15 “Naye Haruni na wanawe watamaliza kufunika mahali patakatifu+ na vyombo+ vyote vya mahali patakatifu wakati kambi inapoondoka, kisha wana wa Kohathi watakuja ili kuvichukua,+ lakini hawapaswi kugusa+ mahali patakatifu wasije wakafa. Vitu hivyo ni mzigo wa wana wa Kohathi katika hema la mkutano.+
4 Basi watu wakatuma ujumbe huko Shilo na kuchukua kutoka huko sanduku la agano la Yehova wa majeshi, anayeketi juu ya makerubi.+ Na wale wana wawili wa Eli walikuwa hapo pamoja na sanduku la agano la Mungu wa kweli, yaani, Hofni na Finehasi.+
2 Ndipo Daudi aliposema: “Mtu yeyote asilibebe sanduku la Mungu wa kweli isipokuwa Walawi, kwa maana Yehova amewachagua hao ili walibebe sanduku la Yehova+ na kumhudumia+ mpaka wakati usio na kipimo.”