Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 22:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Mtu anayetoa dhabihu kwa miungu yoyote isipokuwa kwa Yehova peke yake ataangamizwa.+

  • Kumbukumbu la Torati 7:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Sanamu za kuchongwa za miungu yao mtaziteketeza kwa moto.+ Usitamani fedha na dhahabu iliyo juu yake,+ wala usiichukue kwa ajili yako,+ usije ukanaswa nayo;+ kwa maana hizo ni chukizo+ kwa Yehova Mungu wako.

  • Kumbukumbu la Torati 7:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Nawe usilete chukizo katika nyumba yako nawe uwe kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa kama kitu hicho. Kinai kitu hicho na kukichukia kabisa,+ kwa sababu ni kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuangamizwa.+

  • Yoshua 6:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Na jiji hili litakuwa kitu cha kuharibiwa;+ jiji lenyewe pamoja na kila kitu kilicho ndani yake ni vya Yehova. Rahabu+ yule kahaba peke yake ndiye atakayeendelea kuishi, yeye na wote walio pamoja naye katika nyumba, kwa kuwa aliwaficha wajumbe tuliowatuma.+

  • Yoshua 7:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 Kisha wana wa Israeli wakafanya tendo la kukosa uaminifu kuhusiana na kitu kilichotengwa kwa ajili ya kuharibiwa kwa kuwa Akani+ mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, alichukua sehemu ya vitu vilivyotengwa kwa ajili ya kuharibiwa.+ Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya wana wa Israeli.+

  • 1 Samweli 15:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Sasa nenda, umpige Amaleki,+ umwangamize+ pamoja na vitu vyote alivyo navyo, usimhurumie, nawe uwaue,+ mwanamume na mwanamke, mtoto na mtoto anayenyonya,+ ng’ombe pamoja na kondoo, ngamia pamoja na punda.’”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki