Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 15:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Na Asa akafanya yaliyokuwa sawa machoni pa Yehova, kama Daudi babu yake.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 14:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Na Asa akafanya yaliyokuwa mema na sawa machoni pa Yehova Mungu wake.

  • 2 Mambo ya Nyakati 14:11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 11 Naye Asa akaanza kumwita Yehova Mungu+ wake, na kusema: “Ee Yehova, kwa habari ya kusaidia, si kitu kwako kama kuna wengi au wale wasio na nguvu.+ Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana sisi tunakuegemea wewe,+ nasi kwa jina lako+ tumekuja kupigana na umati huu. Ee Yehova, wewe ni Mungu wetu.+ Usiache mwanadamu anayeweza kufa apate nguvu juu yako.”+

  • 2 Mambo ya Nyakati 15:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Na mara tu Asa alipoyasikia maneno hayo na unabii wa Odedi+ nabii, akajipa moyo, akaondoa kabisa machukizo+ katika nchi yote ya Yuda na Benyamini na katika majiji aliyokuwa ameteka kutoka katika eneo lenye milima la Efraimu,+ na kuifanya upya madhabahu ya Yehova iliyokuwa mbele ya ukumbi wa Yehova.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 17:3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 Na Yehova akaendelea kuwa pamoja na Yehoshafati,+ kwa sababu alitembea katika njia za zamani za Daudi babu yake+ wala hakutafuta Mabaali.+

  • Mhubiri 12:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Huu ndio mwisho wa mambo, kila jambo limekwisha sikiwa: Mwogope Mungu wa kweli+ na kushika amri zake.+ Kwa maana huo ndio wajibu wote wa mwanadamu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki