Turudi Kuwaona Watu Walioonyesha Kupendezwa
1 Wakati wa kutolea kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele, msemaji alifasiria kwamba “watakapofikia mwisho wa kitabu hiki, watu wanyofu wangepaswa kuwa wamejifunza mengi zaidi ili kuweza kuchukua msimamo upande wa Yehova na kubatizwa.” Kitabu hicho kimekusudiwa ili kufundisha haraka ukweli. Kinatoa habari fupi zinazoweza kuwachochea watu kufanya maendeleo ya kiroho. Kinatoa ukweli kwa njia iliyo wazi, bila kupoteza wakati kuonyesha mafundisho ya uongo. Kutumia chombo hicho kwa matokeo kunataka kurudi kuwaona wale walionyesha kupendezwa.
2 Ikiwa tulizungumza na mtu asiyeamini katika Mungu lakini aliyeonyesha kupendezwa fulani, tungeweza kuanzisha mazungumzo kwa kufungua kitabu kwenye picha ya kurasa 4 na 5 na kusema:
◼ “Mara ya mwisho nilipokuja, tuliangalia pamoja picha hii nzuri ajabu inayoonyesha hali za maisha mazuri. Tunakuta ulizo hili la picha: ‘Ni lazima ufanye nini ili uyafurahie?’ Wewe unafiri nini? [Tuache mtu ajibu.] Biblia inatambulisha waziwazi mojawapo ya matakwa ya msingi. [Tusome Yohana 17:3.] Ujuzi ni wa lazima ili tuwe na imani katika Mungu. Njia bora ya kujifunza yale tunayopaswa kujua ni kuanza funzo la hatua kwa hatua la Biblia.” Tufungue kitabu kwenye sura ya kwanza na tuonyeshe mawazo fulani yenye kutia moyo yanayopatikana kwenye mafungu 1 mpaka 5. Tufasirie jinsi tunavyoongoza funzo la Biblia, na tupendekeze kurudi kuendeleza mazungumzo.
3 Ikiwa tunarudi na nia ya kuendeleza mazungumzo tuliyofanya juu ya Mungu kuruhusu ubaya, tunaweza kusema:
◼ “Nilipopita mara yangu ya mwisho, tulizungumza juu ya [tukumbushe tukio tulilotaja.] Hilo lilituongoza kujiuliza kwa nini Mungu anaruhusu mateso mengi ulimwenguni. Ulifikia uamuzi wa mwisho gani? [Tuache msikilizaji ajibu.] Ni jambo lenye kutia moyo kujua kwamba si Mungu aliye chanzo cha hali hizi zinazotesa.” Tufungue kitabu Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele kwenye kurasa 71-2 na tuzungumzie mawazo ya kibiblia yanayopatikana katika mafungu 3 mpaka 5. Tupendekeze kurudi ili kufasiria kwa nini tunaweza kuwa hakika kwamba kuruhusu kwa Mungu mateso kutamalizika hivi karibuni.
4 Ikiwa mtu tunayetembelea mara ya pili ana watoto na anapendezwa na maulizo ya kifamilia, tunaweza kusema:
◼ “Ninawaza wewe kama vile baba (au mama) wa familia, unawatakia watoto wako mema. Kwa kuwa haiwezikani kuwalinda na mambo yote yaliyo maovu, inafaa uwafundishe jinsi ya kupambana na magumu ya maisha. Jinsi gani unaweza kufikia hilo? [Tuache mtu ajibu.] Mojawapo ya mambo ya lazima zaidi ambayo wazazi wanaweza kutoa kwa watoto wao, ni malezi mazuri.” Tufungue kitabu Ujuzi kwenye kurasa 145-6 na tutie mkazo juu ya mashauri yenye kutenda kazi ya Biblia; tusisitize juu ya ulazima wayo na juu ya faida ambazo mtu hujipatia kwa kuyafuata. Tupendekeze kurudi ili kuonyesha jinsi ya kutumia kitabu hicho ili kwamba tuwe na maisha ya familia yenye furaha.
5 Ikiwa tunamtembelea tena mtu ambaye tulitolea ujumbe kwa kifupi, tunaweza kusema:
◼ “Halikuingia kamwe katika kusudi la Mungu kwamba tuzeeke na kufa. Alipenda kwamba tuishi milele katika paradiso duniani.” Tueleze picha ya kurasa 188-9. Tusome fungu 11 la ukurasa 184. Tuagane kukutana tena na mtu huyo kwa ajili ya ziara nyingine.
6 Kitabu hicho hakika ni njia ya ziada inayotumiwa na Yehova ili ‘kuendesha haraka’ kazi ya kukusanya inayotimizwa katika siku hizi za mwisho. (Is. 60:22) Ikiwa tunakitumia kwa matokeo, tutatolea ujuzi unaoweza kumwezesha mtu kupata uhai udumuo milele.