9 Ndipo Musa akamwambia Yoshua:+ “Tuchagulie wanaume, nawe uende+ ukapigane na Waamaleki. Kesho nitasimama juu ya kilima, nikiwa na fimbo ya Mungu wa kweli mkononi mwangu.”+
11 Naye Yehova akasema na Musa uso kwa uso,+ kama vile mwanadamu anavyosema na mwenzake. Aliporudi kambini, mhudumu wake+ Yoshua, mwana wa Nuni,+ akiwa mtumishi, hakuwa akiondoka katikati ya hema.
3 Yehova Mungu wako ndiye anayevuka mbele yako.+ Yeye mwenyewe atayaangamiza mataifa haya kutoka mbele yako, na wewe lazima uyafukuzie mbali.+ Yoshua ndiye anayevuka mbele yako,+ kama alivyosema Yehova.