Kusanyiko La Wilaya 1996—Marekebisho
1 Hakika ni jambo lenye kupendeza kuwako wakati wa karamu za kiroho, iwe wakati wa mikutano ya kutaniko kama vile kwenye makusanyiko ya mzunguko, makusanyiko ya pekee ya siku moja au makusanyiko ya wilaya. Kwa nini hilo? Kwa kuwa ushirika wa watu wanaomwogopa Mungu ni chanzo cha burudiko na kwamba habari mbalimbali za kiroho zinazozungumziwa zinatutia tena akilini mambo yaliyo ya lazima.
2 Muda wa miaka hii ya nyuma, maelfu ya watu wamejiunga nasi kwenye makusanyiko hayo ya kiroho, na wako wengi zaidi sikuzote kufanya hivyo. Kati ya 1985 na 1995, hesabu ya makutaniko imepita toka 49,716 hadi 78,620. Kwa kuwa Yehova anachochea kazi ya kukusanya, inafaa kutayarisha makusanyiko ya wilaya na ya mzunguko mengi zaidi. (Isaya 60:22) Katika eneo letu lenyewe tu, tunaweza kuona matokeo ya ongezeko la ajabu la hesabu ya makutaniko juu ya makusanyiko ya wilaya: 35 yalifanyika katika 1995 kwa kulinganisha na 18 katika 1985. Ukubwa wa kazi ya lazima ya kutayarisha na kuendesha vizuri makusanyiko yote hayo umeongezeka zaidi. Kwa kuwa tunakusanyika ili kufaidika na karamu ya kiroho, ni jambo la hekima kurekebisha mambo yanayohusu kazi za kimwili.
3 Inafaa Kuchukua Mipango Mipya: Tunatafuta baraka ya Yehova, kwani tunasonga mbele. Sisi ni wenye furaha kuona kwamba Yehova anatoa kwa watumishi wake hekima na akili wanayohitaji. Tunapaswa kutambua kwamba kwa njia ya mtumwa mwaminifu na mwenye akili Yesu Kristo anaongoza mambo kwa matokeo mazuri, hivi kwamba kusudi la Yehova linatimia kwa namna ya ajabu. (Mt. 24:45-47; Kol.1:9, 10) Hivyo Baraza Liongozalo limechukua uamuzi ufuatao, ambao tunatangaza: Kuanzia makusanyiko ya wilaya 1996, makusanyiko ya mzunguko na makusanyiko ya pekee ya siku moja ya Septemba 1996, chakula hakitahudumiwa tena. Kila mmoja ataleta chakula na kinywaji chake mwenyewe.
4 Mabadiliko Yanayotazamiwa: Muda wa miaka katika hiyo chakula chepesi kilitayarishwa na kuhudumiwa, ilionekana wazi kwamba mambo madogo ni ya lazima. Kazi iliyotimizwa kwa moyo wote na wale wote waliojitolea kwa hiari ni yenye thamani isiyolinganika; hakika wanastahili shukrani zetu. Lakini tangu sasa, kwa msaada wa marekebisho mapya, maelfu ya akina ndugu na dada waliotoa msaada wao kwa kuongoza magari, na pia kununua, kupika, kutuma na kuhudumia chakula, wataweza hivyo kutumia wakati wao kwa makusudi mengine ya kitheokrasi ya lazima, na hasa kufaidika na ushirika wa kindugu wakati wa makusanyiko. Kwa upande mwingine, wafanya-kazi wa kujipendea waliokuwa wakishughulika kwa ajili ya utumishi wa chakula wataweza kutegemeza utumishi mbalimbali mwingine, kwa mfano utumishi wa ukaribishaji na utumishi wa usafi. Hivyo, mzigo wa kila mmoja utakuwa mwepesi na haitakuwa tena lazima kwamba wafanya-kazi wa kujipendea wengi watumike mpaka saa za nyuma sana jioni, asubuhi mapema au wakati wa programu mbalimbali, ndivyo ilivyokuwa kwa utumishi wa chakula.
5 Tutegemeze Mipango Iliyochukuliwa: Sosaiti inashukuru sana, akina ndugu na dada, kwa tegemezo bora ambalo, muda wa miaka, mlitoa “kwa moyo kamili” kwenye mipango iliyochukuliwa kwenye makusanyiko, kutia ndani ile inayohusu utumishi wa chakula. (1 Sik. 29:9) Na hakuna shaka kwamba akina ndugu na dada ambao walitumika kwa kujipendea na kwa ukarimu, wakionyesha hivyo shukrani yao kwa matendo, wataendelea kuonyesha roho ileile.—Mit. 11:25; Lk. 16:9.
6 Nini la Kufanya Ili Kujipatia Chakula: Kwa sababu ya marekebisho mapya, itafaa kwamba familia zijiletee, peke yazo, yale zinazohitaji ili kujipatia chakula wakati wa mapumziko ya saa sita. Tunathamani zaidi faida bora ambazo programu ya kiroho inatutolea. Ingekuwa kukosa hekima kutia umuhimu usiofaa juu ya chakula cha kimwili. Kwa upande huo, ni jambo la lazima kwamba kila mmoja ‘ajiingize mambo yaliyo ya muhimu zaidi.’ (Flp. 1:9, 10a) Tutatambua kwamba ikiwa tunaridhika na chakula chepesi, tutakuwa wenye makini zaidi na tutafaidika zaidi na programu ya kisha-mchana. Ni kwa sababu hiyo kila mmoja angepaswa kuleta vyakula vyepesi, lakini vyenye kujenga mwili. Kwa mfano, tukumbuke kwamba alipolisha makutano Yesu aliwatolea tu chakula aina mbili, mkate na samaki.—Mt. 14:16-20; ona Lk 10:42a.
7 Mapumziko ya saa sita yatakuwa mafupi zaidi kuliko makusanyiko yaliyotangulia. Hata hivyo, kutakuwa bado na wakati wa kutosha ili kula chakula chepesi na kufaidika na ushirika wa wamoja na wengine kabla ya mwanzo wa programu ya kisha-mchana. Akina ndugu na dada wanaokaa katika mji ambamo kusanyiko linafanyika, au katika mitaa ya kandokando yake, na wanaorudi nyumbani kwao kila jioni, hawatakuwa kamwe na matatizo ya kupika vyakula fulani kwa ajili ya kila mshiriki wa familia. Tunaweza kufanya kidogo kama vile watoto wanaobeba shuleni mikate midogo, matunda, biskwiti na kitu fulani cha kunywa. Watu wengi wanatumia chakula kama hicho mahali pao pa kazi.
8 Ni wazi kwamba mambo yote hayatakuwa rahisi kwa wale wanaokuja kutoka mahali pengine. Itawafaa kutayarisha chakula cha kutumia saa sita. Wamoja wataona kwamba chakula chepesi kutokana na mboga-mboga na matunda kitatosha, na wataweza kula makwao kile watakachohitaji. Inawezekana pia kununua kila siku kile kinachohitajiwa kwa kiamsha-kinywa katika soko ya mji ambamo kusanyiko linafanyika.
9 Kila mahali pa kusanyiko pakiwa ni Jumba la Ufalme kubwa, tutaonyesha hekima kwa kuangalia kutotokeza hali kama ya piki-niki wakati wa mapumziko ya saa sita. Na kama vile hatuli wakati wa mikutano, hatutakula wala kunywa wakati wa programu mbalimbali. Haitaruhusiwa kuleta vibweta vikubwa vya barafu ili kulinda vinywaji kwa ajili ya familia kwenye mahali pa kusanyiko. Vinaweza kuwa vyenye hatari, na havipaswi kufunga njia au kuwekwa juu ya viti vya kukalia. Ni vema zaidi kutumia mifuko midogo ya plastiki au karatasi ili kubeba vyakula fulani fulani ambavyo mmekusudia kula saa sita. Ikiwa ni lazima, kibweta kidogo cha barafu kinachoweza kuingia chini ya kiti kinaweza pia kuwa chenye kufaa. Haitafaa kukiweka juu ya kiti. Hatimaye, tunakumbusha kwamba matumizi ya vinywaji venye alkoli (divai, bia, n.k.) havifai kwenye kusanyiko la Kikristo.
10 Itawafaa pia kuangalia aina ya vyombo ambavyo mtakavyoleta mahali pa kusanyiko. Mnaweza kutumia machupa ya kulinda joto (thermos) kwa ajili ya vinywaji vya moto. Vyombo vinavyotengenezwa kwa bilauri, hata viweje, ni vyenye hatari. Vinakatazwa katika mahali pengi pa kusanyiko. Ikiwa mnanunua vinywaji vya baridi visivyolindwa ndani ya karatasi ya plastiki au ya aluminium, itakuwa vizuri hivyo kuvihamishia ndani ya vyombo vidogo visivyoweza kuvunjika ambavyo vinaweza kuingia kwa wepesi chini ya kiti.
11 Faida Nyingine: Tunaelewa hekima yote ya marekebisho haya mapya. Tutaweza sote kukaza akili kikiki juu ya mambo ya kiroho yanayozungumziwa katika hotuba mbalimbali, hiyo ikiwa ndiyo sababu halisi ya kufanyika kwa makusanyiko. Tunafaidika na ushirika wa ndugu na dada zetu, pia na programu. Kwa hiyo, badala ya kutoka mahali pa kusanyiko wakati wa mapumziko ya saa sita ili kwenda kutafuta kitu fulani cha kula, ni vizuri zaidi kuleta kile tunachohitaji. Tutaweza hivyo kupitisha wakati pamoja na washiriki wenzetu Wakristo na hatutakosa hivyo hata hotuba moja ya programu ya kisha-mchana.
12 Baada ya kujengwa vizuri kiroho, wengine, pamoja na familia zao na marafiki zao, watataka labda kufaidika kwa muda na ushirika wa kindugu na kuzungumzia mambo tuliyojifunza muda wa mchana wote, huku wakitumia mlo mwepesi katika hoteli au mkahawa. Wale watakaojiweza watachagua labda kurudi makwao ili kula chakula cha jioni kama siku nyingine.
13 Hakika sisi ni wenye furaha kuwako wakati wa karamu za kiroho ambazo ni makusanyiko. Tunapokea huko vichapo vipya, mafundisho ya hali ya juu na mashauri yenye kutenda kazi. Hizo ndizo faida ambazo sote tunakumbuka. Tuna pia furaha ya kujikuta katikati ya watumishi wa Mungu. Mezali 10:22 inasema: “Baraka ya [Yehova] inatajirisha, wala hachanganyi huzuni nayo.” Ndivyo ilivyo kwani sisi, watumishi wa Yehova, hatuhudhurii makusanyiko tukiwa wenye kulazimisha mambo ya kimwili au kwa kutafuta raha yetu. Ni pamoja na tamaa yenye kujenga ya kufaidika na makusanyiko kikamilifu kwa upande wa kiroho kwamba tunakusanyika, na Yehova anatuzawabisha kwa uwingi kwa sababu ya hali ya akili ambayo tunaonyesha.—1 Tim. 6:6-8; Ebr. 11:6.
14 Makusanyiko ni matukio yenye kutia moyo yanayotukumbusha wapi tulipo katika mavuno ya kiroho. (Yn. 4:35, 36) Sura ya 54 ya kitabu cha Isaya inafunguliwa kwa mwaliko unaotolewa kwa tengenezo la Yehova linalofananishwa na mwanamke, mwaliko wa kujitayarisha kuona ongezeko lenye shangwe. Kama alivyotabiri Isaya, tengenezo lingepaswa kutazamia kuongezeka tena, kupanuka na likichochewa na nguvu mpya: “Ongeza pahali pa hema yako, na wanyoshe mapazia ya pahali pako pa kukaa; usizuize; ongeza urefu wa kamba zako; kaza vigingi vya hema yako. Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto.” Utimizo wa unabii huo wenye kuvutia unaonekana katika ongezeko la ajabu la ibada safi leo.—Isaya 54:1-4.
15 Ndiyo, hakika, marekebisho mapya ni alama ya usawaziko wa akili. Wahudhuriaji wote wataweza kufaidika na programu ya kiroho wakati wa makusanyiko, kukiwa na kadiri iliyo ndogo iwezekanavyo ya vitu vya kupumbazisha. Tupo hakika kwamba mipango hii itabarikiwa na Yehova, kwani itawezesha kukabiliana vizuri na ongezeko. Kwa kukaza kikiki akili yetu juu ya kile kilicho cha lazima, tutafaidika na siku nzima njema katika ushirika na ndugu na dada zetu, na tutatajirika kiroho. Tunamwomba Yehova abariki jitihada zote ambazo tunaendelea kufanya ili tuje kujilisha kwenye meza ya Yehova.—Ona Kumb. 16:14, 15.
[Box on page 4]
Faida Zinazotokana na Kukomeshwa kwa Utumishiwa wa Chakula
◼ Kazi ndogo kabla, wakati wa na kisha kusanyiko, jambo linalowezesha kufaidika zaidi na ushirika wa akina ndugu na dada.
◼ Hakuna chombo cha kusafisha kwa ajili ya utumishi wa chakula.
◼ Watu wengi zaidi wataweza kufaidika kikamilifu na programu ya kiroho.
◼ Wafanya-kazi wa kujipendea wengi zaidi kwa ajili ya utumishi mwingine mbalimbali.
◼ Wakati zaidi ili kukaza akili kwenye miradi mingine ya kitheokrasi.
Vitu Tunavyoweza Kuleta kwa Ajili ya Mlo wa Saa Sita
◼ Chakula chepesi, rahisi na chenye kujenga mwili.
◼ Matunda, mkate.
◼ Vibweta vidogo vya barafu ili kulinda kinywaji, ikiwezekana.
◼ Vinywaji, maji ya matunda na maji, katika vyombo visivyoweza kuvunjika.
Vitu Ambavyo HATUPASWI Kuleta Mahali pa Makusanyiko
◼ Vinywaji vya alkoli.
◼ Vyombo vilivyotengenezwa kwa bilauri.
◼ Vibweta vikubwa vya barafu ili kulinda vinywaji vya familia.