“Nitakamata Kitabu Chako Kama Unakamata cha Dini Yetu”
Watu fulani tunaohubiria wanasema hivyo. Kwa kuwa hatubadili vitabu vyetu na vitabu vya kidini ambavyo vinaeneza mafundisho ya uongo, namna gani tunaweza kujibu kipingamizi hicho kwa busara? (Rom. 1:25) Tunaweza kusema: “Asante kwa pendekezo lako. Kitabu hicho kinasema nini kuhusu namna ambavyo Mungu atamaliza matatizo ya wanadamu? [Acha mutu ajibu. Ikiwa anakuomba usome kitabu cha dini yake ili upate jibu, unaweza kumukumbusha kwamba haukumutolea kitabu chako bila kumujulisha mambo yanayozungumuziwa ndani. Kisha usome ao utaje maneno yaliyo katika Mathayo 6:9, 10.] Yesu alionyesha kwamba Ufalme wa Mungu utafanya mapenzi ya Mungu yatendeke duniani. Kwa hiyo, ninasoma tu vitabu vya kidini ambavyo vinakazia Ufalme wa Mungu. Je, ninaweza kukuonyesha katika Biblia mambo fulani ambayo Ufalme wa Mungu utafanya?”