Magazeti Yetu Yanachapishwa ili Kuvutia Watu wa Aina Yote
1. Namna gani mtumwa mwaminifu na mwenye busara anamuiga mtume Paulo?
1 Kama vile tu mtume Paulo alivyokuwa akipatanisha namna yake ya kutoa habari njema na hali za watu ili kuwapata “watu wa namna zote,” mtumwa mwaminifu na mwenye busara anatumia magazeti yetu ili kuwafikia watu wa kila aina na wenye kuamini mambo mbalimbali. (1 Kor. 9:22, 23) Tunaweza kufanya matumizi mazuri ya magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! ikiwa tunaelewa watu ambao watasoma magazeti hayo.
2. Gazeti Amkeni! linachapishwa ili kuvutia nani?
2 Amkeni!: Gazeti hili linachapishwa kwa ajili ya watu kama wale ambao mtume Paulo alisema nao alipozungumza na “wanaume wa Athene.” (Mdo. 17:22) Wanaume hao hawakuwa Wakristo, na walikuwa na uelewevu mdogo wa Maandiko. Amkeni! pia inachapishwa kwa ajili ya watu kama hao; wale walio na ujuzi mdogo wa Biblia ao wale ambao hawana ujuzi wowote wa Biblia. Labda hawajui lolote kuhusu mafundisho ya Kikristo, labda hawaamini mambo ya dini, ao labda hawajue kwamba Biblia inaweza kuwa na mashauri yenye kufaa wakati wetu. Kusudi la kwanza la Amkeni! ni kusadikisha wasomaji wake wajue kwamba kuna Mungu wa kweli. Kusudi lingine la gazeti hili ni kusaidia wasomaji waamini Biblia na kuelewa kwamba Mashahidi wa Yehova ni tofauti na vikundi vingine vya kidini.
3. Kila toleo la Mnara wa Mlinzi linachapishwa kwa ajili ya nani?
3 Mnara wa Mlinzi: Toleo la watu wote la Gazeti Mnara wa Mlinzi, linachapishwa kwa ajili ya wale wanaomuheshimu Mungu na kuheshimu Maandiko kwa kiasi fulani. Wana ujuzi fulani wa Biblia lakini hawaelewi vizuri mafundisho ya Biblia. Wao ni kama wale wasikilizaji wa Paulo ambao alisema kuwa ‘walimwogopa Mungu.’ (Mdo. 13:14-16) Toleo la funzo la Gazeti Mnara wa Mlinzi linachapishwa kwanza kwa ajili ya Mashahidi wa Yehova. Paulo alitumaini kwamba wale ambao walisoma barua zake walijua Maandiko na walikuwa na ujuzi sahihi wa kweli. (1 Kor. 1:1, 2) Leo pia, habari zinazopatikana katika toleo la funzo zinaandikwa kwa ajili ya wale wanaohuzuria mikutano na wanaojua usemi wa Mashahidi na kanuni zao.
4. Kwa nini tunapaswa kujua habari zilizo katika kila gazeti tunalotumia katika mahubiri?
4 Ijapokuwa tunatolea watu magazeti yakiwa pamoja, kwa kawaida tunazungumzia tu gazeti moja. Kwa hiyo, fanya kusudi lako liwe kujua habari zilizo katika kila gazeti. Hilo litakusaidia ukazie mambo yatakayovutia watu utakaokutana nao.