Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Feb. 15
“Je, umekwisha kujiuliza namna gani unaweza kuongoza maisha yako katika njia bora zaidi na kufanya maamuzi ya maana? [Acha mtu ajibu.] Mwingine kati ya mwongozo ulio bora zaidi, kama vile ile Kanuni Iliyo Bora, unapatikana katika Biblia. [Soma Matayo 7:12.] Ni kanuni gani nyingine za kimungu ambazo zinaweza kutuletea faida za moja kwa moja? Utapata jibu katika gazeti hili.”
Amkeni! Feb. 22
“Labda umetambua ya kwamba mahali pengi pa kazi pamekuwa penye hatari zaidi. Gazeti hili lina mashauri mazuri kuhusu namna mahali hapo panaweza kufanywa kuwa penye usalama zaidi. Linaonyesha pia ya kwamba hali yetu njema inahusiana na kama tuna maoni yanayosawazika kuhusu kazi ya kimwili. Tafadhali soma gazeti hili.”
MNARA WA MLINZI Machi 1
“Kwa kuona yale yote ambayo yanatukia leo, wengi kati yetu wanajiuliza kile ambacho wakati ujao unatuwekea. Katika sala moja yenye kujulikana sana, Yesu Kristo alifunua sababu kwa nini tunaweza kuutazamia wakati ujao tukiwa na uhakika. [Soma Matayo 6:9, 10.] Wanadamu wanarudilia makosa yaliyofanywa muda mrefu uliopita. Lakini katika siku hizo, wale ambao walimtumikia Mungu walikuwa na wakati ujao wenye furaha. Gazeti hili linaonyesha namna gani sisi pia tunaweza kuwa kama wao.”
Amkeni! Machi 8
“Biblia inatia mkazo juu ya umaana wa elimu yenye nguvu. [Soma Mezali 2:10, 11.] Wengi kati yetu wanatambua namna lilivyo jambo la maana kwa watoto kuwa na walimu wanaostahili. Gazeti Amkeni! linakazia daraka la maana la walimu, namna tunavyopaswa kuthamini kujitolea kwao, na yale ambayo wazazi wanaweza kufanya ili kuwasaidia katika kazi hiyo ngumu.”