20 Lakini kama sivyo, moto+ na utoke ndani ya Abimeleki, uwateketeze wenye mashamba wa Shekemu na nyumba ya Milo,+ kisha moto+ na utoke ndani ya wenye mashamba wa Shekemu na nyumba ya Milo, nao umteketeze Abimeleki.”+
49 Basi watu wote wakajikatia tawi kila mmoja wao, wakamfuata Abimeleki. Ndipo wakayaweka juu ya ngome ile, nao wakaitia moto ngome hiyo juu yao, hivi kwamba watu wote wa mnara wa Shekemu wakafa pia, karibu watu elfu moja, wanaume na wanawake.+
11 Nami hakika nitaleta ubaya wake juu ya nchi yenye kuzaa,+ na kosa lao wenyewe juu ya waovu. Nami kwa kweli nitakifanya kiburi cha wenye kimbelembele kikome, na majivuno ya waonevu nitayashusha.+