Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kumujibia Musikilizaji Mwenye Kukasirika
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Watu wengi ambao tunahubiri ni wenye adabu. Hata hivyo, Yesu alitabiri kwamba watu fulani watatuchukia. (Yoh. 17:14) Kwa hiyo, hatupaswe kushangaa tukikutana na mutu mwenye kukasirika. Wakati tunakutana na musikilizaji mwenye kukasirika, tunapaswa kumujibia kwa njia yenye itafurahisha moyo wa Yehova, Mungu ambaye tunawakilisha. (Rom. 12:17-21; 1 Pet. 3:15) Kufanya hivyo kunaweza kuzuia hali kuwa mubaya zaidi. Pia, hilo litamutolea ushahidi musikilizaji na hata watu wengine, na linaweza kufanya wawe tayari kusikiliza wakati Mashahidi wa Yehova watawatembelea tena.—2 Kor. 6:3.
Tumikisha Shauri Hili Katika Mwezi:
Mufanye mazoezi wakati wa ibada yenu ya familia.
• Kisha kuachana na musikilizaji mwenye kukasirika, uzungumuze na muhubiri mwenzako juu ya maneno ambayo mungetumia ili kumujibu kwa njia nzuri zaidi.