4 Kisha Daudi akatuma wajumbe ili yeye amchukue.+ Basi mwanamke huyo akaja, akaingia kwake,+ akalala naye,+ wakati alipokuwa akijitakasa kutoka katika uchafu wake.+ Baadaye mwanamke huyo akarudi nyumbani kwake.
8 Mwishowe Daudi akamwambia Uria: “Shuka, nenda nyumbani kwako, uoshe miguu yako.”+ Basi Uria akatoka katika nyumba ya mfalme, na zawadi ya fadhili ya mfalme ikaletwa nyuma yake.
13 Zaidi ya hayo, Daudi akamwita ili ale chakula na kunywa mbele yake. Basi akamfanya alewe.+ Hata hivyo, akatoka nje jioni na kulala kitandani mwake pamoja na watumishi wa bwana wake, wala hakushuka kwenda nyumbani kwake.