Wimbo wa Sulemani
6 “Mpenzi wako amekwenda wapi, ewe mwanamke mrembo zaidi kati ya wanawake?+ Mpenzi wako amegeukia upande gani, ili tumtafute pamoja nawe?”
2 “Mpenzi wangu ameshuka kwenda katika bustani yake,+ katika eneo dogo la bustani ya manukato,+ kuchunga+ katikati ya bustani, na kuchuma mayungiyungi. 3 Mimi ni wa mpenzi wangu, naye mpenzi wangu ni wangu.+ Anachunga+ katikati ya mayungiyungi.”
4 “Wewe ni mrembo, ewe msichana mwenzi wangu,+ kama Jiji la Kupendeza,+ unavutia kama Yerusalemu,+ unatisha kama vikosi+ vilivyokusanyika kuzunguka bendera.+ 5 Geuzia mbali macho yako+ kutoka mbele yangu, kwa kuwa yamenishtua mimi. Nywele zako ni kama kundi la mbuzi ambao wameruka chini kutoka Gileadi.+ 6 Meno yako ni kama kundi la kondoo-jike ambao wamepanda kutoka kuoshwa, wote wanazaa mapacha, na kati yao hakuna yeyote aliyepoteza watoto wake.+ 7 Kama kipande cha komamanga ndivyo yalivyo mashavu yako nyuma ya ushungi wako.+ 8 Huenda kuna malkia 60 na masuria 80 na wanawali wasio na hesabu.+ 9 Lakini kuna mmoja ambaye ni njiwa wangu,+ wangu asiye na lawama.+ Kuna mmoja ambaye ni wa mama yake. Yeye ndiye aliye safi wa yule aliyemzaa. Binti wamemwona, nao wakamtangaza kuwa mwenye furaha; malkia na masuria, nao wakaanza kumsifu,+ 10 ‘Mwanamke+ huyu ni nani, anayetazama chini kama mapambazuko,+ mrembo kama mwezi mpevu,+ mwenye kutakata kama jua linaloangaza,+ mwenye kutisha kama vikosi vilivyokusanyika kuzunguka bendera?’”+
11 “Nilikuwa nimeshuka kwenda katika bustani+ ya milozi, nione matumba katika bonde la mto,+ nione kama mzabibu ulikuwa umechipuka, kama mikomamanga ilikuwa imechanua.+ 12 Kabla sijajua, nafsi yangu mimi ilikuwa imenitia katika magari ya watu wangu wenye kujitoa kwa kupenda.”
13 “Rudi, rudi, ewe Mshulami! Rudi, rudi, ili tukutazame!”+
“Mnaona nini kwa Mshulami?”+
“Kitu kama dansi ya kambi mbili!”