo na kuwachagua kwa sababu mulikuwa wengi sana kuliko vikundi vyote vya watu,+ kwa maana mulikuwa taifa la kidogo sana kati ya vikundi vyote vya watu.+ 8 Lakini, ni kwa sababu Yehova anawapenda na kwa sababu alishika kiapo chenye aliapia mababu zenu+ ndiyo maana Yehova aliwatosha kwa mukono wake wenye nguvu, ili kuwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa,+ kutoka katika mamlaka* ya Farao mufalme wa Misri. 9 Unajua muzuri kwamba Yehova Mungu wako ndiye Mungu wa kweli, Mungu muaminifu, mwenye kushika agano lake na upendo mushikamanifu kufikia vizazi elfu (1 000) vya wale wenye kumupenda na kushika amri zake.+ 10 Lakini wale wenye kumuchukia atawalipa uharibifu kwenye uso wao.+ Hatakawia kushugulika na wale wenye kumuchukia; atawalipa kwenye uso wao. 11 Kwa hiyo, ukuwe muangalifu kushika amri na masharti na maamuzi ya hukumu yenye ninakuamuru leo, kwa kuyashika.
12 “Kama munaendelea kusikiliza maamuzi hayo ya hukumu na kuyashika na kuyatenda, Yehova Mungu wako atashika lile agano na upendo mushikamanifu wenye aliapia mababu zako. 13 Atakupenda na kukubariki na kukufanya uongezeke. Ndiyo, atakubariki kwa kukupatia watoto wengi*+ na kwa kukupatia mazao ya udongo wako, nafaka yako, divai yako mupya, mafuta yako,+ vitoto vya mifugo yako na vitoto vya makundi yako, katika inchi yenye aliapia mababu zako kwamba atakupatia.+ 14 Utabarikiwa kuliko vikundi vyote vya watu;+ hakuna mwanaume ao mwanamuke kati yako mwenye atakosa mutoto, wala mifugo yako haitakosa kuzaa.+ 15 Yehova atakuondolea magonjwa yote, na hatakuletea ugonjwa wowote hatari wenye ulijua kule Misri.+ Lakini, ataletea magonjwa hayo wale wote wenye kukuchukia. 16 Utaharibu* vikundi vyote vya watu vyenye Yehova Mungu wako atatia katika mukono wako.+ Haupaswe* kuvihurumia,+ na haupaswe kutumikia miungu yao,+ kwa sababu jambo hilo litakuwa mutego kwako.+
17 “Kama utasema katika moyo wako, ‘Mataifa haya yako na watu wengi kuliko sisi. Namna gani nitaweza kuyafukuza?’+ 18 haupaswe kuyaogopa.+ Unapaswa kujikumbusha mambo yenye Yehova Mungu wako alimutendea Farao na Misri yote,+ 19 zile hukumu kubwa zenye* macho yako yaliona na zile alama na miujiza+ na mukono wenye nguvu na mukono wenye kunyooshwa wenye Yehova Mungu wako alikutosha nao.+ Ni vile Yehova Mungu wako atatendea vikundi vyote vya watu vyenye unaogopa.+ 20 Yehova Mungu wako atatuma hisia ya kuvunjika moyo* juu yao mupaka wale wenye walikuwa wamebakia+ na wenye walikuwa wanajificha wakuwe wameangamia. 21 Usiogope kwa sababu yao, kwa maana Yehova Mungu wako iko* pamoja na wewe,+ Mungu mukubwa na mwenye kuogopesha sana.+
22 “Hakika Yehova Mungu wako atafukuza mataifa haya mbele yako hatua kwa hatua.+ Hautaruhusiwa kuyamaliza haraka, ili wanyama wa pori wasiongezeke na kukushambulia. 23 Yehova Mungu wako atayatia katika mukono wako na kushinda kabisa mataifa hayo mupaka yaharibiwe.+ 24 Atatia wafalme wa mataifa hayo katika mukono wako,+ na utafuta majina yao chini ya mbingu.+ Hakuna mutu mwenye atasimama mbele yako,+ mupaka wakati utakuwa umewaharibu.+ 25 Utateketeza sanamu za kuchongwa za miungu yao ndani ya moto.+ Usitamani feza na zahabu ya sanamu hizo wala usiikamate ili ikuwe yako,+ ili usinaswe katika mutego wake, kwa maana ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.+ 26 Haupaswe kuingiza kitu chenye kuchukiza ndani ya nyumba yako na hivyo ukuwe kama kitu hicho chenye kinapaswa kuharibiwa. Unapaswa kukichukia kabisa na kukichukia sana, kwa sababu ni kitu chenye kinapaswa kuharibiwa.
8 “Munapaswa kuwa waangalifu ili kushika kila amri yenye ninakupatia leo, ili muendelee kuishi+ na kuongezeka na kuingia na kuriti inchi yenye Yehova aliapia mababu zenu.+ 2 Kumbuka njia ya murefu yenye Yehova Mungu wako alikufanya utembee ndani miaka hii makumi ine (40) katika jangwa,+ ili akunyenyekeze na kukujaribu+ kusudi ajue mambo yenye yalikuwa katika moyo wako,+ kama utashika amri zake ao hapana. 3 Kwa hiyo alikunyenyekeza na kukuacha usikie njaa+ na alikukulisha mana,+ yenye wewe haukujua wala baba zako hawakujua, ili akufundishe kwamba mwanadamu haishi kwa mukate tu lakini mwanadamu anaishi kwa kila neno lenye linatoka katika kinywa cha Yehova.+ 4 Nguo yenye ulivaa haikuzeeka, wala miguu yako haikuvimba miaka hiyo makumi ine (40).+ 5 Unajua muzuri katika moyo wako kwamba kama vile mutu anamurekebisha mwana wake, Yehova Mungu wako alikuwa anakurekebisha.+
6 “Sasa unapaswa kushika amri za Yehova Mungu wako kwa kutembea katika njia zake na kumuogopa. 7 Kwa maana Yehova Mungu wako anakuingiza katika inchi ya muzuri,+ inchi yenye mito midogo ya maji,* mabubujiko na chemchemi zenye kutiririka* katika bonde tambarare na katika eneo lenye milima, 8 inchi ya ngano na shayiri, ya mizabibu, miti ya tini, na matunda ya makomamanga,+ inchi ya mafuta ya zeituni na asali,+ 9 inchi yenye haitakuwa na upungufu wa chakula na hautakosa kitu, inchi yenye majiwe yake iko na chuma ndani na katika milima yake utachimba shaba.
10 “Wakati utakuwa umekula na kushiba, unapaswa kumusifu Yehova Mungu wako kwa sababu ya inchi ya muzuri yenye amekupatia.+ 11 Ukuwe muangalifu ili usimusahau Yehova Mungu wako kwa kukosa kushika amri zake, maamuzi yake ya hukumu, na sheria zake zenye ninakuamuru leo. 12 Wakati utakula na kushiba na kujenga nyumba za muzuri na kukaa ndani yazo,+ 13 wakati mifugo yako na makundi yako yataongezeka na feza na zahabu yako kuwa nyingi na wakati utakuwa na kila kitu kwa wingi, 14 usiache moyo wako ukuwe na majivuno+ na kukufanya umusahau Yehova Mungu wako, mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa,+ 15 mwenye alikufanya utembee katika jangwa kubwa na lenye kuogopesha,+ lenye nyoka wenye sumu na nge na udongo wenye kukauka wenye hauna maji. Alifanya maji yatiririke kutoka katika jiwe ngumu+ 16 na alikukulisha mana+ katika jangwa, yenye baba zako hawakujua, ili akunyenyekeze+ na kukujaribu kusudi upate faida katika siku zenye kuja.+ 17 Kama utasema katika moyo wako, ‘Uwezo wangu mwenyewe na nguvu ya mukono wangu mwenyewe vimenipatia utajiri huu,’+ 18 kumbuka kwamba Yehova Mungu wako ndiye anakupatia nguvu ya kupata utajiri,+ ili atimize agano lake lenye aliapia mababu zako, kama vile leo.+
19 “Kama siku moja utamusahau Yehova Mungu wako na kufuata miungu mingine na kuitumikia na kuiinamia, ninashuhudia juu yenu leo kwamba hakika mutaangamia.+ 20 Kama vile mataifa yenye Yehova anaharibu mbele yenu, ni vile mutaangamia, kwa sababu hamukusikiliza sauti ya Yehova Mungu wenu.+
9 “Sikia, Ee Israeli, leo unavuka Yordani+ ili kuingia na kukamata inchi ya mataifa makubwa na yenye nguvu kuliko wewe,+ miji mikubwa na yenye ngome zenye kufika mbinguni,*+ 2 watu wenye nguvu na warefu, wana wa Waanaki,+ wenye unajua na umesikia watu wanasema kuwahusu: ‘Ni nani anaweza kusimama mbele ya wana wa Anaki?’ 3 Kwa hiyo, unapaswa kujua leo kwamba Yehova Mungu wako atavuka mbele yako.+ Yeye ni moto wenye kuteketeza,+ na atawaharibu. Atawanyenyekeza mbele ya macho yako ili uwafukuze haraka* na kuwaharibu, kama vile Yehova amekuahidi.+
4 “Usiseme katika moyo wako wakati Yehova Mungu wako atawafukuza mbele yako, ‘Ni kwa sababu ya haki yangu ndiyo maana Yehova amenileta ili niriti inchi hii.’+ Lakini, ni kwa sababu ya uovu wa mataifa hayo+ ndiyo maana Yehova anayafukuza mbele yako. 5 Haiko kwa sababu ya haki yako ao unyoofu wa moyo wako ndiyo maana unaingia ili kuriti inchi yao. Lakini, ni kwa sababu ya uovu wa mataifa hayo ndiyo maana Yehova Mungu wako anayafukuza mbele yako+ na ili kutimiza neno lenye Yehova aliapia mababu zako, Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+ 6 Basi, ujue kwamba haiko kwa sababu ya haki yako ndiyo maana Yehova Mungu wako anakupatia inchi hii ya muzuri ili uiriti; kwa sababu ninyi ni watu wenye kuwa kichwa-nguvu.*+
7 “Kumbuka—usisahau hata kidogo—namna ulimuchokoza Yehova Mungu wako katika jangwa.+ Tangu siku yenye ulitoka katika inchi ya Misri mupaka wakati mulifika mahali hapa, mumemuasi Yehova.+ 8 Hata katika Horebu mulimuchokoza Yehova, na Yehova aliwakasirikia sana na hivyo alikuwa tayari kuwaharibu.+ 9 Wakati nilipanda mulima ili kupokea yale mabamba ya majiwe,+ mabamba ya agano lenye Yehova alifanya pamoja na ninyi,+ nilibakia kwenye mulima siku makumi ine (40) muchana na usiku,+ sikukula chakula wala kunywa maji. 10 Kisha Yehova akanipatia yale mabamba mbili ya majiwe yenye yaliandikwa na kidole cha Mungu, na juu yake kulikuwa maneno yote yenye Yehova alikuwa amewaambia kwenye mulima kutoka katika moto siku ya mukusanyiko.*+ 11 Kwenye mwisho wa zile siku makumi ine (40) muchana na usiku, Yehova alinipatia yale mabamba mbili ya majiwe, yale mabamba ya agano, 12 na Yehova akaniambia, ‘Simama, shuka haraka kutoka hapa, kwa sababu watu wako wenye ulitosha Misri wametenda kwa upotovu.+ Wamegeuka haraka kutoka katika njia yenye niliwaamuru wafuate. Wamejitengenezea sanamu ya metali.’*+ 13 Kisha Yehova akaniambia, ‘Nimeona watu hawa, na angalia! ni watu wenye kuwa kichwa-nguvu.*+ 14 Uniache, na nitawaharibu na kufuta jina lao chini ya mbingu, na acha nikufanye wewe kuwa taifa lenye nguvu na lenye watu wengi kuliko wao.’+
15 “Kisha nikageuka na kushuka mulima wakati mulima ulikuwa unawaka moto,+ na yale mabamba mbili ya agano yalikuwa katika mikono yangu mbili.+ 16 Kisha nikaangalia na kuona kwamba mulikuwa mumemutendea Yehova Mungu wenu zambi! Mulikuwa mumejitengenezea kitoto-dume cha ngombe cha metali.* Mulikuwa mumegeuka haraka kutoka katika njia yenye Yehova alikuwa amewaamuru mufuate.+ 17 Kwa hiyo nikashika yale mabamba mbili na kuyatupa chini kwa mikono yangu mbili na kuyavunja-vunja mbele ya macho yenu.+ 18 Kisha nikainama uso chini mbele ya Yehova kwa siku makumi ine (40), muchana na usiku, kama mara ya kwanza. Sikukula chakula wala kunywa maji,+ kwa sababu ya zambi zote zenye mulikuwa mumetenda kwa kufanya uovu mbele ya macho ya Yehova na kumukasirisha. 19 Kwa maana niliogopa sana kwa sababu ya kasirani kubwa ya Yehova juu yenu,+ kwa maana alikuwa tayari kuwaharibu. Lakini, Yehova alinisikiliza wakati huo pia.+
20 “Yehova alimukasirikia sana Haruni na hivyo alikuwa tayari kumuharibu,+ lakini nilimulilia Mungu* kwa ajili ya Haruni wakati huo pia. 21 Kisha nikakamata kile kitu cha zambi chenye mulitengeneza, kile kitoto-dume cha ngombe,+ na kukiteketeza ndani ya moto; nikakiponda na kukisagasaga kabisa mupaka kikakuwa laini kama mavumbi, na nikatupa mavumbi hayo katika muto mudogo wenye kutiririka kutoka kwenye mulima.+
22 “Tena, mulimukasirisha pia Yehova kule Tabera,+ kule Masa,+ na kule Kibrot-hataava.+ 23 Wakati Yehova aliwatuma kutoka Kadesh-barnea+ na kuwaambia, ‘Mupande na kuriti inchi yenye hakika nitawapatia!’ muliasi tena agizo la Yehova Mungu wenu,+ na hamukuonyesha imani+ katika yeye na hamukumutii. 24 Mumemuasi Yehova tangu nimewajua.
25 “Kwa hiyo niliendelea kuinama uso chini mbele ya Yehova siku makumi ine (40),+ muchana na usiku, kwa maana niliinamisha uso mupaka chini kwa njia hiyo kwa sababu Yehova alisema atawaharibu. 26 Nikaanza kumulilia* Yehova na kusema, ‘Ee Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, usiharibu watu hawa. Wao ni mali yako mwenyewe,*+ watu wenye ulikomboa kwa ukubwa wako na kuwatosha Misri kwa mukono wenye nguvu.+ 27 Kumbuka watumishi wako Abrahamu, Isaka, na Yakobo.+ Usikazie uangalifu ugumu wa moyo wa watu hawa, uovu wao, na zambi yao.+ 28 Kama unafanya vile watu wa inchi kwenye ulitutosha wanaweza kusema: “Yehova hakuweza kuwaingiza katika inchi yenye aliwaahidi, na kwa sababu aliwachukia, aliwatosha ili awaue katika jangwa.”+ 29 Kwa maana ni watu wako na mali yako mwenyewe,*+ watu wenye ulitosha kwa nguvu zako kubwa na kwa mukono wako wenye kunyooshwa.’+
10 “Wakati huo Yehova aliniambia, ‘Ujichongee mabamba mbili ya majiwe kama yale ya kwanza,+ na upande kuja kwangu kwenye mulima; unapaswa kujitengenezea pia sanduku la mbao. 2 Na nitaandika kwenye mabamba hayo maneno yenye yalikuwa kwenye yale mabamba ya kwanza, yenye ulivunja-vunja, na utatia mabamba hayo ndani ya sanduku hilo.’ 3 Kwa hiyo nikatengeneza sanduku la mbao za mugunga* na kuchonga mabamba mbili ya majiwe kama yale ya kwanza na kupanda kwenye mulima nikiwa na mabamba hayo mbili katika mukono wangu.+ 4 Kisha akaandika kwenye mabamba hayo maneno yenye alikuwa ameandika mbele,+ zile Amri Kumi (10),*+ zenye Yehova alikuwa amewaambia ninyi kwenye mulima kutoka katika moto+ siku ya mukusanyiko;*+ na Yehova akanipatia mabamba hayo. 5 Kisha nikageuka na kushuka kutoka kwenye mulima+ na kutia mabamba hayo katika sanduku lenye nilikuwa nimetengeneza, yangali ndani, kama vile Yehova alikuwa ameniamuru.
6 “Kisha Waisraeli wakaondoka Beeroti Bene-yaakani na kuenda Mosera. Haruni akakufa na kuzikwa kule,+ na Eleazari mwana wake akaanza kutumika akiwa kuhani pa nafasi yake.+ 7 Kutoka kule wakaelekea Gudgoda, na kutoka Gudgoda wakaelekea Yotbata,+ inchi yenye kutiririka mito midogo ya maji.*
8 “Wakati huo Yehova alitia pembeni kabila la Lawi+ ili libebe sanduku la agano la Yehova,+ kusudi lisimame mbele ya Yehova ili kumutolea utumishi, na kubariki katika jina lake,+ kama vile wanafanya mupaka leo. 9 Ndiyo maana Lawi hakupewa fungu wala uriti pamoja na ndugu zake. Yehova ndiye uriti wake, kama vile Yehova Mungu wako alikuwa amemuambia.+ 10 Mimi mwenyewe nilikaa kwenye mulima kama vile nilifanya mara ya kwanza, siku makumi ine (40), muchana na usiku,+ na Yehova alinisikiliza wakati huo pia.+ Yehova hakutaka kukuharibu. 11 Kisha Yehova akaniambia, ‘Tangulia mbele ya watu, na utayarishe kuondoka, ili waingie na kuriti inchi yenye nimeapia mababu zao kwamba nitawapatia.’+
12 “Sasa, Ee Israeli, Yehova Mungu wako anataka ufanye nini?+ Mambo haya tu: kumuogopa Yehova Mungu wako,+ kutembea katika njia zake zote,+ kumupenda, kumutumikia Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote,+ 13 na kushika amri na sheria za Yehova zenye ninakuamuru leo kwa faida yako mwenyewe.+ 14 Angalia, mbingu, hata mbingu za mbingu* ni za Yehova Mungu wako, na dunia na vitu vyote vyenye kuwa ndani yake.+ 15 Lakini ni mababu zako tu ndio Yehova alikaribia na kuwaonyesha upendo wake, na amewachagua ninyi, uzao wao,+ katikati ya vikundi vyote vya watu, kama vile muko leo. 16 Munapaswa sasa kusafisha* mioyo yenu+ na kuacha kuwa kichwa-nguvu vile.*+ 17 Kwa maana Yehova Mungu wenu ni Mungu wa miungu+ na Bwana wa mabwana, Mungu mukubwa, mwenye nguvu, na mwenye kuogopesha sana, mwenye hamutendee mutu yeyote kwa upendeleo+ na hakubali rushwa.* 18 Anatenda haki kwa ajili ya mutoto mwenye hana baba* na mujane+ na anamupenda mukaaji mugeni,+ anamupatia chakula na nguo. 19 Ninyi pia munapaswa kumupenda mukaaji mugeni, kwa maana mulikuwa wakaaji wageni katika inchi ya Misri.+
20 “Unapaswa kumuogopa Yehova Mungu wako, unapaswa kumutumikia yeye,+ unapaswa kushikamana naye, na unapaswa kuapa kwa jina lake. 21 Ni Yeye unapaswa kusifu.+ Yeye ni Mungu wako, mwenye amekufanyia mambo haya makubwa na yenye kuogopesha sana yenye macho yako mwenyewe yameona.+ 22 Mababu zako walishuka Misri+ na watu* makumi saba (70), na sasa Yehova Mungu wako amefanya mukuwe wengi kama nyota za mbinguni.+
11 “Unapaswa kumupenda Yehova Mungu wako+ na kutimiza sikuzote mambo yenye anakuomba ufanye na sheria zake, maamuzi yake ya hukumu, na amri zake. 2 Munajua kama leo ninazungumuza na ninyi, sizungumuze na wana wenu wenye hawajajua wala kuona nizamu ya Yehova Mungu wenu,+ ukubwa wake,+ mukono wake wenye nguvu+ na mukono wake wenye kunyooshwa. 3 Hawakuona alama zake na matendo yake yenye alimutendea Farao mufalme wa Misri katika Misri na inchi yake yote;+ 4 wala mambo yenye alitendea majeshi ya Misri, farasi za Farao na magari yake ya vita, yenye yalifunikwa na maji ya Bahari Nyekundu wakati walikuwa wanawafuatilia ninyi, na Yehova akawaharibu milele.*+ 5 Hawakuona mambo yenye aliwatendea katika jangwa mupaka wakati mulifika mahali hapa, 6 wala mambo yenye alitendea Datani na Abiramu, wana wa Eliabu mwana wa Rubeni, wakati dunia ilifunguka na kuwameza, pamoja na watu wa nyumba zao na mahema yao na kila kiumbe chenye kuishi chenye kiliwafuata, mbele ya macho ya Israeli wote.+ 7 Macho yenu wenyewe yameona matendo yote makubwa yenye Yehova alifanya.
8 “Munapaswa kushika amri yote yenye ninawapatia leo, kusudi mukuwe na nguvu na kuvuka ili kuingia katika inchi hiyo kusudi muiriti, 9 na ili muishi wakati murefu+ katika inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia mababu zenu na uzao wao,*+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+
10 “Inchi yenye unaenda kuriti haiko kama vile inchi ya Misri, kwenye mulitoka, kwenye ulikuwa unapanda mbegu zako na kuzimwangilia maji kwa muguu wako,* kama vile bustani ya mboga za majani. 11 Lakini inchi yenye munakaribia kuvuka kuingia ndani na kuiriti ni inchi ya milima na mabonde tambarare.+ Inakunywa maji ya mvua kutoka mbinguni;+ 12 ni inchi yenye Yehova Mungu wako anatunza. Macho ya Yehova Mungu wako yako juu ya inchi hiyo sikuzote, kuanzia mwanzo wa mwaka mupaka mwisho wa mwaka.
13 “Na kama mutatii kwa bidii amri zangu zenye ninawaamuru leo na kumupenda Yehova Mungu wenu na kumutumikia kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote,+ 14 nitawapatia pia mvua kwa ajili ya inchi yenu kwa wakati wake wenye uliwekwa, mvua ya kipindi cha mvua ya kwanza na mvua ya kipindi cha mvua ya mwisho, na utakusanya nafaka yako na divai yako mupya na mafuta yako.+ 15 Na nitaotesha majani katika mashamba yako kwa ajili ya mifugo yako, na utakula na kushiba.+ 16 Mukuwe waangalifu ili musiache mioyo yenu ishawishiwe kupotoka na kuabudu miungu mingine na kuiinamia.+ 17 Kama hamufanye vile, kasirani ya Yehova itawaka juu yenu, na atafunga mbingu ili mvua isinyeshe+ na udongo hautazaa mazao yake na mutaangamia haraka katika inchi ya muzuri yenye Yehova anawapatia.+
18 “Munapaswa kukazia maneno yangu haya katika moyo wenu na nafsi* yenu na kuyafunga kama kikumbusho kwenye mukono wenu, na yanapaswa kuwa kama utepe wa kichwa kwenye paji la uso wenu.*+ 19 Muyafundishe watoto wenu, na kuongea kuyahusu wakati unakaa katika nyumba yako na wakati unatembea katika barabara na wakati unalala na wakati unaamuka.+ 20 Uyaandike kwenye miimo ya milango ya nyumba yako na kwenye milango yako mikubwa, 21 ili ninyi na wana wenu muishi wakati murefu+ katika inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia mababu zenu,+ sikuzote zenye mbingu zitakuwa juu ya dunia.
22 “Kama munashika kabisa amri hii yenye ninawapatia na kuitenda, kumupenda Yehova Mungu wenu,+ kutembea katika njia zake zote na kushikamana naye,+ 23 Yehova atafukuza mataifa haya yote mbele yenu,+ na mutakamata inchi ya mataifa makubwa zaidi na yenye watu wengi zaidi kuliko ninyi.+ 24 Kila mahali kwenye mutakanyanga kwa muguu wenu patakuwa penu.+ Mupaka wenu utaanzia katika jangwa kufikia Lebanoni, kuanzia ule Muto, muto Efrati, kufikia kwenye bahari ya mangaribi.*+ 25 Hakuna mutu mwenye atasimama mbele yenu.+ Yehova Mungu wenu ataeneza hofu na woga wenu juu ya inchi yote yenye mutatembea juu yake,+ kama vile aliwaahidi.
26 “Angalia, ninatia mbele yenu leo baraka na laana:+ 27 baraka kama munatii amri za Yehova Mungu wenu zenye ninawaamuru leo,+ 28 na laana kama hamutii amri za Yehova Mungu wenu+ na munageuka kutoka katika njia yenye ninawaamuru mufuate leo na munafuata miungu yenye hamukujua.
29 “Wakati Yehova Mungu wako atakuingiza katika inchi yenye utariti, unapaswa kutangaza* baraka kwenye Mulima Gerizimu na laana kwenye Mulima Ebali.+ 30 Je, milima hiyo haiko ngambo ingine ya Yordani kuelekea mangaribi,* katika inchi ya Wakanaani wenye wanaishi Araba, mbele ya Gilgali, pembeni ya ile miti mikubwa ya More?+ 31 Kwa maana munavuka Yordani ili muingie na kuriti inchi yenye Yehova Mungu wenu anawapatia.+ Wakati mutairiti na kuishi ndani yake, 32 munapaswa kuwa waangalifu ili kushika masharti na maamuzi ya hukumu yenye ninatia mbele yenu leo.+
12 “Haya ndiyo masharti na maamuzi ya hukumu yenye munapaswa kuwa waangalifu kufuata sikuzote zenye mutaishi katika inchi yenye Yehova Mungu wa mababu zenu atawapatia muiriti. 2 Mutaharibu kabisa kila mahali kwenye mataifa yenye mutakamata inchi yao yametumikia miungu yao,+ ikuwe juu ya milima mirefu ao juu ya vilima ao chini ya muti wowote wenye majani mengi. 3 Mutabomoa mazabahu zao, mutavunja-vunja nguzo zao takatifu,+ mutateketeza miti yao mitakatifu* ndani ya moto, na kukata-kata sanamu za kuchongwa za miungu yao,+ na kuondoa kabisa majina ya miungu yao mahali pale.+
4 “Hamupaswe kumuabudu Yehova Mungu wenu kwa njia hiyo.+ 5 Lakini, mumutafute Yehova Mungu wenu kila mahali kwenye atachagua kuweka jina lake na mahali kwenye atakaa kati ya makabila yenu yote, na muende pale.+ 6 Ni pale mutapeleka matoleo yenu ya kuteketezwa,+ zabihu zenu, sehemu zenu za kumi,+ muchango kutoka katika mukono wenu,+ matoleo yenu ya naziri, matoleo yenu ya kujipendea,+ na muzaliwa wa kwanza wa mifugo yenu na kundi lenu.+ 7 Ninyi na watu wa nyumba zenu munapaswa kukulia pale mbele ya Yehova Mungu wenu+ na kushangilia katika kazi zenu zote,+ kwa sababu Yehova Mungu wako amekubariki.
8 “Hamupaswe kufanya kama vile tunafanya hapa leo, kila mutu anafanya jambo lenye anaona kuwa sawa mbele ya macho yake mwenyewe,* 9 kwa sababu bado hamujafika mahali pa kupumuzikia+ na katika uriti wenye Yehova Mungu wako anakupatia. 10 Wakati mutavuka Yordani+ na kuishi katika inchi yenye Yehova Mungu wenu anawapatia ili muiriti, hakika atawapatia pumuziko kutokana na maadui wenu wote wenye kuwazunguka, na mutakaa kwa usalama.+ 11 Mutaleta vitu vyote vyenye ninawaamuru mahali kwenye Yehova Mungu wenu atachagua jina lake likae+—matoleo yenu ya kuteketezwa, zabihu zenu, sehemu zenu za kumi,+ muchango kutoka katika mukono wenu, na kila toleo la naziri lenye munafanya naziri kwa Yehova. 12 Mutashangilia mbele ya Yehova Mungu wenu,+ ninyi na watoto wenu wanaume, watoto wenu wanamuke, watumwa wenu wanaume na wanamuke, na Mulawi mwenye kuwa ndani ya miji yenu,* kwa sababu hakupewa fungu wala uriti pamoja na ninyi.+ 13 Ukuwe muangalifu ili usitoe matoleo yako ya kuteketezwa mahali pengine popote penye utaona.+ 14 Utatoa matoleo yako ya kuteketezwa mahali tu kwenye Yehova atachagua katika moja ya maeneo ya makabila yako, na ni pale utafanya kila jambo lenye ninakuamuru.+
15 “Lakini kila wakati wenye unatamani,* unaweza kuchinja na kula nyama,+ kulingana na baraka yenye Yehova Mungu wako amekupatia katika miji yako yote.* Mutu mwenye haiko safi na mutu mwenye iko* safi anaweza kuikula, kama vile munakula swala ao paa. 16 Lakini hamupaswe kula damu;+ utaimwanga kwenye udongo kama maji.+ 17 Hautaruhusiwa kula ndani ya miji yako* sehemu moja ya kumi (1/10) ya nafaka yako, divai yako mupya, mafuta yako, muzaliwa wa kwanza wa mifugo yako na wa kundi lako,+ matoleo yako yoyote ya naziri yenye unafanyia naziri, matoleo yako ya kujipendea, ao muchango kutoka katika mukono wako. 18 Utakula vitu hivyo mbele ya Yehova Mungu wako mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua+—wewe na mutoto wako mwanaume, mutoto wako mwanamuke, mutumishi wako mwanaume na mwanamuke, na Mulawi mwenye kuwa ndani ya miji yako;* na utashangilia mbele ya Yehova Mungu wako katika kazi zako zote. 19 Ukuwe muangalifu ili usimuzarau Mulawi+ siku zote zenye utaishi katika inchi yako.
20 “Wakati Yehova Mungu wako atapanua eneo lako,+ kama vile amekuahidi,+ na useme, ‘Ninataka kula nyama,’ kwa sababu unatamani* kula nyama, unaweza kula nyama wakati wowote wenye unaitamani.*+ 21 Kama mahali kwenye Yehova Mungu wako anachagua kuweka jina lake+ ni mbali na wewe, basi unapaswa kuchinja wanyama fulani katika mifugo yako ao wanyama fulani katika kundi lako lenye Yehova amekupatia, kama vile nimekuamuru, na unapaswa kula ndani ya miji yako* wakati wowote wenye unaitamani.* 22 Unaweza kuikula kama vile unakula swala na paa;+ mutu mwenye haiko safi na mutu mwenye iko* safi anaweza kuikula. 23 Lakini tu uazimie kabisa kuepuka kula damu,+ kwa sababu damu ndiyo uzima,*+ na haupaswe kula uzima* pamoja na nyama. 24 Haupaswe kuikula. Utaimwanga kwenye udongo kama maji.+ 25 Haupaswe kuikula, ili mambo yakuendee muzuri wewe na watoto wako kisha wewe, kwa sababu unafanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho ya Yehova. 26 Unapaswa kukamata tu vitu vitakatifu vyenye ni vyako na matoleo yako ya naziri wakati unakuja mahali kwenye Yehova atachagua. 27 Utatoa kule matoleo yako ya kuteketezwa, nyama na damu,+ juu ya mazabahu ya Yehova Mungu wako, na damu ya zabihu zako inapaswa kumwangwa kwenye mazabahu+ ya Yehova Mungu wako, lakini unaweza kula nyama.
28 “Ukuwe muangalifu kutii maneno haya yote yenye ninakuamuru, ili mambo yakuendee muzuri sikuzote wewe na wana wako kisha wewe, kwa sababu unafanya mambo mema na yenye kuwa sawa mbele ya macho ya Yehova Mungu wako.
29 “Wakati Yehova Mungu wako ataharibu mataifa yenye utakamata inchi yao,+ na wakati utaishi katika inchi yao, 30 ukuwe muangalifu ili usinaswe katika mutego kisha wao kuharibiwa mbele yako. Usiulize kuhusu miungu yao, na kusema: ‘Namna gani mataifa haya yalizoea kutumikia miungu yao? Mimi pia nitafanya vilevile.’+ 31 Haupaswe kumufanyia vile Yehova Mungu wako, kwa sababu mataifa hayo yanafanyia miungu yao kila jambo lenye kuchukiza lenye Yehova anachukia, hata yanateketeza watoto wao wanaume na watoto wao wanamuke ndani ya moto kwa ajili ya miungu yao.+ 32 Unapaswa kutenda kwa uangalifu kila neno lenye ninakuamuru.+ Haupaswe kuongeza kitu juu yake wala kuondoa kitu juu yake.+
13 “Kama nabii ao mutu mwenye kutabiri kupitia ndoto anatokea katikati yako na kukupatia alama ao jambo la ajabu, 2 na alama ao jambo hilo la ajabu lenye alikuambia linatimia wakati anasema, ‘Tufuate miungu mingine,’ miungu yenye haukujua, ‘na tuitumikie,’ 3 haupaswe kusikiliza maneno ya nabii huyo ao mwota-ndoto huyo,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ ili ajue kama munamupenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+ 4 Munapaswa kumufuata Yehova Mungu wenu, munapaswa kumuogopa yeye, munapaswa kushika amri zake, munapaswa kusikiliza sauti yake; yeye ndiye munapaswa kutumikia, na munapaswa kushikamana naye kabisa.+ 5 Lakini nabii huyo ao mwota-ndoto huyo anapaswa kuuawa,+ kwa sababu alichochea uasi juu ya Yehova Mungu wenu—mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri na kukukomboa katika nyumba ya utumwa—ili kukutosha katika njia yenye Yehova Mungu wako amekuamuru utembee ndani yake. Na unapaswa kuondoa jambo la mubaya katikati yako.+
6 “Kama ndugu yako, mutoto mwanaume wa mama yako, ao mutoto wako mwanaume ao mutoto wako mwanamuke ao bibi yako mwenye unapenda ao rafiki yako wa karibu sana* anajaribu kukushawishi kwa uficho, na kusema, ‘Tuende na tutumikie miungu mingine,’+ miungu yenye wewe wala mababu zako hawakujua, 7 kati ya miungu ya vikundi vya watu vyenye kuwazunguka pande zote, ikuwe karibu na ninyi ao mbali na ninyi, kuanzia mwisho mumoja wa inchi mupaka mwisho mwingine wa inchi, 8 haupaswe kukubali ushawishi wake wala kumusikiliza,+ wala usimusikitikie wala kumusikilia huruma wala kumulinda; 9 lakini, unapaswa kumuua kabisa.+ Mukono wako unapaswa kuwa wa kwanza kuja juu yake ili kumuua, kisha mukono wa watu wote utafuata.+ 10 Na unapaswa kumupiga majiwe mupaka akufe,+ kwa sababu alitafuta kukugeuza umuache Yehova Mungu wako, mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. 11 Halafu Israeli wote watasikia na kuogopa, na hawatafanya tena jambo lolote la mubaya kama hilo kati yako.+
12 “Kama unasikia ikisemwa katika mumoja kati ya miji yako yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili ukae ndani yake, 13 ‘Watu wenye hawana mafaa yoyote wametokea kati yako ili kupotosha wakaaji wa muji wao, na kusema, “Tuende na tutumikie miungu mingine,” miungu yenye haukujua,’ 14 unapaswa kupeleleza jambo hilo, kufanya uchunguzi na kuuliza habari kwa uangalifu;+ na kama inahakikishwa kwamba ni kweli jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa kati yako, 15 unapaswa kabisa kupiga na kuua wakaaji wa muji huo kwa upanga.+ Haribu muji huo na kila kitu chenye kuwa ndani yake, pamoja na mifugo yake kwa upanga.+ 16 Kisha utakusanya vitu vyote vya muji huo katikati ya kiwanja cha watu wote cha muji huo na kuteketeza kwa moto muji huo, na vitu vya muji huo vitakuwa toleo nzima kwa ajili ya Yehova Mungu wako. Na muji huo utakuwa rundo la mabomoko milele. Haupaswe kujengwa tena. 17 Mukono wako haupaswe kukamata kitu chochote chenye kilitiwa pembeni ili kuharibiwa,*+ kusudi Yehova aache kasirani yake yenye kuwaka na akuonyeshe rehema na huruma na kukufanya uongezeke, kama vile ameapia mababu zako.+ 18 Kwa maana unapaswa kumutii* Yehova Mungu wako kwa kushika amri zake zote zenye ninakuamuru leo, na hivyo kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho ya Yehova Mungu wako.+
14 “Ninyi ni wana wa Yehova Mungu wenu. Musijikatekate+ wala kunyoa upara kwenye mapaji ya nyuso zenu* kwa ajili ya mutu mwenye amekufa.+ 2 Kwa maana wewe ni kikundi cha watu watakatifu+ kwa ajili ya Yehova Mungu wako, na Yehova amekuchagua kuwa kikundi chake cha watu, mali yake ya pekee,* katikati ya vikundi vyote vya watu vyenye kuwa juu ya uso wa dunia.+
3 “Haupaswe kula kitu chochote chenye kuchukiza.+ 4 Hawa ndio wanyama wenye munaweza kula:+ ngombe-dume, kondoo, mbuzi, 5 paa, swala, kulungu, mbuzi wa pori, mbawala, kondoo wa pori, na kondoo wa mulima. 6 Munaweza kula munyama yeyote mwenye kwato* yenye kupasuka katikati na kugawanyika mara mbili na mwenye anacheua chakula. 7 Lakini hamupaswe kula wanyama wenye kufuata wenye wanacheua ao wenye kwato zenye kupasuka katikati: ngamia, sungura, na wibari, kwa sababu wanacheua lakini hawana kwato* zenye kupasuka katikati. Hawako safi kwenu.+ 8 Pia nguruwe kwa sababu iko* na kwato* yenye kupasuka katikati lakini hacheue. Yeye haiko safi kwenu. Hamupaswe kula nyama yao wala kugusa mizoga yao.
9 “Katikati ya viumbe vyote vyenye kuishi ndani ya maji, munaweza kula hivi: Kitu chochote chenye mapezi* na magamba, munaweza kula.+ 10 Lakini hamupaswe kula kitu chochote chenye hakina mapezi* na magamba. Hakiko safi kwenu.
11 “Munaweza kula ndege yeyote mwenye kuwa safi. 12 Lakini hamupaswe kula hawa: tai, furukombe, tumbusi mweusi,+ 13 mwewe mwekundu, mwewe mweusi, kila aina ya mbua, 14 kila aina ya kunguru, 15 mbuni, bundi, shakwe, kila aina ya kipanga, 16 bundi mudogo, bundi mwenye masikio ya murefu, bata-maji, 17 mwari, tumbusi, munandi, 18 korongo, kila aina ya kulastara, hudihudi, na popo. 19 Pia, kila kiumbe chenye mabawa chenye kupatikana kwa wingi* hakiko safi kwenu. Havipaswe kukuliwa. 20 Munaweza kula kiumbe chochote safi chenye kuruka.
21 “Hamupaswe kula munyama yeyote mwenye alipatikana amekufa.+ Munaweza kumupatia mukaaji mugeni mwenye kuwa ndani ya miji yenu,* na anaweza kumukula, ao munyama huyo anaweza kuuzishwa kwa mugeni. Kwa maana wewe ni kikundi cha watu watakatifu kwa ajili ya Yehova Mungu wako.
“Haupaswe kutokotesha mwana-mbuzi katika maziwa ya mama yake.+
22 “Unapaswa kabisa kutoa sehemu moja ya kumi (1/10)* ya kila kitu chenye mbegu yako inazaa katika mashamba mwaka kwa mwaka.+ 23 Utakula sehemu moja ya kumi (1/10) ya nafaka yako, divai yako mupya, mafuta yako, na muzaliwa wa kwanza wa mifugo yako na wa kundi lako mbele ya Yehova Mungu wako mahali kwenye atachagua jina lake likae,+ ili ujifunze kumuogopa Yehova Mungu wako sikuzote.+
24 “Lakini kama safari ni murefu sana kwako na hivyo hauweze kuipeleka mahali kwenye Yehova Mungu wako anachagua jina lake likae,+ kwa sababu ni mbali sana na wewe (kwa sababu Yehova Mungu wako atakubariki), 25 basi unaweza kuibadilisha kwa feza, na ukiwa na feza zako katika mukono wako, fanya safari mupaka mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua. 26 Kisha unaweza kutumia feza hizo kuuza kitu chochote chenye unatamani*—ngombe, kondoo, mbuzi, divai na pombe zingine, na kitu chochote chenye unapenda;* na utakulia kule mbele ya Yehova Mungu wako na kushangilia, wewe na watu wa nyumba yako.+ 27 Na usimuzarau Mulawi mwenye kuwa ndani ya miji yako,+ kwa sababu hakupewa fungu wala uriti pamoja na wewe.+
28 “Kwenye mwisho wa kila miaka tatu (3), unapaswa kupeleka inje sehemu moja yote ya kumi (1/10) ya mazao yako ya mwaka huo na kuiweka ndani ya miji yako.+ 29 Kisha Mulawi, mwenye hakupewa fungu wala uriti katikati yako, mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba,* na mujane mwenye kuwa ndani ya miji yako atakuja na kula na kushiba,+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika mambo yote yenye unafanya.+
15 “Kwenye mwisho wa kila miaka saba (7), munapaswa kuachilia.+ 2 Haya ndiyo mambo yenye mutaachilia: Kila mwenye alikopesha ataachilia deni lenye jirani yake alikamata. Hapaswe kuomba malipo kwa jirani ao ndugu yake, kwa maana yatatangazwa kuwa yameachiliwa kwa ajili ya Yehova.+ 3 Unaweza kumuomba mugeni alipe,+ lakini unapaswa kuachilia deni lolote lenye ndugu yako anapaswa kukulipa. 4 Lakini, hakuna mutu kati yako mwenye anapaswa kuwa maskini, kwa sababu hakika Yehova atakubariki+ katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili uikamate kuwa uriti, 5 lakini kama tu utatii kabisa sauti ya Yehova Mungu wako na kushika kwa uangalifu amri yote hii yenye ninakupatia leo.+ 6 Kwa maana Yehova Mungu wako atakubariki kama vile amekuahidi, na utakopesha* mataifa mengi, lakini wewe hautahitaji kukopa;+ na utatawala mataifa mengi, lakini hayatakutawala.+
7 “Kama mumoja wa ndugu zako anakuwa maskini kati yako katika muji mumoja kati ya miji ya inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia, usifanye moyo wako kuwa mugumu ao kumufungia mukono ndugu yako maskini.+ 8 Kwa maana unapaswa kumufungulia mukono wako kwa ukarimu+ na usikose kumukopesha* chochote chenye anahitaji ao chenye anakosa. 9 Ukuwe muangalifu ili wazo hili la mubaya lisikuwe katika moyo wako, ‘Mwaka wa saba (7), mwaka wa kuachilia, umekaribia,’+ na hivyo ukatae kumuonyesha ukarimu ndugu yako maskini na kukosa kumupatia chochote. Kama anamulilia Yehova kwa sababu yako, utakuwa umetenda zambi.+ 10 Unapaswa kumupatia kwa ukarimu,+ na haupaswe* kumupatia kwa kunungunika, kwa maana hiyo ndiyo sababu Yehova Mungu wako atabariki kila tendo na kila kazi yako.+ 11 Kwa maana maskini atakuwa sikuzote katika inchi.+ Ndiyo sababu ninakuamuru, ‘Unapaswa kumufungulia mukono wako kwa ukarimu ndugu yako mwenye kuteseka na maskini katika inchi yako.’+
12 “Kama mumoja wa ndugu zako, mwanaume ao mwanamuke Mwebrania, anauzishwa kwako na amekutumikia miaka sita (6), basi katika mwaka wa saba (7) unapaswa kumuachilia huru.+ 13 Na kama unamuachilia huru, usimuache aende mikono wazi. 14 Unapaswa kumupatia kwa ukarimu kitu fulani kutoka katika kundi lako, kutoka katika kiwanja chako cha kupigia-pigia nafaka, na kutoka katika kikamulio chako cha mafuta na divai. Unapaswa kumupatia kama vile Yehova Mungu wako amekubariki. 15 Kumbuka kwamba ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri na kwamba Yehova Mungu wako alikukomboa. Ndiyo sababu ninakuamuru ufanye vile leo.
16 “Lakini kama anakuambia, ‘Sitakuacha!’ kwa sababu anakupenda wewe na nyumba yako, kwa maana amekuwa mwenye furaha wakati amekuwa pamoja na wewe,+ 17 utakamata musumari na kutoboa sikio lake mupaka musumari huo uingie katika mulango, na atakuwa mutumwa wako maisha yake yote. Utamufanyia vilevile mutumwa wako mwanamuke. 18 Usione kuwa vigumu wakati unamuachilia huru na wakati anakuacha, kwa sababu malipo ya kazi yenye alikutumikia miaka sita (6) yalikuwa mara mbili malipo ya kazi ya mufanyakazi wa kulipwa, na Yehova Mungu wako amekubariki katika kila jambo lenye lilifanywa.
19 “Unapaswa kutakasa kila muzaliwa wa kwanza wa kiume wa mifugo yako na wa kundi lako kwa ajili ya Yehova Mungu wako.+ Haupaswe kutumia muzaliwa wa kwanza wa mifugo yako* ili kufanya kazi yoyote wala usimukate manyoya muzaliwa wa kwanza wa kundi lako. 20 Wewe na nyumba yako munapaswa kumukula mbele ya Yehova Mungu wako mwaka kwa mwaka mahali kwenye Yehova atachagua.+ 21 Lakini kama iko* na kasoro—ulemavu, upofu, ao kasoro ingine kubwa—haupaswe kumutoa zabihu kwa Yehova Mungu wako.+ 22 Utamukula ndani ya miji yako,* mutu mwenye haiko safi na mwenye iko* safi watamukula, kama vile ingekuwa swala ao paa.+ 23 Lakini haupaswe kula damu yake;+ utaimwanga kwenye udongo kama maji.+
16 “Shika mwezi wa Abibu* na ufanye Pasaka kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ kwa sababu katika mwezi wa Abibu, Yehova Mungu wako alikutosha Misri usiku.+ 2 Na utamutolea Yehova Mungu wako zabihu ya toleo la Pasaka,+ kutoka katika kundi na mifugo,+ mahali kwenye Yehova atachagua jina lake likae.+ 3 Haupaswe kula kitu chochote chenye kuwa na chachu pamoja na toleo hilo;+ kwa siku saba (7) unapaswa kula mikate yenye haina chachu, mikate ya mateso, kwa sababu ulitoka haraka katika inchi ya Misri.+ Fanya vile siku zote za maisha yako ili ukumbuke siku yenye ulitoka katika inchi ya Misri.+ 4 Unga wowote wenye ulifinyangwa na wenye kuwa na chachu haupaswe kupatikana katika eneo lako lote kwa siku saba (7),+ wala nyama yoyote yenye utatoa zabihu mangaribi ya siku ya kwanza haipaswe kubakia usiku wote mupaka asubui yenye kufuata.+ 5 Hautaruhusiwa kutoa zabihu ya toleo la Pasaka katika muji wowote tu katikati ya miji yenye Yehova Mungu wako anakupatia. 6 Lakini itafanywa mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua jina lake likae. Utatoa zabihu ya toleo la Pasaka mangaribi kisha tu jua kushuka,+ wakati wenye uliwekwa wa kutoka kwako Misri. 7 Unapaswa kupika na kula toleo hilo+ mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua,+ na asubui unaweza kurudia kwenye mahema yako. 8 Kwa siku sita (6) utakula mikate yenye haina chachu, na siku ya saba (7) kutakuwa mukusanyiko mukubwa kwa ajili ya Yehova Mungu wako. Haupaswe kufanya kazi yoyote.+
9 “Utahesabia majuma saba (7). Unapaswa kuanza kuhesabia majuma saba kuanzia wakati unatia mundu* kwa mara ya kwanza kwenye nafaka yenye kusimama.+ 10 Kisha utafanya Sikukuu ya Majuma kwa ajili ya Yehova Mungu wako+ kupitia toleo la kujipendea kutoka katika mukono wako, lenye utatoa kulingana na namna Yehova Mungu wako anakubariki.+ 11 Na unapaswa kushangilia mbele ya Yehova Mungu wako, wewe na mutoto wako mwanaume, mutoto wako mwanamuke, mutumwa wako mwanaume, mutumwa wako mwanamuke, Mulawi mwenye kuwa ndani ya miji yako,* mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba,* na mujane, wenye kuwa katikati yako, mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua jina lake likae.+ 12 Kumbuka kama ulikuwa mutumwa katika Misri,+ na ushike na kutenda masharti haya.
13 “Unapaswa kufanya Sikukuu ya Vibanda*+ kwa siku saba (7) wakati unakusanya kutoka katika kiwanja chako cha kupigia-pigia nafaka na kutoka katika kikamulio chako cha mafuta na divai. 14 Shangilia wakati wa sikukuu yako,+ wewe na mutoto wako mwanaume, mutoto wako mwanamuke, mutumwa wako mwanaume, mutumwa wako mwanamuke, Mulawi, mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane, wenye kuwa ndani ya miji yako. 15 Kwa siku saba (7) utamufanyia Yehova Mungu wako sikukuu+ mahali kwenye Yehova atachagua, kwa maana Yehova Mungu wako atabariki mazao yako yote na mambo yote yenye utafanya,+ na utakuwa mwenye furaha tu.+
16 “Mara tatu (3) kwa mwaka, wanaume wako wote wataonekana mbele ya Yehova Mungu wako mahali kwenye atachagua: kwenye Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu,+ Sikukuu ya Majuma,+ na Sikukuu ya Vibanda,*+ na mutu yeyote katikati yao asionekane mbele ya Yehova mikono wazi. 17 Zawadi yenye kila mutu ataleta italingana na baraka zenye Yehova Mungu wako amekupatia.+
18 “Unapaswa kuweka waamuzi+ na maofisa kwa ajili ya kila kabila katika miji yote* yenye Yehova Mungu wako anakupatia, na wanapaswa kuhukumu watu kwa hukumu yenye haki. 19 Haupaswe kupotosha hukumu,+ kuonyesha upendeleo,+ wala kukubali rushwa,* kwa maana rushwa* inapofusha macho ya wenye hekima+ na inageuza maneno ya wenye haki. 20 Haki—haki ndiyo unapaswa kufuatilia,+ ili uendelee kuishi na kuriti inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia.
21 “Hautapanda muti wa namna yoyote ili ukuwe muti mutakatifu*+ karibu na mazabahu ya Yehova Mungu wako yenye utajitengenezea.
22 “Wala hautajisimamishia nguzo takatifu,+ kitu chenye Yehova Mungu wako anachukia.
17 “Haupaswe kumutolea Yehova Mungu wako zabihu ya ngombe-dume ao kondoo mwenye kasoro ao mwenye kuwa na tatizo lolote, kwa sababu jambo hilo litakuwa chukizo kwa Yehova Mungu wako.+
2 “Kama mwanaume ao mwanamuke anapatikana kati yako, katika muji mumoja kati ya miji yenye Yehova Mungu wako anakupatia, mwenye kuzoea kufanya mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova Mungu wako na kuvunja agano lake,+ 3 na anajiendesha mubaya na kuabudu miungu mingine na kuinamia miungu hiyo ao jua ao mwezi ao jeshi lote la mbinguni,+ jambo lenye sijaamuru.+ 4 Wakati unaambiwa ao kusikia habari hiyo, basi unapaswa kuchunguza jambo hilo kwa uangalifu. Kama inahakikishwa kuwa ni kweli+ jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa katika Israeli, 5 unapaswa kumupeleka inje ya milango mikubwa ya muji mwanaume ao mwanamuke mwenye amefanya uovu huo, na mwanaume ao mwanamuke huyo anapaswa kuuawa kwa kupigwa majiwe.+ 6 Kwa ushuhuda wa* mashahidi wawili ao watatu (3)+ ule mwenye anapaswa kufa atauawa. Hapaswe kuuawa kwa ushuhuda wa shahidi mumoja.+ 7 Mukono wa mashahidi unapaswa kuwa wa kwanza kuja juu yake ili kumuua, na mukono wa watu wote utafuata. Unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katikati yako.+
8 “Kama kunatokea kesi ya hukumu yenye kuwa ngumu sana kwako kuamua katika muji mumoja kati ya miji yako, ikuwe kesi ya hukumu yenye inahusu kumwanga damu+ ao jambo la kuomba haki limetokezwa ao tendo la jeuri limefanywa ao mambo mengine ya mabishano, utasimama na kuenda mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua.+ 9 Uende kwa makuhani Walawi na kwa muamuzi+ mwenye kutumikia wakati huo, na uulize, na watakupatia uamuzi.+ 10 Kisha unapaswa kutenda kulingana na uamuzi wenye wanakupatia mahali pale kwenye Yehova anachagua. Ukuwe muangalifu ili kufanya kulingana na mambo yote yenye wanakuagiza. 11 Unapaswa kutenda kulingana na sheria yenye watakuonyesha na kulingana na uamuzi wenye watakuambia.+ Usigeuke na kuacha uamuzi wenye watakupatia, kwa kuenda kuume ao kushoto.+ 12 Mutu mwenye anatenda kwa kimbelembele kwa kukosa kumusikiliza kuhani mwenye anamutumikia Yehova Mungu wako ao kwa kukosa kumusikiliza muamuzi anapaswa kufa.+ Unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katika Israeli.+ 13 Basi watu wote watasikia na kuogopa, na hawatatenda tena kwa kimbelembele.+
14 “Wakati utaingia katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia na wakati utakuwa umeikamata na kuishi ndani yake, na useme, ‘Niweke mufalme juu yangu kama vile mataifa yote yenye kunizunguka,’+ 15 katika hali hiyo, unapaswa kabisa kumuweka mufalme mwenye Yehova Mungu wako atachagua.+ Utamuweka mufalme kutoka kati ya ndugu zako. Unakatazwa kuweka juu yako mugeni mwenye haiko ndugu yako. 16 Lakini, hapaswe kujipatia farasi wengi+ ao kufanya watu warudie Misri ili kupata farasi wengi zaidi,+ kwa sababu Yehova aliwaambia, ‘Hamupaswe hata kidogo kurudia tena kupitia njia hii.’ 17 Wala hapaswe kujichukulia bibi wengi, ili moyo wake usipotoke;+ wala hapaswe kujipatia feza na zahabu nyingi sana.+ 18 Wakati atakaa kwenye kiti cha ufalme wake, anapaswa kujiandikia katika kitabu* kopi ya Sheria hii, kutoka katika kopi yenye makuhani Walawi wanaweka.+
19 “Kopi hiyo inapaswa kubakia pamoja naye, na anapaswa kusoma ndani yake siku zote za maisha yake,+ kusudi ajifunze kumuogopa Yehova Mungu wake na kushika maneno yote ya Sheria hii na masharti haya kwa kuyatenda.+ 20 Hivyo moyo wake hautajiinua juu ya ndugu zake, na hataacha amri hiyo, kwa kuenda kuume ao kushoto, ili abakie wakati murefu juu ya ufalme wake, yeye na wana wake katikati ya Israeli.
18 “Makuhani Walawi, na kwa kweli kabila lote la Lawi, hawatapewa fungu wala uriti pamoja na Israeli. Watakula matoleo yenye yanatolewa kwa Yehova kwa njia ya moto, yenye ni uriti wake.+ 2 Kwa hiyo hawatakuwa na uriti katikati ya ndugu zao. Yehova ndiye uriti wao, kama vile amewaambia.
3 “Sasa hii ndiyo itakuwa haki ya makuhani kutoka kwa watu: Kila mutu mwenye anatoa zabihu, kama ni ngombe-dume ao kondoo, anapaswa kumupatia kuhani bega, mataya,* na tumbo. 4 Utamupatia matunda ya kwanza ya nafaka yako, divai yako mupya, mafuta yako, na manyoya ya kwanza ya kondoo yenye yalikatwa kwenye kundi lako.+ 5 Yehova Mungu wako amemuchagua yeye na wana wake katikati ya makabila yako yote ili kufanya utumishi katika jina la Yehova sikuzote.+
6 “Lakini kama Mulawi anatoka katika muji mumoja kati ya miji yako katika Israeli kwenye alikuwa anaishi+ na anatamani* kuenda mahali kwenye Yehova anachagua,*+ 7 anaweza kutumikia kule katika jina la Yehova Mungu wake sawasawa na ndugu zake wote, Walawi, wenye kusimama kule mbele ya Yehova.+ 8 Atapokea fungu lilelile la chakula pamoja nao,+ zaidi ya malipo yenye anapata kisha kuuzisha vitu vya mababu zake.
9 “Wakati utakuwa umeingia katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia, haupaswe kujifunza kuiga mazoea yenye kuchukiza ya mataifa hayo.+ 10 Asipatikane katikati yako mutu yeyote mwenye kupitisha mutoto wake mwanaume ao mutoto wake mwanamuke katika moto,+ mutu yeyote mwenye kufanya uaguzi,+ mutu yeyote mwenye kufanya uchawi,+ mutu yeyote mwenye kutafuta alama za mambo yenye yatatokea,+ mulozi,+ 11 mutu yeyote mwenye anafunga wengine kwa uchawi, mutu yeyote mwenye anatafuta shauri kwa mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu+ ao mutu mwenye kutabiri matukio,+ ao mutu yeyote mwenye kuuliza habari kwa wafu.+ 12 Kwa maana kila mutu mwenye kufanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova, na kwa sababu ya mazoea hayo yenye kuchukiza, Yehova Mungu wako anafukuza mataifa hayo mbele yako. 13 Utajionyesha kuwa bila lawama mbele ya Yehova Mungu wako.+
14 “Kwa maana mataifa haya yenye unakamata inchi yao yalizoea kusikiliza wale wenye kufanya uchawi+ na uaguzi,+ lakini Yehova Mungu wako hakukuruhusu kufanya jambo lolote kama hilo. 15 Yehova Mungu wako atakuinulia nabii kama mimi kati ya ndugu zako. Unapaswa kumusikiliza. + 16 Hilo ndilo jibu kwa mambo yenye ulimuomba Yehova Mungu wako kule Horebu katika siku ya mukusanyiko,*+ wakati ulisema, ‘Usiache nisikie sauti ya Yehova Mungu wangu ao kuona tena moto huu mukubwa, ili nisikufe.’+ 17 Kisha Yehova akaniambia, ‘Jambo lenye wamesema ni sawa. 18 Nitawainulia nabii kama wewe+ katikati ya ndugu zao, na nitatia maneno yangu katika kinywa chake,+ na atawaambia mambo yote yenye nitamuamuru.+ 19 Kwa kweli, nitamuomba hesabu kila mutu mwenye hatasikiliza maneno yangu yenye nabii huyo atasema katika jina langu.+
20 “Kama nabii yeyote anasema kwa kimbelembele katika jina langu neno lenye sikumuamuru aseme ao anasema katika jina la miungu mingine, nabii huyo anapaswa kufa.+ 21 Lakini, unaweza kusema katika moyo wako: “Namna gani tutajua kama Yehova hakusema neno hilo?” 22 Wakati nabii anasema neno katika jina la Yehova na neno hilo halitimie ao halifanyike, basi Yehova hakusema neno hilo. Nabii huyo alilisema kwa kimbelembele. Haupaswe kumuogopa.’
19 “Wakati Yehova Mungu wako ataharibu mataifa yenye Yehova Mungu wako anakupatia inchi yao na wakati utakuwa umekamata inchi yao na kuishi katika miji yao na nyumba zao,+ 2 utatia pembeni miji tatu (3) katikati ya inchi yako yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili uiriti.+ 3 Utagawanya katika sehemu tatu (3) eneo la inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili uiriti, na utatayarisha barabara ili muuaji yeyote aweze kukimbilia katika muji mumoja kati ya miji hiyo.
4 “Sasa itakuwa hivi kuhusu muuaji mwenye anaweza kukimbilia kule ili aishi: Wakati anamupiga mwenzake bila kukusudia na hakukuwa anamuchukia mbele;+ 5 kama vile wakati anaenda na mwenzake katika pori ili kuokota kuni na anainua mukono wake ili akate muti na shoka, lakini shoka linachomoka kwenye mupini na kugonga mwenzake na anakufa, muuaji huyo anapaswa kukimbilia katika muji mumoja kati ya miji hiyo.+ 6 Kama hafanye vile, katika kasirani kali,* mulipiza-kisasi cha damu+ anaweza kumufuatilia, kumukamata, na kumuua, kwa sababu muji huo ulikuwa mbali sana. Lakini, hakustahili kufa, kwa sababu hakukuwa anamuchukia mwenzake mbele.+ 7 Ndiyo sababu ninakuamuru: ‘Utie pembeni miji tatu (3).’
8 “Kama Yehova Mungu wako anapanua eneo lako kama vile aliapia mababu zako+ na kama amekupatia inchi yote yenye aliahidi kupatia mababu zako+ 9 —ikiwa unashika kwa uaminifu amri hii yote yenye ninakupatia leo, kumupenda Yehova Mungu wako na kutembea sikuzote katika njia zake+—basi utaongeza miji ingine tatu (3) kwenye hiyo miji tatu.+ 10 Hivyo hakuna damu yenye haina kosa yenye itamwangwa+ katika inchi yako yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti, na hatia yoyote ya damu haitakuja juu yako.+
11 “Lakini kama mutu alikuwa anamuchukia mwenzake+ na alikuwa anangojea kumushambulia na akamuumiza* mupaka kufa na akakufa, na mutu huyo amekimbilia katika muji mumoja kati ya miji hiyo, 12 basi wazee wa muji wake watamuita kutoka kule na kumutia katika mukono wa mulipiza-kisasi cha damu, na mutu huyo anapaswa kufa.+ 13 Hautamusikilia huruma,* na unapaswa kuondoa hatia ya damu yenye haina kosa katika Israeli,+ ili mambo yakuendee muzuri.
14 “Wakati utapokea uriti wako katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili uiriti, haupaswe kuondoa alama ya mupaka wa jirani yako+ mahali kwenye mababu zako waliweka mipaka.
15 “Shahidi mumoja hawezi kufanya mutu mwingine akuwe na hatia* kwa kosa lolote ao zambi yoyote yenye anaweza kutenda.+ Kwa ushuhuda wa* mashahidi wawili ao kwa ushuhuda wa mashahidi watatu (3) jambo litahakikishwa.+ 16 Kama shahidi mwenye nia mubaya anatoa ushuhuda juu ya mutu na anamushitaki kwa kosa fulani,+ 17 watu hao wawili wenye kuwa na mabishano watasimama mbele ya Yehova, mbele ya makuhani na waamuzi wenye watakuwa wanatumikia wakati huo.+ 18 Waamuzi watachunguza kwa uangalifu,+ na kama mutu huyo mwenye alishuhudia ni shahidi wa uongo na ameleta shitaka la uongo juu ya ndugu yake, 19 mutamutendea kama vile alipanga kumutendea ndugu yake,+ na unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katikati yako.+ 20 Wale wenye kubakia watasikia na kuogopa, na hawatafanyaka tena jambo la mubaya kama hilo kati yako.+ 21 Haupaswe kumusikilia* huruma:+ Uzima utakuwa* kwa uzima,* jicho kwa jicho, jino kwa jino, mukono kwa mukono, muguu kwa muguu.+
20 “Kama unaenda kupigana vita na maadui wako na unaona kwamba farasi zao na magari yao na wanajeshi wao ni wengi kuliko wako, usiwaogope, kwa maana Yehova Mungu wako mwenye alikutosha katika inchi ya Misri iko* pamoja na wewe.+ 2 Wakati munakaribia kuenda katika pigano, kuhani atakaribia na kusema na watu.+ 3 Atawaambia, ‘Sikia, Ee Israeli, munakaribia kupigana na maadui wako. Musikuwe na moyo wa woga. Musiogope wala kuwa na hofu wala kutetemeka kwa sababu yao, 4 kwa maana Yehova Mungu wenu anatembea pamoja na ninyi ili awapiganie juu ya maadui wenu na awaokoe.’+
5 “Maofisa pia wataambia watu, ‘Ni nani amejenga nyumba mupya na hajaizindua? Arudie kwenye nyumba yake. Kama hafanye vile, anaweza kufa katika pigano na mwanaume mwingine ataizindua. 6 Na ni nani amepanda shamba la mizabibu na hajaanza kutumia matunda yake? Aende na arudie kwenye nyumba yake. Kama hafanye vile, anaweza kufa katika pigano na mwanaume mwingine ataanza kutumia matunda yake. 7 Na ni nani amemuchumbia mwanamuke lakini hajamuoa? Aende na arudie kwenye nyumba yake.+ Kama hafanye vile, anaweza kufa katika pigano na mwanaume mwingine atamuoa.’ 8 Maofisa watauliza pia watu, ‘Ni nani mwenye kuogopa na mwenye moyo wa woga?+ Anapaswa kurudia kwenye nyumba yake, ili asifanye ndugu zake wavunjike moyo kama yeye.’*+ 9 Wakati maofisa watakuwa wamemaliza kusema na watu, wataweka wakubwa wa majeshi ili kuongoza watu.
10 “Kama unakaribia muji ili kupigana nao, utautangazia pia masharti ya amani.+ 11 Kama muji huo unakupatia jibu la amani na unajifungua kwako, watu wote wenye kupatikana kule watakuwa wako kwa ajili ya kazi ya kulazimishwa, na watakutumikia.+ 12 Lakini kama muji huo unakataa kufanya amani na wewe na kuliko kufanya vile unapigana vita na wewe, utauzunguka kwa ajili ya vita, 13 na hakika Yehova Mungu wako atautia katika mukono wako, na unapaswa kupiga na kuua kila mwanaume katika muji huo kwa upanga. 14 Lakini, wanamuke, watoto, mifugo, na kila kitu chenye kuwa katika muji huo, vitu vyote vya muji huo, unaweza kuvinyanganya kwa ajili yako mwenyewe,+ na utakula vitu vyenye ulichukua kutoka kwa maadui wako, vyenye Yehova Mungu wako amekupatia.+
15 “Ni vile utatendea miji yote yenye kuwa mbali sana na wewe ambayo haiko miji ya mataifa haya yenye kuwa karibu. 16 Lakini katika miji ya vikundi hivi vya watu, yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti, haupaswe kuacha kitu chochote chenye kupumua kiishi.+ 17 Lakini, unapaswa kuwaharibu kabisa, Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi, na Wayebusi,+ kama vile Yehova Mungu wako amekuamuru; 18 kusudi wasiwafundishe ninyi kufuata mazoea yao yote yenye kuchukiza yenye wamefanyia miungu yao, na hivyo kuwafanya mumutendee zambi Yehova Mungu wenu.+
19 “Kama unazunguka muji kwa ajili ya vita ili kuukamata na umepigana nao kwa siku nyingi, haupaswe kuharibu miti yake kwa kutumia shoka juu yake. Unaweza kula matunda yake, lakini haupaswe kuikata.+ Je, utazunguka muti wa mashamba kwa ajili ya vita kama vile unazunguka mwanadamu kwa ajili ya vita? 20 Unaweza kuharibu tu muti wenye unajua kama hautumiwe kwa ajili ya chakula. Unaweza kuukata na kutengeneza vitu vya kutumia ili kuzunguka muji wenye kupigana na wewe, mupaka wakati muji huo utaanguka.
21 “Kama mutu anapatikana ameuawa katika eneo la mashamba la inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili uiriti na haijulikane ni nani alimuua, 2 wazee na waamuzi wako+ wataenda na kupima umbali kutoka kwenye maiti hiyo mupaka kwenye miji yenye kuizunguka. 3 Kisha wazee wa muji wa karibu sana na maiti hiyo watakamata katika mifugo mwana-ngombe mwenye hajatumiwa hata siku moja kufanya kazi, mwenye hajakokota nira hata siku moja, 4 na wazee wa muji huo watapeleka mwana-ngombe huyo kwenye bonde* lenye kutiririka maji lenye halijalimwa wala kupandwa mbegu, na watamuvunja shingo mwana-ngombe huyo kule katika bonde.+
5 “Na makuhani, Walawi, watakaribia kwa sababu Yehova Mungu wako amewachagua wamutolee utumishi,+ watangaze baraka katika jina la Yehova.+ Watatangaza namna kila mabishano yenye kuhusisha jeuri yanapaswa kumalizwa.+ 6 Kisha wazee wote wa muji wenye kuwa karibu sana na maiti hiyo watanawa mikono yao+ juu ya mwana-ngombe huyo mwenye alivunjwa shingo katika bonde, 7 na watasema, ‘Mikono yetu haikumwanga damu hii, wala macho yetu hayakuona wakati ilimwangwa. 8 Usihesabie jambo hili juu ya watu wako Israeli, wenye ulikomboa,+ Ee Yehova, na usiache hatia ya damu yenye haina kosa ibakie kati ya watu wako Israeli.’+ Basi hatia hiyo ya damu haitahesabiwa juu yao. 9 Katika njia hiyo utaondoa hatia ya damu yenye haina kosa katikati yako kwa kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho ya Yehova.
10 “Kama unaenda kupigana vita na maadui wako na Yehova Mungu wako anawashinda kwa ajili yako na unawakamata mateka,+ 11 na unaona mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri kati ya watu hao wenye walikamatwa mateka na unavutiwa naye na unataka kumukamata akuwe bibi yako, 12 unaweza kumuleta katika nyumba yako. Kisha atanyoa kichwa chake, atatunza kucha zake, 13 na kutosha nguo yake ya utekwa, na atakaa katika nyumba yako. Atamulia baba yake na mama yake kwa mwezi muzima,+ na kisha unaweza kulala naye; utakuwa bwana yake naye atakuwa bibi yako. 14 Lakini kama haupendezwe naye, basi utamuacha aende zake+ mahali popote penye anataka.* Lakini hauwezi kumuuzisha ili upate feza ao kumutendea kwa ukali, kwa sababu umemupatisha haya.
15 “Kama mwanaume iko* na bibi wawili na anamupenda mumoja kupita mwingine* na wote wawili wamemuzalia wana na mwana muzaliwa wa kwanza ni wa mwanamuke mwenye hapendwe,+ 16 siku atapatia wana wake uriti wake, hataruhusiwa kumutendea mwana wa mwanamuke mwenye anapendwa sawa vile ni muzaliwa wake wa kwanza na kupuuza mwana wa mwanamuke mwenye hapendwe, ule muzaliwa wa kwanza. 17 Anapaswa kumutambua mwana wa mwanamuke mwenye hapendwe kuwa muzaliwa wa kwanza kwa kumupatia sehemu mbili za kila kitu chenye iko* nacho, kwa sababu mwana huyo ndiye mwanzo wa nguvu zake za uzazi. Haki ya muzaliwa wa kwanza ni yake.+
18 “Kama mutu iko* na mwana mwenye iko* kichwa-nguvu na muasi na hamutii baba yake ao mama yake,+ na wamejaribu kumurekebisha lakini anakataa kuwasikiliza,+ 19 baba yake na mama yake watamushika na kumupeleka kwa wazee kwenye mulango mukubwa wa muji wake 20 na kuambia wazee wa muji wake, ‘Huyu mwana wetu iko* kichwa-nguvu na ni muasi, anakataa kututii. Ni mulafi+ na mulevi.’+ 21 Basi watu wote wa muji wake wanapaswa kumuua kwa kumupiga majiwe. Ni vile unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katikati yako, na Israeli wote watasikia na kuogopa.+
22 “Kama mutu anatenda zambi yenye kustahili hukumu ya kifo na ameuawa+ na umemutundika kwenye muti,+ 23 maiti yake haipaswe kubakia kwenye muti usiku wote.+ Lakini, utahakikisha kwamba unamuzika siku hiyo, kwa sababu mutu mwenye ametundikwa ni kitu chenye kulaaniwa na Mungu,+ na haupaswe kuchafua inchi yako yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti.+
22 “Kama unamuona ngombe-dume wa ndugu yako ao kondoo wake akipotea njia, usijifanye kama haumuone. + Unapaswa kumurudisha kwa ndugu yako. 2 Lakini kama ndugu yako haishi karibu na wewe ao haumujue, utamupeleka munyama huyo kwenye nyumba yako, na atabakia kwako mupaka wakati ndugu yako atamutafuta. Kisha utamurudishia munyama huyo.+ 3 Ni vile utafanyia punda wake, nguo yake, na kitu chochote chenye ndugu yako amepoteza na wewe umekipata. Haupaswe kujifanya kama haukione.
4 “Kama unamuona punda wa ndugu yako ao ngombe-dume wake akianguka katika barabara, haupaswe kumuacha kwa makusudi. Unapaswa kumusaidia kusimamisha munyama huyo.+
5 “Mwanamuke hapaswe kuvaa nguo ya mwanaume, na mwanaume hapaswe kuvaa nguo ya mwanamuke. Kwa maana kila mutu mwenye kufanya vile ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.
6 “Kama unapata katika njia chicha ya* ndege yenye vitoto ao mayai, ikuwe katika muti ao chini, na mama amekaa juu ya vitoto ao mayai, haupaswe kukamata mama pamoja na kitoto chake.+ 7 Hakikisha umemufukuza mama, lakini unaweza kukamata kitoto kwa ajili yako. Fanya vile ili mambo yakuendee muzuri na uishi wakati murefu.
8 “Kama unajenga nyumba mupya, unapaswa pia kujenga ukuta mufupi kwa ajili ya sehemu ya juu ya nyumba yako,+ ili usilete hatia ya damu juu ya nyumba yako kwa sababu ya mutu kuanguka kutoka kwenye nyumba yako.
9 “Haupaswe kupanda aina mbili za mbegu katika shamba lako la mizabibu.+ Kama unafanya vile, mazao yote ya mbegu yenye ulipanda na pia mazao ya shamba la mizabibu yatanyanganywa kwa ajili ya patakatifu.
10 “Haupaswe kulima kwa kutumia ngombe-dume na punda pamoja.+
11 “Haupaswe kuvaa nguo yenye ilitengenezwa kwa kuchanganya manyoya ya kondoo na kitani.+
12 “Utatengeneza mafundo kwenye pembe ine (4) za nguo yenye unavaa.+
13 “Kama mwanaume anachukua bibi na kulala naye lakini kisha anafikia kumuchukia* 14 na anamushitaki kwamba iko* na mwenendo mubaya na kumuharibishia sifa kwa kusema, ‘Nimechukua mwanamuke huyu, lakini wakati nililala naye, sikupata alama ya kuonyesha kwamba alikuwa bikira,’ 15 baba na mama ya mutoto huyo mwanamuke wataonyesha alama ya ubikira wa mutoto huyo mwanamuke kwa wazee kwenye mulango mukubwa wa muji. 16 Baba ya mutoto huyo mwanamuke atawaambia wazee hao, ‘Nilipatia mwanaume huyu binti yangu ili akuwe bibi yake, lakini anamuchukia* 17 na anamushitaki kwamba iko* na mwenendo mubaya kwa kusema, “Nimevumbua kwamba binti yako hana alama ya ubikira.” Sasa hii ndiyo alama ya ubikira wa binti yangu.’ Kisha watatandika nguo hiyo mbele ya wazee wa muji. 18 Wazee wa muji+ watamuchukua mwanaume huyo na kumutia nizamu.+ 19 Watamulipisha amande* ya shekeli* mia moja (100) za feza na kuzipatia baba ya mutoto huyo mwanamuke, kwa sababu mwanaume huyo alimuharibishia sifa bikira wa Israeli,+ na ataendelea kuwa bibi yake. Mwanaume huyo hataruhusiwa kuvunja ndoa naye sikuzote za maisha yake.
20 “Lakini, kama mashitaka hayo ni ya kweli, na hakuna alama ya kuonyesha kwamba mutoto huyo mwanamuke alikuwa bikira, 21 watapeleka inje mutoto huyo mwanamuke mupaka kwenye muingilio wa nyumba ya baba yake, na wanaume wa muji wake watamuua kwa kumupiga majiwe, kwa sababu ametenda jambo la haya+ katika Israeli kwa kufanya uasherati* katika nyumba ya baba yake.+ Ni vile unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katikati yako.+
22 “Kama mwanaume anapatikana akilala na mwanamuke ambaye ni bibi ya mwanaume mwingine, wote wawili wanapaswa kuuawa pamoja, ule mwanaume mwenye alilala na mwanamuke na ule mwanamuke vilevile.+ Ni vile unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katika Israeli.
23 “Kama bikira amechumbiwa na mwanaume, na mwanaume mwingine anakutana naye katika muji na kulala naye, 24 utawapeleka inje wote wawili mupaka kwenye mulango mukubwa wa muji huo na kuwaua kwa kuwapiga majiwe, mutoto huyo mwanamuke kwa sababu hakulalamika katika muji na mwanaume huyo kwa sababu alimupatisha haya bibi ya mwanaume mwenzake.+ Ni vile unapaswa kuondoa uovu katikati yako.
25 “Lakini, kama mwanaume huyo alikuta mutoto huyo mwanamuke mwenye kuchumbiwa katika eneo la mashamba na mwanaume huyo alimukamata kwa nguvu na kulala naye, mwanaume huyo mwenye alilala naye atakufa peke yake, 26 na haupaswe kumutendea jambo lolote mutoto huyo mwanamuke. Mutoto huyo mwanamuke hakutenda zambi yenye kustahili kifo. Hali hii ni sawa na ya mutu mwenye anashambulia mwenzake na kumuua.*+ 27 Kwa maana mwanaume huyo alimukuta katika eneo la mashamba, na mutoto huyo mwanamuke mwenye kuchumbiwa akalalamika, lakini hapakukuwa mutu wa kumuokoa.
28 “Kama mwanaume anakutana na mutoto mwanamuke mwenye kuwa bikira ambaye hajachumbiwa na anamukamata kwa nguvu na kulala naye na wanavumbuliwa,+ 29 mwanaume mwenye alilala naye anapaswa kupatia baba ya mutoto huyo mwanamuke shekeli makumi tano (50) za feza, na atakuwa bibi yake.+ Kwa sababu mwanaume huyo alimupatisha haya, hataruhusiwa kuvunja ndoa naye siku zote za maisha yake.
30 “Mwanaume yeyote hapaswe kuchukua bibi ya baba yake, ili asimupatishe haya baba yake.*+
23 “Mwanaume yeyote mwenye amefanywa kuwa towashi kwa sababu mapumbu yake yamepondwa ao mwenye amekatwa kiungo chake cha kiume hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.+
2 “Mwana-haramu yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.+ Hata kufikia kizazi cha kumi (10), muzao wake yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.
3 “Mwamoni ao Mumoabu yeyote hapaswe kuingia katika kutaniko la Yehova.+ Hata kufikia kizazi cha kumi (10), muzao wao yeyote hapaswe kuingia hata siku moja katika kutaniko la Yehova, 4 kwa sababu hawakuwasaidia na chakula na maji wakati mulikuwa katika njia kutoka Misri,+ na kwa sababu walimulipa Balaamu mwana wa Beori kutoka Petori kule Mesopotamia ili awalaani* ninyi.+ 5 Lakini Yehova Mungu wako alikataa kumusikiliza Balaamu.+ Kuliko kufanya vile, Yehova Mungu wako alibadilisha laana hiyo kuwa baraka kwa ajili yako,+ kwa sababu Yehova Mungu wako alikupenda.+ 6 Haupaswe hata kidogo kuhangaikia hali njema yao wala mafanikio yao siku zako zote.+
7 “Haupaswe kumuchukia Mwedomu, kwa sababu yeye ni ndugu yako.+
“Haupaswe kumuchukia Mumisri, kwa sababu ulikuwa mukaaji mugeni katika inchi yake.+ 8 Kizazi cha tatu (3) cha watoto wao wenye watazaa kinaweza kuingia katika kutaniko la Yehova.
9 “Wakati unapiga kambi ili kupigana na maadui wako, unapaswa kuepuka kitu chochote kibaya.*+ 10 Kama mwanaume anakuwa muchafu kwa sababu ametokwa na mbegu za uzazi* usiku,+ anapaswa kuenda inje ya kambi na asirudie katika kambi. 11 Wakati inafika mangaribi, anapaswa kunawa maji, na kisha anaweza kurudia katika kambi wakati jua linashuka.+ 12 Mahali pa faraga* panapaswa kuwekwa ili patumiwe inje ya kambi, na ni pale unapaswa kuenda. 13 Kipande kidogo cha muti kinapaswa kuwa katika vitu vyako. Wakati unashutama inje, unapaswa kukitumia ili kuchimba shimo na kisha ufunike mavi yako. 14 Kwa maana Yehova Mungu wako anatembea katika kambi yako+ ili kukukomboa na kutia maadui wako katika mukono wako, na kambi yako inapaswa kuwa takatifu,+ ili asione kitu chochote chenye hakifae katikati yako na ageuke na kuacha kutembea pamoja na wewe.
15 “Haupaswe kumutia mutumwa katika mukono wa bwana wake wakati anamukimbia bwana wake na kuja kwako. 16 Anaweza kukaa kati yako mahali popote penye atachagua katika muji mumoja kati ya miji yako, popote penye anapenda. Haupaswe kumutendea mubaya.+
17 “Binti yeyote kati ya mabinti wa Israeli hapaswe kuwa kahaba wa hekalu,+ wala mwana yeyote kati ya wana wa Israeli hapaswe kuwa kahaba wa hekalu.+ 18 Haupaswe kuleta malipo ya kahaba mwanamuke ao malipo ya* kahaba mwanaume* katika nyumba ya Yehova Mungu wako ili kutimiza naziri, kwa sababu vyote viwili ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.
19 “Haupaswe kumulipisha ndugu yako faida,+ ikuwe faida juu ya feza, juu ya chakula, ao juu ya kitu chochote chenye faida inaweza kuombwa juu yake. 20 Unaweza kumulipisha mugeni faida,+ lakini haupaswe kumulipisha ndugu yako faida,+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika kazi zako zote katika inchi yenye unaenda kuriti.+
21 “Kama unafanya naziri kwa Yehova Mungu wako,+ usikawie kuitimiza.+ Kwa maana Yehova Mungu wako hakika atakudai naziri hiyo; kama sivyo, utakuwa umetenda zambi.+ 22 Lakini kama unajizuia kufanya naziri, hautakuwa na hatia ya zambi.+ 23 Unapaswa kutimiza neno la midomo yako,+ na unapaswa kutimiza naziri yenye ulifanya kwa kinywa chako mwenyewe ili kuwa toleo la kujipendea kwa Yehova Mungu wako.+
24 “Kama unaingia katika shamba la mizabibu la jirani yako, unaweza kula zabibu za kutosha ili kutosheleza hamu yako ya kula,* lakini haupaswe kutia zabibu zozote katika chombo chako.+
25 “Kama unaingia katika shamba la nafaka yenye kusimama ya jirani yako, unaweza kuchuma kwa mukono wako masuke yenye kukomaa, lakini haupaswe kutia mundu* kwenye nafaka ya jirani yako.+
24 “Kama mwanaume anamuoa mwanamuke lakini hapendezwe naye kwa sababu alipata jambo fulani lenye halifae juu yake, anapaswa kuandika cheti cha kuvunja ndoa kwa ajili ya mwanamuke huyo,+ kumupatia cheti hicho, na kumufukuza atoke katika nyumba yake.+ 2 Kisha yeye kuondoka katika nyumba ya mwanaume huyo, anaweza kuenda na kuwa bibi ya mwanaume mwingine.+ 3 Kama mwanaume huyo wa pili anamuchukia* na anamuandikia cheti cha kuvunja ndoa, anamupatia cheti hicho, na anamufukuza katika nyumba yake ao kama mwanaume huyo wa pili mwenye alimuoa anakufa, 4 bwana yake wa kwanza mwenye alimufukuza hataruhusiwa kumuchukua tena ili akuwe bibi yake kisha mwanamuke huyo kuchafuliwa, kwa maana jambo hilo ni chukizo kwa Yehova. Haupaswe kuleta zambi katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti.
5 “Wakati mwanaume ameoa karibuni, hatatumika katika jeshi ao kupewa kazi ingine yoyote. Atakuwa huru kwa mwaka mumoja na atabakia katika nyumba yake na kumufurahisha bibi yake.+
6 “Mutu yeyote hapaswe kukamata jiwe la kusagia la mukono ao jiwe la juu la kusagia kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo,+ kwa sababu kufanya vile ni sawa na kukamata riziki ya* mutu kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo.
7 “Kama mutu anapatikana amemubeba kwa nguvu ndugu yake Mwisraeli na amemutesa na kumuuzisha,+ mutu huyo mwenye kubeba watu kwa nguvu anapaswa kufa.+ Unapaswa kuondoa mambo ya mubaya katikati yako.+
8 “Wakati ukoma* unatokea, ukuwe muangalifu sana ili kufanya kulingana na mambo yote yenye makuhani Walawi watawaagiza.+ Mukuwe waangalifu ili kufanya sawasawa na vile niliamuru makuhani Walawi. 9 Kumbuka namna Yehova Mungu wako alimutendea Miriamu katika njia wakati mulikuwa munatoka Misri.+
10 “Kama unamukopesha jirani yako kitu chochote,+ haupaswe kuingia katika nyumba yake ili kumunyanganya kitu chenye ameahidi kuwekesha kwa ajili ya mukopo. 11 Utasimama inje, na mutu huyo mwenye alipokea mukopo atakuletea inje kitu chenye anawekesha kwa ajili ya mukopo. 12 Na kama mutu huyo iko* katika uhitaji, haupaswe kulala na ungali na kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo.+ 13 Unapaswa kabisa kumurudishia kitu chenye amewekesha kwa ajili ya mukopo wakati tu jua linashuka, na ataenda kulala akiwa na nguo yake,+ na atakubariki; na hilo litamaanisha haki kwa ajili yako mbele ya Yehova Mungu wako.
14 “Haupaswe kupunja mufanyakazi wa kulipwa mwenye kuwa katika uhitaji na mwenye iko* maskini, akuwe mumoja wa ndugu zako ao mukaaji mugeni katika inchi yako, ndani ya miji yako.*+ 15 Utamupatia mushahara wake siku ileile,+ mbele ya jua kushuka, kwa sababu iko* katika uhitaji na uzima wake unategemea* mushahara wake. Kama haufanye vile, atamulilia Yehova kwa sababu yako, na utakuwa na hatia ya zambi.+
16 “Baba hawapaswe kuuawa kwa sababu ya mambo yenye watoto wao wanafanya, na watoto hawapaswe kuuawa kwa sababu ya mambo yenye baba zao wanafanya.+ Kila mutu anapaswa kuuawa kwa sababu tu ya zambi yake mwenyewe.+
17 “Haupaswe kupotosha hukumu ya mukaaji mugeni ao ya mutoto mwenye hana baba,*+ na haupaswe kukamata nguo ya mujane kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo.+ 18 Kumbuka kwamba ulikuwa mutumwa katika Misri, na Yehova Mungu wako akakukomboa kutoka kule.+ Ndiyo sababu ninakuamuru ufanye vile.
19 “Wakati unavuna mavuno yako katika shamba lako na unasahau fungu la mbegu katika shamba, usirudie ili kulikamata. Litaachwa kwa ajili ya mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane,+ ili Yehova Mungu wako akubariki katika mambo yote yenye unafanya.+
20 “Wakati unapiga muzeituni ili kuangusha zeituni, haupaswe kufanya vile tena kwenye matawi yake. Zeituni zenye kubakia zitakuwa za mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane.+
21 “Wakati unakusanya zabibu katika shamba lako la mizabibu, haupaswe kurudia kukusanya masalio. Yataachwa kwa ajili ya mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane. 22 Kumbuka kwamba ulikuwa mutumwa katika inchi ya Misri. Ndiyo sababu ninakuamuru ufanye vile.
25 “Wakati mabishano yanatokea katikati ya watu, wanaweza kuenda mbele ya waamuzi,+ na waamuzi watawaamua na kumutangaza mwenye haki kwamba hana hatia na mutu muovu kwamba iko* na hatia.+ 2 Kama mutu muovu anastahili kupigwa,+ muamuzi atamufanya alale uso chini, na atapigwa mbele yake. Hesabu ya viboko inapaswa kulingana na uovu wa jambo lenye alifanya. 3 Anaweza kumupiga kufikia viboko makumi ine (40),+ lakini hapana zaidi. Kama anaendelea kumupiga viboko zaidi kuliko viboko hivyo, ndugu yako atapata haya mbele ya macho yako.
4 “Haupaswe kufunga kinywa cha ngombe-dume wakati anakanyanga-kanyanga nafaka.+
5 “Kama ndugu wanaishi pamoja na mumoja wao anakufa bila kupata mwana, bibi ya ule mwenye alikufa hataolewa na mutu fulani inje ya familia hiyo. Shemeki yake ataenda kwake, atamuchukua akuwe bibi yake, na kufunga naye ndoa ya mutu na shemeki yake.+ 6 Muzaliwa wa kwanza mwenye bibi huyo atazaa ataendeleza jina la ndugu yake mwenye alikufa,+ ili jina lake lisifutwe katikati ya Israeli.+
7 “Sasa kama mwanaume huyo hataki kuoa mujane wa ndugu yake, basi mujane wa ndugu yake ataenda kwa wazee kwenye mulango mukubwa wa muji na kusema, ‘Ndugu ya bwana yangu amekataa kulinda jina la ndugu yake katika Israeli. Amekataa kufunga na mimi ndoa ya mutu na shemeki yake.’ 8 Wazee wa muji wake wanapaswa kumuita na kuzungumuza naye. Kama anakazana na kusema, ‘Sitaki kumuoa,’ 9 basi mujane wa ndugu yake atamukaribia mbele ya wazee, atatosha kiatu cha mwanaume huyo kwenye muguu wake,+ atamutemea mate katika uso wake, na kusema, ‘Ni vile anapaswa kutendewa mwanaume mwenye hatajenga nyumba ya ndugu yake.’ 10 Kisha mambo hayo jina la familia yake* katika Israeli litakuwa ‘Nyumba ya mutu mwenye alitoshwa kiatu.’
11 “Kama wanaume wawili wanapigana na bibi ya mumoja wao anaingilia kati ili kumulinda bwana yake kutokana na ule mwenye kumupiga na ananyoosha mukono wake na kukamata sehemu za siri za ule mwenye kupiga bwana yake, 12 unapaswa kumukata mukono mwanamuke huyo. Haupaswe* kusikia huruma.
13 “Haupaswe kuwa na namna mbili ya majiwe ya kupimia katika mufuko wako,+ jiwe la mukubwa na jiwe la kidogo. 14 Haupaswe kuwa na namna mbili ya vyombo vya kupimia* katika nyumba yako,+ kikubwa na kidogo. 15 Unapaswa kuwa na jiwe la kupimia lenye kuwa sawa na la haki na kipimo chenye kuwa sawa na cha haki, ili uishi wakati murefu katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia.+ 16 Kwa maana kila mutu mwenye hatende haki mwenye anafanya mambo hayo ni chukizo kwa Yehova Mungu wako.+
17 “Kumbuka mambo yenye Amaleki alikutendea katika njia wakati ulikuwa unatoka Misri,+ 18 namna alikutana na wewe katika njia na kushambulia wale wote wenye walikuwa wanajikokota nyuma yako wakati ulikuwa umechoka na kuishiwa nguvu. Hakumuogopa Mungu. 19 Wakati Yehova Mungu wako atakuwa amekupatia pumuziko kutokana na maadui wako wote wenye kukuzunguka katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti ili uikamate,+ unapaswa kufuta jina la Amaleki chini ya mbingu.+ Haupaswe kusahau.
26 “Wakati mwishowe utaingia katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia kuwa uriti na wakati utakuwa umeiriti na kuishi ndani yake, 2 utakamata sehemu fulani ya matunda ya kwanza ya mazao* yote ya udongo, yenye utakusanya katika inchi yako yenye Yehova Mungu wako anakupatia, na utayatia katika kitunga na kuenda mahali kwenye Yehova Mungu wako atachagua jina lake likae.+ 3 Utaenda kwa kuhani mwenye atakuwa anatumikia wakati huo na kumuambia, ‘Leo ninamujulisha Yehova Mungu wako kwamba nimeingia katika inchi yenye Yehova aliapia mababu zetu kwamba atatupatia sisi.’+
4 “Kisha kuhani atakamata kitunga hicho katika mukono wako na kukiweka mbele ya mazabahu ya Yehova Mungu wako. 5 Kisha utatangaza hivi mbele ya Yehova Mungu wako: ‘Baba yangu alikuwa Mwaramu mwenye alikuwa anatanga-tanga,*+ na akashuka kuenda Misri+ na kukaa kule akiwa mugeni, pamoja na watu kidogo katika nyumba yake.+ Lakini kule akakuwa taifa kubwa, lenye nguvu na lenye watu wengi.+ 6 Na Wamisri wakatutendea mubaya na kutukandamiza na kuweka utumwa mukali juu yetu.+ 7 Kwa hiyo tukaanza kumulilia Yehova, Mungu wa mababu zetu, na Yehova akasikia sauti yetu na kuangalia mateso yetu na taabu yetu na kukandamizwa kwetu.+ 8 Mwishowe Yehova akatutosha Misri kwa mukono wenye nguvu na mukono wenye kunyooshwa+ na kwa matendo yenye kuogopesha sana na kwa alama na miujiza.+ 9 Kisha akatuleta mahali hapa na kutupatia inchi hii, inchi yenye kutiririka maziwa na asali.+ 10 Sasa nimeleta matunda ya kwanza ya mazao ya udongo wenye Yehova amenipatia.’+
“Unapaswa kutia kitunga hicho chini mbele ya Yehova Mungu wako na kuinama mbele ya Yehova Mungu wako. 11 Kisha utashangilia kwa sababu ya mambo yote ya muzuri yenye Yehova Mungu wako amekupatia wewe na nyumba yako, wewe na Mulawi na mukaaji mugeni mwenye kuwa kati yako.+
12 “Wakati utamaliza kutoa+ sehemu moja yote ya kumi (1/10) ya mazao yako katika mwaka wa tatu (3), mwaka wa sehemu moja ya kumi, utapatia sehemu hiyo Mulawi, mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba,* na mujane, nao watakula na kushiba katika miji yako.*+ 13 Kisha utasema mbele ya Yehova Mungu wako, ‘Nimeondoa sehemu takatifu katika nyumba yangu na kuipatia Mulawi, mukaaji mugeni, mutoto mwenye hana baba, na mujane,+ kama vile umeniamuru. Sijavunja wala kuzarau amri zako. 14 Sikuikula wakati nilikuwa ninaomboleza wala kuondoa sehemu yake yoyote wakati nilikuwa muchafu ao kutoa sehemu yake yoyote kwa ajili ya wafu. Nimetii sauti ya Yehova Mungu wangu na kufanya mambo yote yenye uliniamuru. 15 Sasa angalia chini ukiwa katika makao yako matakatifu, mbinguni, na ubariki watu wako Israeli na inchi yenye umetupatia,+ kama vile uliapia mababu zetu,+ inchi yenye kutiririka maziwa na asali.’+
16 “Leo Yehova Mungu wako anakuamuru utende masharti haya na maamuzi haya ya hukumu. Unapaswa kuyashika na kuyatenda kwa moyo wako wote+ na nafsi* yako yote. 17 Leo Yehova amekutangazia kwamba atakuwa Mungu wako wakati unatembea katika njia zake na kushika masharti yake,+ amri zake,+ na maamuzi yake ya hukumu,+ na wakati unasikiliza sauti yake. 18 Na leo umemutangazia Yehova kwamba utakuwa kikundi chake cha watu, mali yake ya pekee,*+ kama vile amekuahidi, na kwamba utashika amri zake zote 19 na kwamba atakuweka juu ya mataifa mengine yote yenye amefanya,+ na hivyo kukupatia sifa na kujulikana sana na utukufu wakati unajionyesha kuwa kikundi cha watu watakatifu kwa ajili ya Yehova Mungu wako,+ kama vile amekuahidi.”
27 Kisha Musa pamoja na wazee wa Israeli wakaamuru watu, na kusema: “Mushike kila amri yenye ninawapatia leo. 2 Na siku mutavuka Yordani kuingia katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia, utasimamisha majiwe makubwa na kuyapiga lipu.*+ 3 Kisha uandike juu yake maneno yote ya Sheria hii wakati utakuwa umevuka, ili uingie katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia, inchi yenye kutiririka maziwa na asali, kama vile Yehova, Mungu wa mababu zako, amekuahidi.+ 4 Wakati mutakuwa mumevuka Yordani, mutasimamisha majiwe hayo kwenye Mulima Ebali+ na utayapiga lipu,* kama vile ninawaamuru leo. 5 Pia utamujengea Yehova Mungu wako mazabahu kule, mazabahu ya majiwe. Usitumie vyombo vya chuma juu ya majiwe hayo.+ 6 Utajenga mazabahu ya Yehova Mungu wako kwa majiwe mazima na kumutolea Yehova Mungu wako matoleo ya kuteketezwa juu yake. 7 Utatoa zabihu za ushirika+ na kuzikula mahali pale,+ na utashangilia mbele ya Yehova Mungu wako.+ 8 Na utaandika waziwazi maneno yote ya Sheria hii juu ya majiwe hayo.”+
9 Kisha Musa na makuhani Walawi wakasema na Israeli wote, na kuwaambia: “Nyamaza na usikilize, Ee Israeli. Leo hii umekuwa kikundi cha watu wa Yehova Mungu wako.+ 10 Unapaswa kusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako na kushika amri zake+ na masharti yake, yenye ninakuamuru leo.”
11 Siku hiyo Musa akaamuru watu, na kusema: 12 “Makabila haya yatasimama kwenye Mulima Gerizimu+ ili kubariki watu wakati mutakuwa mumevuka Yordani: Simeoni, Lawi, Yuda, Isakari, Yosefu, na Benyamini. 13 Na makabila haya yatasimama kwenye Mulima Ebali+ ili kutangaza laana: Rubeni, Gadi, Asheri, Zabuloni, Dani, na Naftali. 14 Na Walawi watamujibu kila mutu wa Israeli kwa sauti kubwa:+
15 “‘Alaaniwe mutu mwenye anatengeneza sanamu ya kuchongwa+ ao sanamu ya metali,*+ kitu chenye kuwa chukizo kwa Yehova,+ chenye kilitengenezwa na mikono ya fundi,* na mwenye amekificha.’ (Na watu wote watajibu, na kusema, ‘Amina!’*)
16 “‘Alaaniwe mutu mwenye anamutendea baba yake ao mama yake kwa zarau.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
17 “‘Alaaniwe mutu mwenye anahamisha alama ya mupaka wa jirani yake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
18 “‘Alaaniwe mutu mwenye anamufanya kipofu apotee njia.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
19 “‘Alaaniwe mutu mwenye anapotosha hukumu+ ya mukaaji mugeni, ya mutoto mwenye hana baba,* ao ya mujane.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
20 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na bibi ya baba yake, kwa sababu amemuletea baba yake haya.’*+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
21 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na munyama yeyote.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
22 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na dada yake, binti ya baba yake ao binti ya mama yake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
23 “‘Alaaniwe mutu mwenye analala na mama-mukwe wake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
24 “‘Alaaniwe mutu mwenye anavizia na kuua jirani yake.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
25 “‘Alaaniwe mutu mwenye anakubali rushwa* ili amuue* mutu mwenye hana kosa.’*+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
26 “‘Alaaniwe mutu mwenye hataunga mukono maneno haya ya Sheria hii kwa kuyatenda.’+ (Na watu wote watasema, ‘Amina!’)
28 “Na kama kwa kweli unasikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kuwa muangalifu ili kutenda amri zake zote zenye ninakuamuru leo, hakika Yehova Mungu wako atakuweka juu ya mataifa mengine yote ya dunia.+ 2 Baraka hizi zote zitakuja juu yako na kukufikia,+ kwa sababu unaendelea kusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako:
3 “Utabarikiwa katika muji na utabarikiwa katika eneo la mashamba.+
4 “Watoto wako watabarikiwa*+ na pia mazao ya udongo wako na uzao wa mifugo yako, kitoto chako cha ngombe na kitoto chako cha kondoo.+
5 “Kitunga chako+ na bakuli lako la kufinyangia unga+ vitabarikiwa.
6 “Utabarikiwa wakati utaingia ndani, na utabarikiwa wakati utaenda inje.
7 “Yehova atafanya maadui wako wenye kukushambulia washindwe mbele yako.+ Watakushambulia kutoka upande mumoja, lakini watakukimbia kuelekea pande saba (7) tofauti.+ 8 Yehova ataagiza baraka kwa ajili yako juu ya madepo yako+ na kila kazi yako, na hakika atakubariki katika inchi yenye Yehova Mungu wako anakupatia. 9 Yehova atakufanya kuwa kikundi chake cha watu watakatifu,+ kama vile alikuapia,+ kwa sababu unaendelea kushika amri za Yehova Mungu wako na kutembea katika njia zake. 10 Vikundi vyote vya watu vya dunia vitalazimika kuona kwamba jina la Yehova limeitwa juu yako,+ na vitakuogopa.+
11 “Yehova atakufanya ukuwe na watoto wengi sana na mifugo mingi sana na udongo wenye kuzaa sana+ katika inchi yenye Yehova aliapia mababu zako kwamba atakupatia.+ 12 Yehova atakufungulia depo yake ya muzuri, mbingu, ili kupatia inchi yako mvua kwa wakati wake+ na ili kubariki mambo yote yenye unafanya. Utakopesha mataifa mengi, lakini wewe mwenyewe hautahitaji kukopa.+ 13 Yehova atakufanya kuwa kichwa, hapana mukia; na utakuwa juu,+ hapana chini, kama unaendelea kutii amri za Yehova Mungu wako zenye ninakuamuru leo ili ushike na kutenda. 14 Haupaswe kugeuka na kuacha maneno yote yenye ninakuamuru leo, kwa kuenda kuume ao kushoto,+ kwa kufuata miungu mingine ili kuitumikia.+
15 “Lakini kama hautasikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kuwa muangalifu ili kutenda amri zake zote na sheria zake zenye ninakuamuru leo, laana hizi zote zitakuja juu yako na kukufikia:+
16 “Utalaaniwa katika muji, na utalaaniwa katika eneo la mashamba.+
17 “Kitunga chako+ na bakuli lako la kufinyangia unga+ vitalaaniwa.
18 “Watoto wako*+ na mazao ya udongo wako na kitoto chako cha ngombe na kitoto chako cha kondoo+ kitalaaniwa.
19 “Utalaaniwa wakati utaingia ndani, na utalaaniwa wakati utaenda inje.
20 “Yehova atatuma laana juu yako, muvurugo na azabu katika kila kazi yako mupaka wakati utakuwa umeharibiwa na kumalizika haraka, kwa sababu ya mazoea yako mabaya na kuniacha mimi.+ 21 Yehova atafanya ugonjwa ukuandame mupaka wakati utakuwa umeharibiwa katika inchi yenye unaenda kuriti.+ 22 Yehova atakupiga kwa kifua kikubwa, homa kali,+ kuvimba, homa yenye kuchoma, upanga,+ ugonjwa wenye kukausha mimea, na kuvu;+ na vitakuandama mupaka wakati utakuwa umemalizika. 23 Anga zenye kuwa juu ya kichwa chako zitakuwa shaba, na dunia yenye kuwa chini yako, itakuwa chuma.+ 24 Yehova atafanya mvua ya inchi yako kuwa ungaunga na mavumbi yenye yatakunyeshea kutoka mbinguni mupaka wakati utakuwa umeharibiwa kabisa. 25 Yehova atafanya ushindwe mbele ya maadui wako.+ Utawashambulia kutoka upande mumoja, lakini utawakimbia kuelekea pande saba (7) tofauti; na utakuwa kitu cha kuogopesha sana kwa falme zote za dunia.+ 26 Na mizoga yako itakuwa chakula kwa ajili ya kila ndege wa anga na munyama wa inchi, bila mutu wa kuwaogopesha.+
27 “Yehova atakupiga kwa majipu ya Misri, emoroide,* ukurutu wa ngozi,* na vipele vya ngozi, hautaweza kupona magonjwa hayo. 28 Yehova atakupiga kwa ugonjwa wa wazimu na upofu+ na kukufanya uvurugike.* 29 Utapapasa-papasa katikati ya muchana, kama vile kipofu anapapasa-papasa katika giza,+ na hautapata matokeo ya muzuri katika jambo lolote lenye unafanya; na kila mara watu watakupunja na kukuiba vitu, na hakuna mwenye atakuokoa.+ 30 Utachumbia mwanamuke, lakini mwanaume mwingine atamulala kinguvu. Utajenga nyumba, lakini hautaishi ndani yake.+ Utapanda shamba la mizabibu, lakini hautaanza kutumia matunda yake.+ 31 Ngombe-dume wako atachinjwa mbele ya macho yako, lakini hautakula nyama yake. Punda wako ataibiwa mbele ya macho yako, lakini hatarudishwa kwako. Maadui wako watapewa kondoo wako, lakini hakuna mwenye atakuokoa. 32 Watu wengine watapewa watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke+ wakati utakuwa unaangalia, na sikuzote utatamani kuwaona, lakini mikono yako haitakuwa na nguvu za kufanya kitu chochote. 33 Mavuno ya udongo wako na mazao yako yote yatakuliwa na watu wenye haujue,+ na sikuzote watu watakupunja na kukuponda-ponda. 34 Utapata ugonjwa wa wazimu kwa sababu ya mambo yenye macho yako yataona.
35 “Yehova atakupiga kwa majipu yenye maumivu makali na yenye hayawezi kupona kwenye magoti na miguu yako, kuanzia kikanyangio cha muguu wako mupaka kwenye sehemu ya juu ya katikati ya kichwa chako. 36 Yehova atakupeleka wewe na mufalme mwenye uliweka juu yako kwenye taifa lenye wewe na mababu zako hamukujua,+ na kule utatumikia miungu mingine, miungu ya miti na ya majiwe.+ 37 Na utakuwa kitu cha kuogopesha sana na cha kuzarauliwa,* na kitu cha kuchekelewa kati ya vikundi vyote vya watu kwenye Yehova atakupeleka.+
38 “Utapeleka mbegu nyingi katika shamba, lakini utavuna kidogo,+ kwa sababu nzige watazimeza. 39 Utapanda na kupalilia mashamba ya mizabibu, lakini hautakunywa divai yoyote wala kukusanya zabibu zozote,+ kwa sababu kidudu kitazikula. 40 Utakuwa na miti ya zeituni katika eneo lako lote, lakini hautajipakaa mafuta yoyote, kwa sababu zeituni zako zitaanguka. 41 Utazaa watoto wanaume na watoto wanamuke, lakini hawataendelea kuwa wako, kwa sababu wataenda katika utekwa.+ 42 Makundi ya vidudu yatavamia* miti yako yote na mazao ya udongo wako. 43 Mukaaji mugeni mwenye kuwa katikati yako ataendelea kupanda juu yako zaidi na zaidi, wakati wewe utaendelea kushuka chini zaidi na zaidi. 44 Atakukopesha, lakini wewe hautamukopesha.+ Atakuwa kichwa, lakini wewe mwenyewe utakuwa mukia.+
45 “Laana hizi zote+ hakika zitakuja juu yako na kukufuatilia na kukufikia mupaka wakati utakuwa umeharibiwa,+ kwa sababu haukusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako kwa kushika amri zake na sheria zake zenye alikuamuru.+ 46 Na zitaendelea kubakia juu yako na uzao wako kama alama na jambo la ajabu la kudumu,+ 47 kwa sababu haukumutumikia Yehova Mungu wako kwa furaha na shangwe ya moyo wakati ulikuwa na kila kitu kwa wingi.+ 48 Yehova atatuma maadui wako wakushambulie, na utawatumikia+ wakati uko na njaa+ na kiu na wakati unakosewa nguo na wakati unakosewa kila kitu. Atatia nira ya chuma kwenye shingo yako mupaka wakati atakuwa amekuharibu.
49 “Yehova atainua juu yako taifa la mbali,+ kutoka mwisho wa dunia; litakurukia kama tai,+ taifa lenye hautaelewa luga yake,+ 50 taifa lenye uso mukali lenye haliheshimie muzee wala kumuonyesha kijana wema.+ 51 Watakula uzao wa mifugo yako na mazao ya udongo wako mupaka wakati utakuwa umeharibiwa. Hawatakuachia nafaka yoyote, divai mupya wala mafuta, kitoto cha ngombe wala kitoto cha kondoo mupaka wakati watakuwa wamekuharibu.+ 52 Watakuzunguka kwa ajili ya vita, na hivyo kukufungia ndani ya miji yako yote* katika inchi yako yote mupaka wakati kuta zako za murefu na zenye ngome zenye unategemea zitaanguka. Ndiyo, hakika watakuzunguka kwa ajili ya vita katika miji yako yote, katika inchi yako yote yenye Yehova Mungu wako amekupatia.+ 53 Halafu utalazimika kula watoto wako* mwenyewe, nyama ya watoto wako wanaume na watoto wako wanamuke+ wenye Yehova Mungu wako amekupatia, kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako atakuletea.
54 “Hata mwanaume mupole* sana na mwenye hisia nyingi kati yako hatamusikilia huruma ndugu yake ao bibi yake mupendwa ao wana wake wenye wanabakia, 55 na hatawapatia hata kidogo sehemu yoyote ya nyama ya wana wake yenye atakula, kwa maana hana kitu kingine chochote cha kula kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako ataleta katika miji yako.+ 56 Na mwanamuke mupole* sana na mwenye hisia nyingi kati yako mwenye hawezi hata kufikiria kutia kikanyangio cha muguu wake chini kwa sababu ni mupole sana+ hatakuwa na huruma kuelekea bwana yake mupendwa wala mutoto wake mwanaume wala mutoto wake mwanamuke, 57 hata kuelekea vitu vyenye kutoka katikati ya miguu yake kisha kuzaa na kuelekea wana wenye anazaa, kwa maana atawakula kwa uficho kwa sababu ya kuzungukwa sana kwa ajili ya vita na kwa sababu ya taabu yenye adui yako ataleta katika miji yako.
58 “Kama hautashika kwa uangalifu maneno yote ya Sheria hii yenye kuandikwa katika kitabu hiki+ na kama hauogope jina hili lenye utukufu na lenye kuogopesha sana,+ la Yehova+ Mungu wako, 59 Yehova atakupiga wewe na uzao wako kwa mapigo makali sana, mapigo makubwa na yenye kuendelea,+ na magonjwa hatari na yenye kuendelea. 60 Atakuletea tena magonjwa yote ya Misri yenye ulikuwa unaogopa, na hakika yatashikamana na wewe. 61 Tena, Yehova atakuletea pia kila ugonjwa ao pigo lenye haliandikwe katika kitabu hiki cha Sheria mupaka wakati utakuwa umeharibiwa. 62 Hata kama mumekuwa wengi sana kama vile nyota za mbinguni,+ ni watu kidogo katikati yenu ndio watabakia,+ kwa sababu haukusikiliza sauti ya Yehova Mungu wako.
63 “Na kama vile Yehova alifurahia wakati fulani kuwafanya mufanikiwe na kuongezeka, ni vile Yehova atafurahia kuwaharibu na kuwaangamiza; na mutaongolewa kutoka katika inchi yenye unakaribia kuriti.
64 “Yehova atakusambaza kati ya mataifa yote, kutoka mwisho mumoja wa dunia mupaka mwisho mwingine wa dunia,+ na kule utalazimika kutumikia miungu ya miti na ya majiwe, yenye wewe na mababu zako hamukujua.+ 65 Hautakuwa na amani katika mataifa hayo+ wala mahali pa kupumuzishia kikanyangio cha muguu wako. Lakini, ukiwa kule Yehova atakupatia moyo wenye wasiwasi+ na macho yenye kuwa zaifu na hisia ya kupoteza tumaini.*+ 66 Uzima wako utakuwa katika hatari kubwa, na utasikia woga usiku na muchana; na hautakuwa hakika kama utaokoka. 67 Asubui utasema, ‘Ingekuwa muzuri kama ilikuwa mangaribi!’ na mangaribi utasema, ‘Ingekuwa muzuri kama ilikuwa asubui!’ kwa sababu ya woga wenye utasikia katika moyo wako na kwa sababu ya mambo yenye macho yako yataona. 68 Na hakika Yehova atakurudisha Misri kwa mashua,* kupitia ile njia yenye nilikuambia: ‘Hautaiona tena hata kidogo,’ na kule mutalazimika kujiuzisha kwa maadui wenu ili kuwa watumwa wanaume na watumwa wanamuke, lakini hakutakuwa mutu wa kuwauza.”
29 Haya ndiyo maneno ya agano lenye Yehova alimuamuru Musa afanye pamoja na watu wa Israeli katika inchi ya Moabu, zaidi ya lile agano lenye alifanya pamoja nao kule Horebu.+
2 Kisha Musa akaita Israeli wote na kuwaambia, “Mumeona mambo yote yenye Yehova alifanya mbele ya macho yenu katika inchi ya Misri juu ya Farao na juu ya watumishi wake wote na inchi yake yote,+ 3 hukumu kubwa zenye* macho yako yaliona, zile alama kubwa na miujiza.+ 4 Lakini Yehova hajawapatia moyo wa kuelewa na macho ya kuona na masikio ya kusikia, mupaka leo.+ 5 ‘Wakati nilikuwa ninawaongoza kwa miaka makumi ine (40) katika jangwa,+ nguo zenu hazikuzeeka juu yenu na viatu vyenu havikuzeeka kwenye miguu yenu.+ 6 Hamukukula mukate, na hamukukunywa divai wala pombe yoyote, ili mujue kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu.’ 7 Mwishowe mulifika mahali hapa, na Sihoni mufalme wa Heshboni+ na Ogu mufalme wa Bashani+ wakakuja kupigana na sisi, lakini tuliwashinda.+ 8 Kisha pale tulikamata inchi yao na kuipatia Warubeni, Wagadi, na nusu ya kabila la Manase kuwa uriti wao.+ 9 Kwa hiyo, mushike maneno ya agano hili na kuyatii, ili kila jambo lenye munafanya likuwe na matokeo mazuri.+
10 “Leo ninyi wote munasimama mbele ya Yehova Mungu wenu; vichwa vya makabila yenu, wazee wenu, maofisa wenu, kila mwanaume wa Israeli, 11 watoto wenu, bibi zenu,+ na mukaaji mugeni+ mwenye anaishi katikati ya kambi yako, kuanzia mutu mwenye anakuokotea kuni mupaka mutu mwenye anakushotea maji. 12 Uko hapa ili uingie katika agano la Yehova Mungu wako na kiapo chake, agano lenye Yehova Mungu wako anafanya pamoja na wewe leo+ 13 ili akufanye leo kuwa kikundi chake cha watu+ na akuwe Mungu wako,+ kama vile amekuahidi na kama vile aliapia mababu zako, Abrahamu,+ Isaka,+ na Yakobo.+
14 “Sasa sifanye agano hili na kiapo hiki pamoja na ninyi tu, 15 lakini ni pamoja na wale wenye kusimama hapa pamoja na sisi leo mbele ya Yehova Mungu wetu na pamoja na wale wenye hawako hapa pamoja na sisi leo. 16 (Kwa maana munajua muzuri namna tuliishi katika inchi ya Misri na namna tulipita katikati ya mataifa mbalimbali wakati tulikuwa katika safari.+ 17 Na mulikuwa munaona vitu vyao vyenye kuchukiza na sanamu zao zenye kuchukiza*+ za miti na majiwe, feza na zahabu, zenye walikuwa nazo.) 18 Mukuwe waangalifu ili kusikuwe mwanaume ao mwanamuke, familia ao kabila kati yenu leo lenye moyo wake utageuka na kumuacha Yehova Mungu wetu ili kuenda kutumikia miungu ya mataifa hayo,+ ili kusikuwe kati yenu muzizi wenye kuzaa tunda lenye sumu na pakanga.+
19 “Lakini kama mutu anasikia maneno ya kiapo hiki na anajivuna katika moyo wake, na kusema, ‘Nitakuwa na amani, hata kama ninaendelea kutembea katika njia za moyo wangu mwenyewe,’ na hivyo kuharibu kila kitu* katika njia yake, 20 Yehova hatakuwa tayari kumusamehe.+ Lakini, kasirani kali ya Yehova itawaka juu ya mutu huyo, na laana yote yenye kuandikwa katika kitabu hiki hakika itakuja juu yake,+ na Yehova kwa kweli atafuta jina la mutu huyo chini ya mbingu. 21 Kisha Yehova atamuondoa katika makabila yote ya Israeli ili apate musiba kulingana na laana yote ya agano yenye kuandikwa katika kitabu hiki cha Sheria.
22 “Wakati kizazi cha siku zenye kuja cha wana wenu na mugeni kutoka inchi ya mbali wataona mapigo ya inchi, magonjwa yenye Yehova ameleta juu ya inchi— 23 kiberiti na chumvi na kuteketea, na hivyo inchi yote haitapandwa wala kuotesha mimea, wala hakuna mumea wowote wenye utaota ndani yake, kama vile ilikuwa wakati wa kupinduliwa kwa Sodoma na Gomora,+ Adma na Seboimu,+ miji yenye Yehova alipindua katika kasirani yake na katika kasirani yake kali— 24 wao na mataifa yote watasema, ‘Sababu gani Yehova alitendea hivi inchi hii?+ Ni nini kilitokeza kasirani hii kali, yenye kuwaka?’ 25 Kisha watasema, ‘Ni kwa sababu waliacha agano la Yehova,+ Mungu wa mababu zao, lenye alifanya nao wakati aliwatosha katika inchi ya Misri.+ 26 Lakini walienda na kutumikia miungu mingine na kuiinamia, miungu yenye hawakukuwa wamejua na yenye hakukuwa amewaruhusu waabudu.*+ 27 Basi kasirani yenye kuwaka ya Yehova ikakuja juu ya inchi hiyo kwa kuleta juu ya inchi hiyo laana yote yenye kuandikwa katika kitabu hiki.+ 28 Kwa hiyo, Yehova akawaongoa kutoka kwenye udongo wao katika kasirani yake+ na kasirani kali na kuuzika sana na akawapeleka katika inchi ingine, mahali kwenye wako leo.’+
29 “Mambo yenye kufichwa ni ya Yehova Mungu wetu,+ lakini mambo yenye kufunuliwa ni yetu na wazao wetu milele, ili tushike maneno yote ya Sheria hii.+
30 “Wakati maneno haya yote yatakuja juu yako, baraka na laana yenye nimeweka mbele yako,+ na uyakumbuke*+ katika mataifa yote kwenye Yehova Mungu wako amekusambaza,+ 2 na urudie kwa Yehova Mungu wako+ na kusikiliza sauti yake kulingana na mambo yote yenye ninakuamuru leo, wewe na wana wako, kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote,+ 3 basi Yehova Mungu wako atarudisha watu wako wenye walikamatwa mateka+ na kukuonyesha rehema+ na kukukusanya tena kutoka katika vikundi vyote vya watu kwenye Yehova Mungu wako amekusambaza.+ 4 Hata kama watu wako wanasambazwa mupaka mwisho wa mbingu, Yehova Mungu wako atakukusanya na kukurudisha kutoka kule.+ 5 Yehova Mungu wako atakurudisha katika inchi yenye baba zako waliriti, na utairiti; na atakufanya ufanikiwe na kukufanya uongezeke kuliko baba zako.+ 6 Yehova Mungu wako atasafisha* moyo wako na moyo wa uzao wako,+ na hivyo utamupenda Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote na ili uishi.+ 7 Kisha Yehova Mungu wako ataleta laana hizi zote juu ya maadui wako, wenye walikuchukia na kukutesa.+
8 “Halafu utarudia na kusikiliza sauti ya Yehova na kushika amri zake zote zenye ninakuamuru leo. 9 Yehova Mungu wako atakufanya upate matokeo ya muzuri sana katika kazi yote ya mikono yako,+ atafanya ukuwe na watoto wengi na mifugo mingi na mazao mengi ya udongo wako, kwa maana Yehova atafurahia tena kukufanya upate matokeo ya muzuri, kama vile alifurahia mababu zako.+ 10 Kwa maana wakati huo utasikiliza sauti ya Yehova Mungu wako na kushika amri zake na sheria zenye kuandikwa katika kitabu hiki cha Sheria, na utarudia kwa Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi* yako yote.+
11 “Sasa amri hii yenye ninakuamuru leo haiko nguvu sana kwako, wala haiko kwenye hauwezi kufika.*+ 12 Haiko mbinguni, ili useme, ‘Ni nani mwenye atapanda mupaka mbinguni na atuletee amri hiyo, ili tuisikie na kuishika?’+ 13 Wala haiko ngambo ingine ya bahari, ili useme, ‘Ni nani atavuka ngambo ingine ya bahari ili atuletee amri hiyo, ili tuisikie na kuishika?’ 14 Kwa maana lile neno liko karibu sana na wewe, katika kinywa chako mwenyewe na katika moyo wako mwenyewe,+ ili ulitende.+
15 “Angalia, ninaweka mbele yako leo uzima na mema, na kifo na mabaya.+ 16 Kama utasikiliza amri za Yehova Mungu wako zenye ninakuamuru leo, kwa kumupenda Yehova Mungu wako,+ kutembea katika njia zake, na kushika amri zake na kanuni zake na maamuzi yake ya hukumu, basi utaishi+ na kuongezeka, na Yehova Mungu wako atakubariki katika inchi yenye unaenda kuriti.+
17 “Lakini kama moyo wako unageuka+ na hausikilize na unashawishiwa na unainamia miungu mingine na kuitumikia,+ 18 ninawaambia leo kwamba hakika mutaangamia.+ Hamutaishi wakati murefu katika inchi yenye unavuka Yordani ili kuiriti. 19 Ninachukua mbingu na dunia kuwa mashahidi juu yako leo kwamba nimeweka uzima na kifo mbele yako, baraka na laana;+ na unapaswa kuchagua uzima ili uendelee kuishi,+ wewe na wazao wako,+ 20 kwa kumupenda Yehova Mungu wako,+ kwa kusikiliza sauti yake, na kushikamana naye,+ kwa maana yeye ni uzima wako na kwa uwezo wake utafanya wakati murefu katika inchi yenye Yehova aliapa kwamba atapatia mababu zako Abrahamu, Isaka, na Yakobo.”+
31 Kisha Musa akatoka na kuambia Israeli wote maneno haya, 2 akawaambia: Leo niko na miaka mia moja makumi mbili (120).+ Siwezi tena kuwaongoza,* kwa sababu Yehova ameniambia, ‘Hautavuka muto huu wa Yordani.’+ 3 Yehova Mungu wako ndiye anavuka mbele yako, naye mwenyewe ataharibu mataifa haya mbele yako, na utayafukuza.+ Yoshua ndiye atakuongoza kuvuka,+ kama vile Yehova amesema. 4 Yehova atayatendea kama vile alitendea Sihoni+ na Ogu,+ wafalme wa Waamori, na inchi yao wakati aliwaharibu.+ 5 Yehova atawashinda kwa ajili yako, na mutawatendea kulingana na amri yote yenye nimewapatia.+ 6 Mukuwe hodari na wenye nguvu.+ Musiogope wala musikuwe na hofu mbele yao,+ kwa sababu Yehova Mungu wako ndiye anatembea pamoja na wewe. Hatakutupa wala kukuacha.”+
7 Kisha Musa akamuita Yoshua na kumuambia mbele ya macho ya Israeli wote: “Ukuwe hodari na mwenye nguvu,+ kwa sababu ni wewe utaingiza watu hawa katika inchi yenye Yehova aliapia mababu zao kwamba atawapatia, na utawapatia inchi hiyo kuwa uriti wao.+ 8 Yehova ndiye anatembea mbele yako, na ataendelea kuwa pamoja na wewe.+ Hatakutupa wala kukuacha. Usiogope wala kuwa na hofu.”+
9 Kisha Musa akaandika Sheria hii+ na kuipatia makuhani, Walawi, wenye wanabeba sanduku la agano la Yehova, na wazee wote wa Israeli. 10 Musa akawaamuru, na kusema: “Kwenye mwisho wa kila miaka saba (7), wakati wenye uliwekwa katika mwaka wa kuachilia,+ wakati wa Sikukuu ya Vibanda,*+ 11 Wakati Israeli wote wanakuja mbele ya Yehova+ Mungu wao mahali kwenye anachagua, unapaswa kusoma Sheria hii kwa ajili ya Israeli wote ili waisikie.+ 12 Kusanya watu pamoja,+ wanaume, wanamuke, watoto,* na mukaaji wako mugeni mwenye kuwa katika miji yako,* ili wasikilize na kujifunza juu ya Yehova Mungu wenu na kumuogopa na kuwa waangalifu kutimiza maneno yote ya Sheria hii. 13 Halafu wana wao wenye hawakujua Sheria hii watasikiliza+ na kujifunza kumuogopa Yehova Mungu wenu siku zote zenye mutaishi katika inchi yenye munavuka Yordani ili kuiriti.”+
14 Kisha Yehova akamuambia Musa, “Angalia! Wakati wako wa kufa umekaribia.+ Ita Yoshua, na muende* kwenye hema ya mukutano, ili nimuweke katika madaraka yake.”+ Kwa hiyo Musa na Yoshua wakaenda na kusimama kwenye hema ya mukutano. 15 Kisha Yehova akatokea pale kwenye hema katika nguzo ya wingu, na nguzo hiyo ya wingu ikasimama karibu na muingilio wa hema.+
16 Sasa Yehova akamuambia Musa: “Angalia! Unakaribia kufa,* na watu hawa wataanza kufanya ukahaba wa kiroho na miungu ya kigeni yenye kuwazunguka katika inchi kwenye wanaenda.+ Wataniacha+ na kuvunja agano langu lenye nimefanya pamoja nao.+ 17 Wakati huo kasirani yangu itawaka juu yao,+ na nitawaacha+ na kuficha uso wangu ili wasiuone+ mupaka wakati watateketezwa. Halafu kisha kupatwa na misiba na taabu nyingi,+ watasema, ‘Je, haiko kwa sababu Mungu haiko katikati yetu ndiyo maana misiba hii imekuja juu yetu?’+ 18 Lakini nitaendelea kuficha uso wangu siku hiyo kwa sababu ya uovu wote wenye wametenda kwa kugeuka kuelekea miungu mingine.+
19 “Sasa mujiandikie wimbo huu+ na uufundishe Waisraeli.+ Ufanye wajifunze wimbo huu* ili ukuwe ushahidi wangu juu ya watu wa Israeli.+ 20 Wakati nitawaleta katika inchi yenye niliapia mababu zao+—inchi yenye kutiririka maziwa na asali+—na wakule na kushiba na kufanikiwa,*+ watageukia miungu mingine na kuitumikia na kunikosea heshima na kuvunja agano langu.+ 21 Wakati misiba na taabu nyingi zitakuja juu yao,+ wimbo huu utakuwa ushahidi kwao (kwa sababu wazao wao hawapaswe kuusahau), kwa sababu tayari ninajua muelekeo wenye+ wamekomalisha hata mbele sijawaingiza katika inchi yenye nimewaapia.”
22 Kwa hiyo Musa akaandika wimbo huu siku hiyo na kuufundisha Waisraeli.
23 Kisha akamuweka* Yoshua+ mwana wa Nuni katika madaraka yake na kusema: “Ukuwe hodari na mwenye nguvu,+ kwa sababu ni wewe utaingiza Waisraeli katika inchi yenye nimewaapia,+ na nitaendelea kuwa pamoja na wewe.”
24 Wakati tu Musa alimaliza kuandika maneno yote ya Sheria hii katika kitabu,+ 25 Musa akaamuru Walawi wenye wanabeba sanduku la agano la Yehova, na kusema: 26 “Mukamate kitabu hiki cha Sheria+ na mukiweke pembeni ya sanduku la agano+ la Yehova Mungu wenu, na kitakuwa ushahidi juu yako mahali pale. 27 Kwa maana mimi mwenyewe ninajua muzuri uasi wenu+ na ugumu wa moyo wenu.*+ Kama mumekuwa munamuasi sana Yehova wakati ningali muzima pamoja na ninyi, basi itakuwa namna gani kisha kifo changu! 28 Munikusanyie wazee wote wa makabila yenu na maofisa wenu, na niwaambie maneno haya katika masikio yao, na nikamate mbingu na dunia kuwa mashahidi juu yao.+ 29 Kwa maana ninajua muzuri kwamba kisha kifo changu hakika mutatenda uovu+ na kuacha njia yenye nimewaamuru ninyi. Na hakika musiba utawafikia+ kwenye mwisho wa siku hizo, kwa sababu mutatenda mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova na mutamukasirisha kupitia kazi za mikono yenu.”
30 Kisha katika masikio ya kutaniko lote la Israeli, Musa akarudilia-rudilia maneno ya wimbo huu kuanzia mwanzo mupaka mwisho:+
32 “Mutege sikio, Enyi mbingu, na mimi nitasema,
Na dunia isikie maneno ya kinywa changu.
2 Mafundisho yangu yataanguka kama mvua;
Maneno yangu yataanguka matone-matone kama umande,
Kama mvua ya kidogo-kidogo juu ya majani
Na kama matone mengi ya mvua juu ya mimea.
3 Kwa maana nitatangaza jina la Yehova.+
Museme kuhusu ukubwa wa Mungu wetu!+
5 Wao ndio wametenda kwa upotovu.+
Hawako watoto wake, kasoro ni yao wenyewe.+
Wao ni kizazi chenye kuharibika na chenye kupotoka!+
Je, yeye haiko Baba yenu mwenye aliwaumba,+
Je, haiko Yeye ndiye aliwafanya na kuwaimarisha kabisa?
7 Kumbuka siku za zamani;
Mufikirie miaka ya vizazi vyenye vimepita.
Uliza baba yako, na atakuambia;+
Wazee wako, na watakujulisha.
8 Wakati Mwenye Kuwa Juu Zaidi alipatia mataifa uriti wao,+
Wakati alitenganisha wana wa Adamu,*+
Aliweka mupaka wa vikundi vya watu+
Kulingana na hesabu ya wana wa Israeli.+
11 Kama vile tai anatikisa chicha yake,*
Anapanda juu ya vitoto vyake,
Akinyoosha mabawa yake, na kuvikamata,
Akivibeba juu ya mabawa yake,+
12 Yehova peke yake aliendelea kumuongoza;*+
Hakuna mungu yeyote wa kigeni mwenye alikuwa pamoja naye.+
Alimukulisha asali kutoka katika mwamba
Na mafuta kutoka katika jiwe ngumu,
14 Siagi ya mifugo na maziwa ya kundi,
Pamoja na kondoo wazuri sana,*
Na kondoo-dume wa Bashani, na mbuzi-dume,
Pamoja na ngano ya muzuri sana;*+
Na ulikunywa divai kutoka katika damu* ya zabibu.
15 Wakati Yeshuruni* alinenepa, alipiga-piga muguu kwa uasi.
Umenenepa, umekuwa na mafuta mengi katika mwili, tumbo lako limenenepa.+
Kwa hiyo akamuacha Mungu, mwenye alimufanya,+
Na akamuzarau Mwamba wa wokovu wake.
16 Waliamusha kasirani yake kali kupitia miungu ya kigeni;+
Walikuwa wanamukasirisha na mambo yenye kuchukiza.+
17 Walikuwa wanatoa zabihu kwa pepo wachafu, hapana kwa Mungu,+
Kwa miungu yenye hawakujua,
Mipya yenye ilikuja sasa hivi,
Kwa miungu yenye mababu zenu hawakujua.
19 Wakati Yehova aliona jambo hilo, aliwakataa+
Kwa sababu watoto wake wanaume na watoto wake wanamuke walimukasirisha.
20 Kwa hiyo akasema, ‘Nitaficha uso wangu wasiuone;+
Nitaona chenye kitawapata.
21 Wameamusha kasirani yangu kali* kwa kitu chenye hakiko mungu;+
Wamenikasirisha kwa sanamu zao zenye hazina mafaa yoyote.+
Kwa hiyo nitawachochea wakuwe na wivu kupitia wale wenye hawako kikundi cha watu;+
Nitawakasirisha kwa kutumia taifa pumbavu.+
22 Kwa maana kasirani yangu imewaka moto+
Wenye utateketeza mupaka kwenye sehemu za chini kabisa za Kaburi,*+
Na utateketeza dunia na mazao yake
Na kuchoma misingi ya milima.
23 Nitaongeza misiba yao;
Nitawapiga kwa mishale yangu mupaka iishe.
Nitawatumia meno ya wanyama ili yawashambulie+
Na sumu ya wanyama wenye kutambaa katika mavumbi.
25 Inje, upanga utawaacha mikono wazi;+
Ndani, kuko woga mukubwa+
Kwa kijana mwanaume na bikira,
Mutoto mwenye kunyonya pamoja na muzee mwenye imvi.+
26 Ningesema: “Nitawasambaza;
Nitafanya kumbukumbu lao lisahauliwe kati ya wanadamu,”
27 Haingekuwa kwa sababu ya kuogopa namna adui yangu atatenda,+
Kwa sababu wapinzani wanaweza kulielewa mubaya,+
Wanaweza kusema: “Nguvu zetu zimeshinda;+
Haiko Yehova ndiye alifanya mambo haya yote.”
29 Kama tu wangekuwa na hekima!+ Wangefikiri sana juu ya jambo hili.+
Wangewaza kuhusu mwisho wao.+
30 Namna gani mutu mumoja angeweza kufuatilia elfu moja (1 000),
Na wawili kukimbiza elfu kumi (10 000)?+
Haingewezekana kama Mwamba wao hangekuwa amewauzisha+
Na kama Yehova hangewatia katika mukono wa maadui.
32 Kwa maana muzabibu wao unatoka katika muzabibu wa Sodoma
Na kutoka katika matuta ya Gomora.+
Zabibu zao ni zabibu za sumu,
Vishada vyao ni vichungu.+
33 Divai yao ni sumu ya nyoka,
Sumu kali ya nyoka-kobra.
34 Je, hili haliwekwe karibu na mimi,
Halifungwe kwa muhuri katika depo yangu?+
35 Kisasi ni changu, na malipo,+
Kwa wakati wenye kuwekwa wakati muguu wao utatereza,+
Kwa maana siku ya musiba wao iko karibu,
Na chenye kinawangojea kitafika haraka.’
36 Kwa maana Yehova atahukumu watu wake,+
Na atasikilia huruma* watumishi wake+
Wakati ataona kwamba nguvu zao zimeisha,
Na kwamba wenye hawana uwezo na wenye kuwa wazaifu tu ndio wamebakia.
37 Halafu atasema, ‘Miungu yao iko wapi,+
Mwamba wenye walikimbilia,
38 Yenye ilikuwa inakula mafuta ya zabihu zao,*
Kunywa divai ya matoleo yao ya kinywaji?+
Isimame na kuwasaidia ninyi.
Ikuwe mahali penu pa kukimbilia.
Mimi ninaua, na mimi ninafanya kuwa muzima.+
40 Kwa maana ninainua mukono wangu mbinguni,
Na ninaapa: “Kama vile hakika ninaishi milele,”+
41 Kama ninanoa upanga wangu wenye kumetameta
Na kutayarisha mukono wangu kwa ajili ya hukumu,+
Nitalipiza kisasi juu ya maadui wangu+
Na kuwalipa wale wenye kunichukia.
42 Nitalewesha mishale yangu kwa damu,
Na upanga wangu utakula nyama,
Pamoja na damu ya wenye waliuawa na pia watu wenye walikamatwa mateka,
Pamoja na vichwa vya viongozi wa adui.’
43 Mufurahi, ninyi mataifa, pamoja na watu wake,+
Kwa maana atalipizia kisasi damu ya watumishi wake,+
Na atalipiza kisasi maadui wake+
Na atafunika zambi kwa ajili ya* inchi ya watu wake.”
44 Basi Musa akakuja na kurudilia-rudilia maneno yote ya wimbo huo katika masikio ya watu,+ yeye na Hoshea*+ mwana wa Nuni. 45 Kisha Musa kumaliza kuambia Israeli wote maneno hayo yote, 46 akawaambia: “Muweke katika moyo wenu maonyo yote yenye ninawapatia leo,+ ili muamuru wana wenu wakuwe waangalifu kufanya maneno yote ya Sheria hii.+ 47 Kwa maana hili haliko neno lenye halina maana kwenu, lakini linamaanisha uzima wenu,+ na kupitia neno hili munaweza kuishi wakati murefu katika inchi yenye munavuka Yordani ili kuiriti.”
48 Yehova akasema na Musa siku ileile, na kumuambia: 49 “Panda juu ya mulima huu wa Abarimu,+ Mulima Nebo,+ wenye kuwa katika inchi ya Moabu, wenye unaangaliana na Yeriko, na uangalie inchi ya Kanaani, yenye ninapatia Waisraeli kuwa mali yao.+ 50 Kisha utakufa juu ya mulima wenye utapanda sasa hivi, na utakusanywa kwa watu wako,* kama vile Haruni ndugu yako alikufa juu ya Mulima Hori+ na akakusanywa kwa watu wake, 51 kwa sababu ninyi wote wawili hamukukuwa waaminifu kwangu kati ya Waisraeli kwenye maji ya Meriba+ ya Kadeshi katika jangwa la Zini, kwa sababu hamukunitakasa mbele ya watu wa Israeli.+ 52 Utaona inchi hiyo kwa mbali, lakini hautaingia katika inchi hiyo yenye ninapatia watu wa Israeli.”+
33 Sasa hii ndiyo baraka yenye Musa mutu wa Mungu wa kweli alitangazia Waisraeli mbele ya kifo chake.+ 2 Alisema:
“Yehova—alikuja kutoka Sinai,+
Na akawaangazia kutoka Seiri.
Aliangaza kwa utukufu kutoka katika eneo lenye milima la Parani,+
Na alikuwa pamoja na makumi ya maelfu ya watakatifu,+
Na wapiganaji-vita wake kwenye mukono wake wa kuume.+
5 Na akakuwa mufalme kule Yeshuruni,*+
Wakati vichwa vya watu walikusanyika pamoja,+
Pamoja na makabila yote ya Israeli.+
7 Na akamutangazia Yuda baraka hii:+
“Ee Yehova, sikia sauti ya Yuda,+
Na umurudishe kwa watu wake.
8 Kuhusu Lawi akasema:+
“Tumimu yako* na Urimu yako+ ni vya mutu mwenye kuwa mushikamanifu kwako,+
Mwenye ulijaribu kule Masa.+
Ulianza kushindana naye karibu na maji ya Meriba,+
9 Mutu mwenye aliambia baba yake na mama yake, ‘Sijawaheshimia.’
Hata ndugu zake hakuwatambua,+
Na alipuuza wana wake mwenyewe.
Kwa maana walitii neno lako,
Na walishika agano lako.+
11 Ee Yehova, bariki nguvu zake,
Na ufurahie kazi ya mikono yake.
Vunja miguu ya* wale wenye wanainuka ili kumupinga,
Ili wale wenye kumuchukia wasiinuke tena.”
12 Kuhusu Benyamini alisema:+
“Muache mupendwa wa Yehova akae kwa usalama pembeni yake;
Wakati anamulinda siku nzima,
Atakaa katikati ya mabega yake.”
13 Kuhusu Yosefu alisema:+
“Inchi yake ibarikiwe na Yehova+
Kwa vitu vya muzuri vya mbinguni,
Kwa umande na maji kutoka katika chemchemi zenye kuwa chini,+
14 Kwa vitu vya muzuri vyenye kuletwa na jua
Na mazao ya muzuri kila mwezi,+
15 Kwa vitu vya muzuri sana kutoka katika milima ya zamani*+
Na vitu vya muzuri kutoka katika vilima vyenye kudumu,
16 Kwa vitu vya muzuri vya dunia na vitu vyenye kuijaza,+
Na kwa kukubaliwa na Ule mwenye kukaa katika muti mudogo wa miiba.+
Na vikuje juu ya kichwa cha Yosefu,
Kwenye sehemu ya juu ya katikati ya kichwa cha ule mwenye alichaguliwa kutoka kati ya ndugu zake.+
17 Utukufu wake ni kama wa muzaliwa wa kwanza wa ngombe-dume,
Na pembe zake ni pembe za ngombe-dume wa pori.
Atayatumia ili kusukuma* vikundi vya watu
Mataifa yote mupaka kwenye miisho ya dunia.
Wao ni makumi ya maelfu ya Efraimu,+
Nao ni maelfu ya Manase.”
18 Kuhusu Zabuloni alisema:+
“Shangilia, Ee Zabuloni, wakati unatoka inje,
Na wewe, Isakari, katika mahema yako.+
19 Wataita vikundi vya watu viende kwenye mulima.
Kule watatoa zabihu za haki.
20 Kuhusu Gadi alisema:+
“Amebarikiwa ule mwenye anapanua mipaka ya Gadi.+
Analala kule kama simba,
Akiwa tayari kupasua mukono, ndiyo, sehemu ya juu ya katikati ya kichwa.
Vichwa vya watu watakusanyika pamoja.
Haki ya Yehova ataitimiza,
Na maamuzi yake ya hukumu pamoja na Israeli.”
22 Kuhusu Dani alisema:+
“Dani ni mwana-simba.+
Ataruka kutoka Bashani.”+
23 Kuhusu Naftali alisema:+
“Naftali ametosheka kwa sababu ya kukubaliwa
Na amejaa baraka ya Yehova.
Kamata mangaribi na kusini.”
24 Kuhusu Asheri alisema:+
“Asheri amebarikiwa kuwa na wana.
Apendwe na ndugu zake,
Na atumbukize* miguu yake katika mafuta.
26 Hakuna mwenye kuwa kama Mungu wa kweli+ wa Yeshuruni,+
Mwenye anapita katika mbingu ili kukusaidia
Na kupita juu ya mawingu katika utukufu wake.+
28 Israeli atakaa kwa usalama,
Na chemchemi ya Yakobo itatengwa peke yake
Katika inchi ya nafaka na divai mupya,+
Mwenye anga zake zitaangusha matone-matone ya umande.+
29 Wewe ni mwenye furaha, Ee Israeli!+
Ni nani mwenye kuwa kama wewe,+
Kikundi cha watu wenye kufurahia wokovu wa Yehova,+
Ngao yako yenye kukulinda+
Na upanga wako wenye utukufu?
34 Kisha Musa akatoka katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu na kupanda mupaka kwenye Mulima Nebo,+ kwenye kichwa cha Pisga,+ yenye kuangaliana na Yeriko.+ Na Yehova akamuonyesha inchi yote, kuanzia Gileadi mupaka Dani,+ 2 na Naftali yote na inchi ya Efraimu na Manase, na inchi yote ya Yuda mupaka bahari ya mangaribi,*+ 3 na Negebu+ na ile Wilaya,+ bonde tambarare la Yeriko, muji wa miti ya mitende, mupaka Soari.+
4 Kisha Yehova akamuambia: “Hii ndiyo inchi yenye niliapia Abrahamu, Isaka, na Yakobo, na kusema, ‘Nitapatia uzao wako* inchi hii.’+ Nimekuruhusu uione kwa macho yako mwenyewe, lakini hautavuka kuingia kule.”+
5 Kisha Musa mutumishi wa Yehova akakufa kule katika inchi ya Moabu kama vile Yehova alikuwa amesema.+ 6 Akamuzika katika bonde katika inchi ya Moabu, ngambo ingine ya Bet-peori, na hakuna mwenye anajua kaburi lake liko wapi mupaka leo.+ 7 Musa alikuwa na miaka mia moja makumi mbili (120) wakati alikufa.+ Macho yake hayakukuwa yamefifia, na nguvu zake hazikukuwa zimeisha. 8 Watu wa Israeli wakamulia Musa katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu kwa siku makumi tatu (30).+ Kisha siku za kumulia na kumuombolezea Musa zikaisha.
9 Yoshua mwana wa Nuni alikuwa amejaa roho ya hekima, kwa sababu Musa alikuwa ameweka mukono wake juu yake;+ na Waisraeli wakaanza kumusikiliza, na wakafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru Musa.+ 10 Lakini hakujatokea tena nabii mwingine katika Israeli mwenye kuwa kama Musa,+ mwenye Yehova alijua uso kwa uso.+ 11 Alifanya alama zote na miujiza yenye Yehova alikuwa amemutuma afanye katika inchi ya Misri juu ya Farao na juu ya watumishi wake wote na juu ya inchi yake yote,+ 12 pamoja na mukono wenye nguvu na nguvu zenye kuogopesha zenye Musa alionyesha mbele ya macho ya Israeli wote.+
Tnn., “wana wa Israeli.”
Inaonekana ni mustari wa milima ya Lebanoni.
Tnn., “mbegu yao.”
Ao “Bonde la Muto.”
Tnn., “walifanya mioyo yetu iyeyuke.”
Ni kusema, yenye kuta za murefu sana.
Tnn., “kwa ukamilifu; kabisa.”
Ao pengine, “Mungu amemutia nguvu.”
Ao “Musiwachokoze.”
Ao “Bonde la Muto.”
Ao “Bonde la Muto.”
Ao “Bonde la Muto.”
Ni kusema, Krete.
Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”
Ao “watakuwa na maumivu kama ya kuzaa.”
Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”
Ao “Bonde la Muto.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”
Ao pengine, “jiwe la rangi nyeusi la volkano.”
Mukono mumoja ulikuwa sawa na santimetre 44.5 (inchi 17.5). Angalia Nyongeza B14.
Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”
Maana yake “Vijiji vya Mahema vya Yairi.”
Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”
Ni kusema, Bahari Yenye Kufa.
Ao “eko.”
Ao “na kuangalia sana nafsi yako.”
Tnn., “mupaka kwenye moyo wa mbingu.”
Tnn., “yale Maneno Kumi.”
Ao “muangalie sana nafsi zenu.”
Ao “wa uriti wake.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “majaribu.”
Tnn., “mbegu yao.”
Ao “Bonde la Muto la Arnoni.”
Ni kusema, Bahari ya Chumvi, ao Bahari Yenye Kufa.
Ao “kwa kunizarau mimi.” Tnn., “zidi ya uso wangu.”
Ao “mufano wa.”
Ao “fazili zenye upendo.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “na mambo yakuendee muzuri.”
Tnn., “maneno.”
Ao “katikati ya wanadamu wote.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nguvu yako yote ya uzima; mali yako yote.”
Ao “uyarudilie-rudilie kwa; uyaingize katika.”
Tnn., “katikati ya macho yako.”
Tnn., “mbele ya.”
Ao “kuoana.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mali yake yenye anapendezwa nayo sana.”
Tnn., “mukono.”
Tnn., “atabariki uzao wa tumbo lako la uzazi.”
Tnn., “Utameza.”
Tnn., “Jicho lako halipaswe.”
Ao “majaribu makubwa yenye.”
Ao pengine, “wasiwasi; woga mukubwa.”
Ao “eko.”
Ao “mabonde ya mito yenye maji.”
Ao “chemchemi za maji zenye kuenda chini sana.”
Ni kusema, yenye kuta za murefu sana.
Ao “ukamate inchi yao.”
Tnn., “wenye shingo ngumu.”
Ao “kutaniko.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Tnn., “wenye shingo ngumu.”
Ao “cha kuyeyushwa.”
Ao “niliomba dua.”
Ao “kuomba dua kwa.”
Ao “uriti wako.”
Ao “uriti wako.”
Ao “mushita.”
Tnn., “yale Maneno Kumi.”
Ao “kutaniko.”
Ao “mabonde ya mito yenye maji.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mbingu za juu sana.”
Tnn., “kutahiri govi la.” Govi ni ngozi yenye kufunika sehemu ya mbele ya kiungo cha uzazi cha mwanaume mwenye hajatahiriwa.
Tnn., “na musifanye shingo yenu kuwa ngumu tena.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “yatima.”
Ao “nafsi.”
Ao “mupaka leo.”
Tnn., “mbegu yao.”
Ni kusema, kwa kutumia njia fulani yenye inatumia nguvu za muguu, ikuwe gurudumu la maji ao kuchimba na kufungua mifereji ya maji.
Angalia Maana ya Maneno.
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “katikati ya macho yenu.”
Ni kusema, ile Bahari Kubwa, Mediterania.
Ao “kutoa.”
Ao “mahali jua linashuka.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “jambo lenye anafikiri kuwa sawa.”
Tnn., “milango yenu mikubwa.”
Ao “katika tamaa yote ya nafsi yako.”
Tnn., “ndani ya milango yako yote mikubwa.”
Ao “eko.”
Tnn., “ndani ya milango yako mikubwa.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “nafsi yako inatamani.”
Ao “katika tamaa yote ya nafsi yako.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “katika tamaa yote ya nafsi yako.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi.”
Ao “nafsi.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “rafiki yako mwenye kuwa kama nafsi yako mwenyewe.”
Ao “chenye kilifanywa kitakatifu kwa kupigwa marufuku.”
Ao “kusikiliza sauti ya.”
Tnn., “kutia (kunyoa) upara katikati ya macho yenu.”
Ao “mali yake yenye anapendezwa nayo sana.”
Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
Ao “eko.”
Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.
Pezi ni kiungo cha samaki chenye kinamusaidia kuogelea.
Pezi ni kiungo cha samaki chenye kinamusaidia kuogelea.
Ao “kidudu.”
Tnn., “milango yenu mikubwa.”
Ao “zaka.”
Ao “nafsi yako inatamani.”
Ao “kitu chochote chenye nafsi yako inakuomba.”
Ao “yatima.”
Ao “kukopesha kwa kuomba mutu aache kitu fulani.”
Ao “kumukopesha kwa kumuomba aache kitu fulani.”
Tnn., “moyo wako haupaswe.”
Tnn., “ngombe-dume wako.”
Ao “eko.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “eko.”
Angalia Nyongeza B15.
Mundu ni kisu chenye kujikunja chenye kinatumiwa ili kuvuna.
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “yatima.”
Ao “Makao ya Muda.”
Ao “Makao ya Muda.”
Tnn., “ndani ya milango yako yote mikubwa.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “kata-midomo.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “kinywa cha.”
Ao “kitabu cha kukunjwa.”
Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
Ao “nafsi yake inatamani.”
Ni kusema, mahali kwenye Yehova anachagua kuwa nafasi kubwa ya ibada.
Ao “kutaniko.”
Tnn., “kwa sababu moyo wake uko moto.”
Ao “anaumiza nafsi yake.”
Tnn., “Jicho lako halitamusikilia huruma.”
Tnn., “kusimama juu ya mutu mwingine.”
Tnn., “kinywa cha.”
Tnn., “Jicho lako halitasikia.”
Ao “Nafsi itakuwa.”
Ao “nafsi.”
Ao “eko.”
Ao “asifanye moyo wa ndugu zake uyeyuke kama moyo wake mwenyewe.”
Ao “bonde la muto.”
Ao “kulingana na nafsi yake.”
Ao “eko.”
Tnn., “bibi wawili, mumoja anapendwa na mwingine anachukiwa.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “nyumba ya; kiota cha.”
Ao “kisha anamukataa.”
Ao “eko.”
Ao “anamukataa.”
Ao “eko.”
Ao “faini.”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “ukahaba.”
Ao “anamuua, anaua nafsi.”
Tnn., “asifunue upindo wa nguo ya baba yake.”
Ao “aite ubaya juu yenu.”
Ao “chenye kuchafua.”
Ao “shahawa.”
Ni kusema, musalani, choo, W.C.
Ao “mapato ya.”
Tnn., “imbwa.”
Ao “kutosheleza nafsi yako.”
Mundu ni kisu chenye kujikunja chenye kinatumiwa ili kuvuna.
Ao “anamukataa.”
Ao “kukamata uzima wa; kukamata nafsi ya.”
Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “ukoma” liko na maana nyingi na linaweza kutia ndani magonjwa mbalimbali yenye kuambukizwa ya ngozi. Linaweza pia kutia ndani magonjwa fulani yenye kuambukizwa yenye yanapatikana kwenye nguo na ndani ya nyumba.
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi yake inategemea.”
Ao “yatima.”
Ao “eko.”
Ao “jina la nyumba yake.” Tnn., “jina lake.”
Tnn., “Jicho lako halipaswe.”
Tnn., “efa na efa.” Angalia Nyongeza B14.
Tnn., “matunda.”
Ao pengine, “anaangamia.”
Ao “yatima.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mali yake yenye anapendezwa nayo sana.”
Ao “kuyapakaa chokaa.”
Ao “utayapakaa chokaa.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Ao “fundi wa mbao na metali.”
Ao “Ikuwe vile!”
Ao “yatima.”
Tnn., “amefunua upindo wa nguo ya baba yake.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “amupige na kumuua.”
Ao “nafsi ya damu yenye haina hatia.”
Tnn., “Uzao wa tumbo lako la uzazi utabarikiwa.”
Tnn., “Uzao wa tumbo lako la uzazi.”
Ao “bawasiri.”
Ni ugonjwa fulani wa ngozi.
Ao “muvurugiko wa moyo.”
Tnn., “mezali.”
Ao “Vidudu vyenye kuruka vitavamia.”
Tnn., “milango yako yote mikubwa.”
Tnn., “uzao wa tumbo lako la uzazi.”
Ao “mwororo.”
Ao “mwororo.”
Ao “nafsi yenye kupoteza tumaini.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “majaribu makubwa yenye.”
Pengine neno la Kiebrania lenye linatumiwa hapa linahusiana na maneno “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.
Tnn., “kitu chenye kumwangiwa maji muzuri pamoja na kitu chenye kukauka.”
Tnn., “hawakukuwa wamepewa.”
Tnn., “uyarudishe katika moyo wako.”
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “atatahiri.”
Angalia Maana ya Maneno.
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “haiko mbali.”
Tnn., “kuenda inje na kuingia ndani.”
Ao “Makao ya Muda.”
Tnn., “watoto wadogo.”
Tnn., “milango yako mikubwa.”
Ao “mukamate nafasi zenu.”
Tnn., “kulala pamoja na baba zako.”
Tnn., “Uutie katika vinywa vyao.”
Tnn., “kunenepa.”
Inaonekana ni Mungu.
Tnn., “shingo yenu ngumu.”
Ao pengine, “jamii ya wanadamu.”
Ao “nyumba yake; kiota chake.”
Ni kusema, Yakobo.
Tnn., “mafuta ya kondoo.”
Tnn., “mafuta ya figo ya ngano.”
Ao “maji.”
Maana yake “Mutu Munyoofu,” jina la heshima la Israeli.
Ao “wivu wangu.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao pengine, “lenye halisikie shauri.”
Ao “atasikitika kwa sababu ya.”
Ao “inakula zabihu zao za muzuri sana.”
Ao “atasafisha.”
Jina la kwanza la Yoshua. Hoshea ni ufupisho wa jina Hoshaya, lenye kumaanisha “Mwenye Aliokolewa na Yah; Yah Ameokoa.”
Haya ni maneno ya kishairi yenye kumaanisha kifo.
Maana yake “Mutu Munyoofu,” jina la heshima la Israeli.
Ao “imepambana kwa ajili ya.”
Neno “yako” katika mustari huu linahusiana na Mungu.
Tnn., “katika pua yako.”
Ao “viuno vya.”
Ao pengine, “milima ya mashariki.”
Ao “kupiga.”
Tnn., “watanyonya wingi wa.”
Ao “hazina zenye kufichwa za.”
Ao “anawe.”
Tnn., “Na kama vile siku zako ziko ni vile nguvu zako zitakuwa.”
Ao pengine, “mahali pao pa juu.”
Ni kusema, ile Bahari Kubwa, Mediterania.
Tnn., “mbegu yako.”