Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Yoshua 10:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Na ikawa kwamba mara tu Adoni-sedeki mfalme wa Yerusalemu aliposikia kwamba Yoshua ameteka Ai+ na kuliharibu,+ kwamba jinsi alivyofanya Yeriko+ na mfalme wake,+ ndivyo alivyofanya Ai na mfalme wake,+ na kwamba wakaaji wa Gibeoni walikuwa wamefanya amani na Israeli+ na kuendelea kukaa katikati yao,

  • Yoshua 10:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Ndipo Yoshua akaanza kusema na Yehova siku ile ambayo Yehova aliwatia Waamori mikononi mwa wana wa Israeli, naye akasema machoni pa Israeli:

      “Ewe jua,+ simama tuli juu ya Gibeoni,+

      Nawe mwezi, juu ya nchi tambarare ya chini ya Aiyaloni.”+

  • Yoshua 18:25
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 25 Gibeoni+ na Rama na Beerothi,

  • Yoshua 21:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Na kutoka katika kabila la Benyamini, Gibeoni+ na kiwanja chake cha malisho, Geba+ na kiwanja chake cha malisho,

  • 2 Samweli 20:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Walikuwa karibu na lile jiwe kubwa lililo katika Gibeoni,+ naye Amasa+ akaja kuwapokea. Sasa Yoabu alikuwa amejifunga, amevaa vazi; naye alikuwa amefunga upanga kiunoni mwake, ukiwa katika ala yake. Naye akaenda mbele, nao ukaanguka.

  • 1 Wafalme 3:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Yehova akamtokea Sulemani katika ndoto+ usiku kule Gibeoni;+ na Mungu akasema: “Omba kile ninachopaswa kukupa.”+

  • 1 Mambo ya Nyakati 14:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Basi Daudi akafanya kama vile Mungu wa kweli alivyokuwa amemwamuru,+ nao wakaipiga kambi ya Wafilisti kutoka Gibeoni+ mpaka Gezeri.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 1:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Kisha Sulemani na kutaniko lote pamoja naye wakaenda mahali pa juu palipokuwa katika Gibeoni;+ kwa maana hapo ndipo lilipokuwa lile hema la mkutano+ la Mungu wa kweli, ambalo Musa mtumishi+ wa Yehova alitengeneza nyikani.

  • Isaya 28:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Kwa maana Yehova atasimama kama katika Mlima Perasimu,+ atafadhaika kama katika nchi tambarare ya chini karibu na Gibeoni,+ ili afanye tendo lake​—​tendo lake ni la ajabu​—​na ili afanye kazi yake​—​kazi yake si ya kawaida.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki