1 Mambo ya Nyakati
25 Tena Daudi na wakuu+ wa vikundi vya utumishi+ wakatenga kwa ajili ya utumishi sehemu ya wana wa Asafu, Hemani+ na Yeduthuni+ wenye kutoa unabii kwa vinubi,+ kwa vinanda+ na kwa matoazi.+ Na kutoka katika hesabu yao kukawa na wanaume rasmi kwa ajili ya utumishi wao. 2 Wa wana wa Asafu, Zakuri na Yosefu+ na Nethania na Asharela,+ wana wa Asafu chini ya amri ya Asafu+ mwenye kutoa unabii chini ya mfalme. 3 Wa Yeduthuni:+ wana wa Yeduthuni, Gedalia+ na Zeri+ na Yeshaya,+ na Shimei, Hashabia na Matithia,+ sita, chini ya amri ya Yeduthuni baba yao, aliyekuwa akitoa unabii akiwa na kinubi kwa ajili ya kumshukuru na kumsifu Yehova.+ 4 Wa Hemani:+ wana wa Hemani, Bukia,+ Matania,+ Uzieli,+ Shebueli na Yerimothi, Hanania,+ Hanani, Eliatha,+ Gidalti+ na Romamti-ezeri,+ Yoshbekasha,+ Malothi,+ Hothiri,+ Mahaziothi. 5 Hawa wote ndio waliokuwa wana wa Hemani, mwonaji+ wa mfalme katika mambo ya Mungu wa kweli ili ainue pembe yake; basi Mungu wa kweli akampa Hemani wana kumi na wanne na binti watatu.+ 6 Hawa wote ndio waliokuwa chini ya amri ya baba yao katika nyimbo kwenye nyumba ya Yehova, wakiwa na matoazi,+ vinanda+ na vinubi+ kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya Mungu wa kweli.
Chini ya amri ya mfalme kulikuwa Asafu na Yeduthuni na Hemani.+
7 Na hesabu yao pamoja na ndugu zao waliozoezwa nyimbo kwa Yehova,+ wote wakiwa wajuzi,+ ikawa 288. 8 Basi wakapiga kura+ kuhusu vitu vinavyopaswa kutunzwa, mdogo akiwa sawasawa na mkubwa,+ mwenye ujuzi+ pamoja na mwenye kujifunza.
9 Na kura ikatoka: ya kwanza ya Asafu kwa ajili ya Yosefu,+ ya pili ya Gedalia+ (yeye na ndugu zake na wanawe walikuwa 12); 10 ya tatu ya Zakuri,+ wanawe na ndugu zake, 12; 11 ya 4 ya Izri,+ wanawe na ndugu zake, 12; 12 ya 5 ya Nethania,+ wanawe na ndugu zake, 12; 13 ya 6 ya Bukia, wanawe na ndugu zake, 12; 14 ya 7 ya Yesharela,+ wanawe na ndugu zake, 12; 15 ya 8 ya Yeshaya, wanawe na ndugu zake, 12; 16 ya 9 ya Matania, wanawe na ndugu zake, 12; 17 ya 10 ya Shimei, wanawe na ndugu zake, 12; 18 ya 11 ya Azareli,+ wanawe na ndugu zake, 12; 19 ya 12 ya Hashabia, wanawe na ndugu zake, 12; 20 ya 13, ya Shubaeli,+ wanawe na ndugu zake, 12; 21 ya 14, ya Matithia, wanawe na ndugu zake, 12; 22 ya 15, ya Yeremothi, wanawe na ndugu zake, 12; 23 ya 16, ya Hanania, wanawe na ndugu zake, 12; 24 ya 17, ya Yoshbekasha, wanawe na ndugu zake, 12; 25 ya 18, ya Hanani, wanawe na ndugu zake, 12; 26 ya 19, ya Malothi, wanawe na ndugu zake, 12; 27 ya 20, ya Eliatha, wanawe na ndugu zake, 12; 28 ya 21, ya Hothiri, wanawe na ndugu zake, 12; 29 ya 22, ya Gidalti, wanawe na ndugu zake, 12; 30 ya 23, ya Mahaziothi,+ wanawe na ndugu zake, 12; 31 ya 24, ya Romamti-ezeri,+ wanawe na ndugu zake, 12.