Tunapaswa Kuwatembelea Tena Na Tena
1 Je! uliitikia ifaavyo mara ya kwanza mtu fulani aliposema nawe juu ya habari njema? Ikiwa sivyo, unapaswa kuwa mwenye shukrani kwamba Mashahidi wa Yehova walikutembelea tena na tena hadi ulipokubali mwishowe pendekezo la kujifunza Biblia. Ni vizuri kufikiria jambo hilo unapotumika tena na tena eneo ulilogawiwa.
2 Maisha ya watu ni yenye kubadilika daima. Wao hupambana na matatizo mapya na hali mpya, wanasikia matukio yenye kusumbua katika jamii au katika dunia, wanapata matatizo ya kiuchumi, au wanapatwa na ugonjwa au kifo katika familia. Mambo kama hayo yaweza kufanya watake kujifunza sababu ya taabu hizo. Tunapaswa kutambua mambo yanayolemea akili za watu na kutenda kwa kuleta ujumbe wenye kufariji.
3 Hii Ni Kazi ya Kuokoa Uhai: Fikiria waokoaji-uhai wakifanya kazi msiba unapotokea. Ingawa wengine wanaweza kuwa wakitafutia mahali ambapo waokokaji wachache hupatikana, hawalegei wala kuacha kwa sababu wafanyakazi wenzao hupata waokokaji wengi zaidi mahali pengine. Utendaji wetu wa kuokoa uhai haujakwisha bado. Kila mwaka, mamia ya maelfu ya wale wanaotaka kuokoka “dhiki kubwa” hupatikana.—Ufu. 7:9, 14.
4 “Kila mtu aitiaye jina la Yehova ataokolewa.” (Rom. 10:13-15) Maneno hayo yangepaswa yafanye kila mmoja wetu aone uhitaji wa kudumu katika kuhubiri. Tangu tulipoanza kumaliza eneo letu kwa kulitembelea, watoto wamekomaa na sasa wao ni watu wazima vya kutosha; wanaweza kufikiria wenyewe wakati wao ujao na kusudi la uhai. Hatuwezi kujua ni nani atakayesikiliza mwishowe. (Muh. 11:6) Wengi waliokuwa wapingaji wamekubali kweli. Kazi yetu ni ya kuendelea kuwapa watu nafasi ya kusikia na kuokolewa kutoka ulimwengu huu uliozeeka, si ya kuwahukumu. Kama walivyofanya wanafunzi wa kwanza wa Yesu, inafaa ‘tuendelee kwenda’ kwa watu na kujaribu kuchochea kupendezwa kwao katika ujumbe wa Ufalme.—Mt. 10:6, 7.
5 Jambo la kwamba bado njia ni yenye kufunguliwa kwetu ili tuhubiri ni wonyesho wa fadhili za Yehova. (2 Pet. 3:9) Kadiri tunavyofanya wengine wasikie tena na tena, tunaonyesha wazi upendo wa Mungu, na kwa hiyo tunamtukuza yeye.