Tutumike kwa Nafsi Yetu Yote
1 Tunazo sababu nyingi za kuwa wenye shukrani kwa Yehova. Kwa mfano, yale aliyofanya wakati wa nyuma, yale anayotimiza kwa sasa na yale atakayofanya tena kwa wakati ujao. Shukrani ingepaswa kutusukuma kufanya nini? Zaburi moja ya Daudi inaleta jibu lifuatalo: “Nitabariki [Yehova] wakati wote; sifa yake itakuwa kinywani mwangu daima.”—Zab. 34:1.
2 Biblia inaonyesha waziwazi kwamba tunapaswa kuhubiri. Tunatimiza kazi hiyo ‘kwa nafsi yetu yote, kama kwa Yehova.’ (Kol. 3:23.) Ikiwa tunashiriki kwelikweli kwa nafsi yetu yote katika huduma, ni kwa kadiri gani tutaitimiza? Tunapofikiria upendo ambao Yehova alio nao kwetu, bila shaka moyo wetu unatusukuma kusema kwa bidii juu yake na makusudi yake ya ajabu. Tunayo nia ya kufanya yote tuwezayo kutimiza.
3 Tunaweza kutazamia kwa haki kwamba mtu anayetumikia kwa nafsi yake yote anatamani kuwa na akili yenye kukazwa kikiki juu ya utumishi wake mtakatifu. Mtunga zaburi, ambaye kwa wazi alikuwa akiona mambo kwa namna hiyo, alisema: “mara saba kila siku ninakusifu.” (Zab. 119:164) Wale wanaokubaliana na hisia-moyo za mtunga zaburi wanatafuta kufaidika na uwezekano mbalimbali walio nao wa kumsifu Yehova. Kulingana na hali yao, wanafanya yote wawezayo ili kutumika kwa bidii.
4 Tunazo Nafasi Nyingi za Kumsifu Yehova: Si lazima kungoja kuwa katika mahubiri ya mlango kwa mlango ili kuhubiri habari njema. Wafanyakazi wenzetu, wanashule wenzetu, washiriki wa familia yetu na marafiki zetu wanahitaji kusikia ujumbe wa Ufalme. Tunapokuwa katika safari, tunaweza kuanzisha mazungumzo, ambayo labda yataongoza kwenye utoaji wa ushuhuda kwa wafanyakazi wa hoteli, wafanyakazi wa mkahawa fulani au wafanyakazi wa bomba la mafuta ya motokaa (stesheni), au kwa madreva wa teksi. Nyumbani kwetu, tunaweza kutoa ushuhuda kwa majirani zetu. Ikiwa tunalazwa hospitalini, tunaweza kuhubiri kwa namna ya vivi hivi kwa waganga wa kike, kwa matabibu na wagonjwa wengine.
5 Ushuhuda wa Vivi Hivi Unatoa Matunda: Siku moja, walipokuwa wakitembea katika shamba la wanyama, Mashahidi wawili walianzisha mazungumzo na kijana mmoja mwanamume aliyekuwa akijitembeza na mtoto wake. Siku zilipopita, mwanamume huyo na mke wake walikubali ukweli. Kijana mwanamume huyo alikiri baadaye kwamba, punde kidogo tu kabla ya kukutana na Mashahidi wawili kwa mara ya kwanza, alisali kwa Mungu kwa kumwomba: ‘Ikiwa wewe unaishi, uniruhusu nikujue.’ Kwake, kukutana katika shamba la wanyama lilikuwa jibu la Yehova kwa sala yake.
6 Wale wanaojitoa kabisa kwa nafsi yao yote katika nia yao ya kuleta msaada wa kiroho kwa majirani zao wanajipatia shangwe kubwa. Wanajua kwamba utumishi huo, wanaotimiza “kwa moyo mkamilifu,” unamfurahisha Yehova.—1 Sik. 28:9.