Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/08/10
“Unafikiri watu wana lazima ya nini ili kupata furaha? [Acha mutu ajibu. Kisha soma Mathayo 5:3.] Hilo ni jambo moja kati ya mambo ambayo Yesu alifundisha ili kupata furaha. Habari hii inazungumzia yale Yesu alifundisha kuhusu namna tunaweza kupata furaha ya kweli.” Zungumzia habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 16.
Amkeni! Mwezi wa 8
“Sinema nyingi leo zinaonyesha mambo ya mashetani, ulozi, na uchawi. Je, unawaza mashetani wako kweli? [Acha mutu ajibu. Kisha soma 1 Wakorintho 10:20.] Habari hii inaonyesha yale Biblia inasema kuhusu mashetani na jinsi tunavyoweza kuwa waangalifu.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 20.
Mnara wa Mlinzi 01/09/10
Taja habari yenye kuhangaisha watu katika eneo lenu. Kisha useme: “Je, umekwisha kujiuliza kwa nini watu wanafanya mabaya hayo? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatutolea sababu ya kuwa na tumaini. [Soma 2 Petro 3:13.] Gazeti hili linaonyesha yale ambayo Biblia inasema kuhusiana na sababu zinazowasukuma watu watende mabaya na namna Mungu atakavyomaliza mambo hayo.”
Amkeni! Mwezi wa 9
“Je, unafikiri kwamba telefone za mkononi, barua za internet, na njia zingine za kisasa za kupashana habari zimefanya watu wasijisikie kuwa pekee yao ao zinafanya watu wajisikie kuwa pekee yao? [Acha mutu ajibu.] Hili ni shauri moja linaloweza kutusaidia tupambane na hali ya mutu kujisikia kuwa pekee yake. [Soma Matendo 20:35.] Gazeti hili linatoa mashauri mengine yenye kufaa kutoka katika Biblia.”