Mashahidi wa Yehova—Watu Wanaotenda kwa Imani, Sehemu ya 2: Kuangaza Nuru
Katika mwaka wa 1919 kisha Ndugu Rutherford na wenzake kufunguliwa, Wanafunzi wa Biblia walikuwa na kazi kubwa mbele yao. Kama inavyoonyeshwa katika video Mashahidi wa Yehova—Watu Wanaotenda kwa Imani, Sehemu ya 2: Kuangaza Nuru, Wanafunzi wa Biblia wangepingwa na watu wengi, ujuzi wao wa Maandiko ungeendelea kuongezeka, na imani yao ingekuwa nguvu zaidi. (Met. 4:18; Mal. 3:1-3; Yoh. 15:20) Kisha kufuata video hii, je, unaweza kujibu maulizo yafuatayo?
(1) Ili kueneza habari njema, Wanafunzi wa Biblia walitumia njia gani mbalimbali za kuhubiri? (2) Ni mambo gani ya maana yaliyozungumuziwa kwenye mikusanyiko ya pekee sana katika miaka ya 1931 na 1935? (3) Ni habari gani ya maana iliyozungumuziwa katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 mwezi wa 11, 1939? (4) Eleza yale yaliyotukia katika jumba lililoitwa Madison Square Garden wakati Ndugu Rutherford alikuwa akitoa hotuba yenye kichwa “Serikali na Amani.” (5) Ni maelezo gani ya maana sana yaliyozungumuziwa katika hotuba ya Ndugu Knorr yenye kichwa “Amani—Je, Inaweza Kudumu?” (6) Katika mwaka wa 1942, Mashahidi wa Yehova walifanya mipango gani ili kupanua kazi yao ya kuhubiri? (7) Eleza mapambano fulani ya kisheria yaliyofanyika huko Etas-Unis, Canada, na Grèce. (8) Namna gani Masomo ya Gileadi ilisaidia kuenea kwa kazi ya kuhubiri? (9) Ni kazi gani ya maana iliyoanzishwa katika mwaka wa 1946, na kwa nini? (10) Mashahidi wa Yehova walikamata hatua gani ili kuhakikisha kama mwenendo wao ulipatana na kanuni za Biblia? (11) Fasiria mabadiliko fulani yaliyofanywa katika mwaka wa 1970 ili tengenezo liongozwe kupatana na mufano unaoonyeshwa katika Biblia. (12) Namna gani kutazama video hii kumekusaidia kuelewa vizuri zaidi kama hili ni tengenezo la Yehova na kama ni yeye ndiye anayeliongoza? (13) Namna gani video hii imekusaidia ili uazimie zaidi kuendelea kuhubiri kwa bidii ijapokuwa vizuizi? (14) Namna gani tunaweza kutumia video hii ili kusaidia watu wa jamaa yetu, watu tunaojifunza nao Biblia, na watu wengine?
Kila siku inayopita, mambo fulani yanaongezeka kuhusiana na historia ya Mashahidi wa Yehova. Historia ya Mashahidi wa sasa itakapoandikwa, itaonyesha nini kuhusu jitihada zetu katika mahubiri? Acheni basi tufuate mufano wa ndugu zetu wa zamani kwa kuendelea kufanya ‘nuru iangaze,’ na tufanye hivyo kwa bidii!—2 Kor. 4:6.