Tusaidiane Vizuri Tunapohubiri Pamoja
1. Kuhubiri na mutu mwingine kuna faida gani?
1 Wakati mmoja Yesu aliwatuma wanafunzi wake 70 ili kuhubiri, na ‘aliwatuma wawili-wawili.’ (Luka 10:1) Bila shaka mpango huo ulitolea wanafunzi nafasi ya kusaidiana na kutiana moyo walipokuwa wakihubiri. Tunapohubiri pamoja na mutu mwengine, namna gani tunaweza kusaidiana?
2. Wakati mhubiri mwenzako anapohubiri, namna gani unaweza kumsikiliza na kwa nini?
2 Kwa Kusikiliza: Sikiliza kwa uangalifu mwenzako anapohubiri. (Yak. 1:19) Andiko linaposomwa fuata katika Biblia yako. Mtazame yule anayesema, iwe ni mhubiri mwenzako ao msikilizaji. Ikiwa unafuata kwa uangalifu mazungumzo, hilo litamtia moyo msikilizaji afuate kwa uangalifu pia.
3. Wakati gani tunaweza kumsaidia yule tunayehubiri naye?
3 Kwa Kujua Wakati Unaofaa Ili Kusema: Tunapohubiri, ikiwa ni mhubiri mwenzetu ndiye ameanzisha mazungumzo, tunaonyesha heshima kwa kumuacha aongoze mazungumzo. (Rom. 12:10) Tutaepuka kumkatiza-katiza. Ikiwa anasahau jambo fulani ao msikilizaji anatokeza kipingamizi ao ulizo, na hivyo mhubiri mwenzetu anaomba msaada, tutajikaza kuongeza mawazo ya zaidi kwa yale aliyotoa kuliko kuanzisha habari iliyo tofauti na ile anayozungumzia. (Met. 16:23; Mhu. 3:1, 7) Ikiwa tunasema jambo fulani, maneno yetu yanapaswa kusaidia msikilizaji aelewe ushahidi unaotolewa.—1 Kor. 14:8.
4. Ni nini kitakachotusaidia tuwe na furaha na kupata matokeo mazuri katika mahubiri?
4 Wale wanafunzi 70 walipomaliza mahubiri ‘walirudi wakiwa na shangwe.’ (Luka 10:17) Tunapohubiri pamoja na mhubiri mwingine, sisi pia tutakuwa na furaha na kupata matokeo mazuri ikiwa tunasikiliza na kujua wakati unaofaa ili kusema.