22 Nanyi mtachukua tawi la hisopo+ na kulichovya katika damu iliyo ndani ya beseni na kuipaka sehemu ya juu ya mlango na juu ya ile miimo miwili ya mlango kwa kiasi fulani cha damu iliyo kwenye beseni; na yeyote kati yenu asitoke nje ya mlango wa nyumba yake mpaka asubuhi.
18 Ndipo mtu aliye safi+ atachukua hisopo+ na kuichovya ndani ya maji yale na kuyatapanya juu ya hema na vyombo vyote na nafsi zote zilizokuwa hapo na juu ya yule aliyegusa mfupa au mtu aliyeuawa au maiti au kaburi.
33 Naye alikuwa akisema kuhusu miti, kuanzia mwerezi ulio katika Lebanoni+ mpaka mhisopo+ unaomea juu ya ukuta; na alikuwa akisema kuhusu wanyama+ na kuhusu viumbe vinavyoruka+ na kuhusu vitu vyenye kutambaa+ na kuhusu samaki.+