20 Na Yehova akaendelea kumwambia Haruni: “Katika nchi yao hutakuwa na urithi, wala hakuna fungu lolote litakalokuwa lako katikati yao.+ Mimi ni fungu lako na urithi wako katikati ya wana wa Israeli.+
12 Nanyi mtashangilia mbele za Yehova Mungu wenu,+ ninyi na wana wenu na binti zenu na watumishi wenu na vijakazi wenu na Mlawi aliye ndani ya malango yenu, kwa sababu hana fungu wala urithi pamoja nanyi.+
3 Kwa maana Musa alikuwa ametoa urithi wa yale makabila mawili na wa ile nusu ya kabila ng’ambo ile nyingine ya Yordani;+ naye hakuwapa Walawi urithi katikati yao.+