14 Ndipo wanaume hao wakamwambia: “Nafsi zetu na zife badala yenu!+ Ikiwa hamtasema juu ya hii shughuli yetu, itatukia kwamba wakati Yehova atakapotupa nchi hii, sisi pia tutakutendea kwa fadhili zenye upendo na kwa uaminifu.”+
17 Na jiji hili litakuwa kitu cha kuharibiwa;+ jiji lenyewe pamoja na kila kitu kilicho ndani yake ni vya Yehova. Rahabu+ yule kahaba peke yake ndiye atakayeendelea kuishi, yeye na wote walio pamoja naye katika nyumba, kwa kuwa aliwaficha wajumbe tuliowatuma.+
22 Na Yoshua akawaambia wale wanaume wawili waliokuwa wameipeleleza nchi: “Ingieni katika nyumba ya yule mwanamke, yule kahaba, mkamtoe nje mwanamke huyo na wote walio wake, kama vile mlivyomwapia.”+