Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 3/10 uku. 3
  • Tusaidiane Vizuri Tunapohubiri Pamoja

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tusaidiane Vizuri Tunapohubiri Pamoja
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2010
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Saidia Yule Unayehubiri Naye
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri​—Umutegemeze Yule Unayehubiri Naye
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
  • Tutiane Moyo Tunapokuwa Katika Kazi ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2010
km 3/10 uku. 3

Tusaidiane Vizuri Tunapohubiri Pamoja

1. Kuhubiri na mutu mwingine kuna faida gani?

1 Wakati mmoja Yesu aliwatuma wanafunzi wake 70 ili kuhubiri, na ‘aliwatuma wawili-wawili.’ (Luka 10:1) Bila shaka mpango huo ulitolea wanafunzi nafasi ya kusaidiana na kutiana moyo walipokuwa wakihubiri. Tunapohubiri pamoja na mutu mwengine, namna gani tunaweza kusaidiana?

2. Wakati mhubiri mwenzako anapohubiri, namna gani unaweza kumsikiliza na kwa nini?

2 Kwa Kusikiliza: Sikiliza kwa uangalifu mwenzako anapohubiri. (Yak. 1:19) Andiko linaposomwa fuata katika Biblia yako. Mtazame yule anayesema, iwe ni mhubiri mwenzako ao msikilizaji. Ikiwa unafuata kwa uangalifu mazungumzo, hilo litamtia moyo msikilizaji afuate kwa uangalifu pia.

3. Wakati gani tunaweza kumsaidia yule tunayehubiri naye?

3 Kwa Kujua Wakati Unaofaa Ili Kusema: Tunapohubiri, ikiwa ni mhubiri mwenzetu ndiye ameanzisha mazungumzo, tunaonyesha heshima kwa kumuacha aongoze mazungumzo. (Rom. 12:10) Tutaepuka kumkatiza-katiza. Ikiwa anasahau jambo fulani ao msikilizaji anatokeza kipingamizi ao ulizo, na hivyo mhubiri mwenzetu anaomba msaada, tutajikaza kuongeza mawazo ya zaidi kwa yale aliyotoa kuliko kuanzisha habari iliyo tofauti na ile anayozungumzia. (Met. 16:23; Mhu. 3:1, 7) Ikiwa tunasema jambo fulani, maneno yetu yanapaswa kusaidia msikilizaji aelewe ushahidi unaotolewa.—1 Kor. 14:8.

4. Ni nini kitakachotusaidia tuwe na furaha na kupata matokeo mazuri katika mahubiri?

4 Wale wanafunzi 70 walipomaliza mahubiri ‘walirudi wakiwa na shangwe.’ (Luka 10:17) Tunapohubiri pamoja na mhubiri mwingine, sisi pia tutakuwa na furaha na kupata matokeo mazuri ikiwa tunasikiliza na kujua wakati unaofaa ili kusema.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine