Wimbo wa Mipando. Wa Daudi.
124 “Kama Yehova hangekuwa upande wetu,”+
Sasa Israeli na aseme,+
 2 “Kama Yehova hangekuwa upande wetu+
Watu waliposimama dhidi yetu,+
 3 Ndipo wangetumeza hata tukiwa hai,+
Hasira yao ilipokuwa inawaka juu yetu.+
 4 Ndipo maji yangetufagilia mbali,+
Mto wenyewe ungepita juu ya nafsi yetu.+
 5 Ndipo yangepita juu ya nafsi yetu
Maji ya kimbelembele.+
 6 Na abarikiwe Yehova, ambaye hakututoa+
Tuwe mawindo kwa meno yao.+
 7 Nafsi yetu ni kama ndege ambaye ameponyoka+
Kutoka katika mtego wa watega-chambo.+
Mtego umevunjwa,+
Na sisi tumeponyoka.+
 8 Msaada wetu uko katika jina la Yehova,+
Mtengenezaji wa mbingu na dunia.”+