16 Ndipo utakapolazimika kuwachukua baadhi ya binti zao kwa ajili ya wana wako,+ na binti zao hakika watafanya uasherati na miungu yao na kuwafanya wana wako wafanye uasherati na miungu yao.+
12 “Lakini mkirudi nyuma kwa vyovyote+ na kushikamana na mabaki ya mataifa haya,+ yaani, haya yanayobaki na ninyi, na kufanya nao mapatano ya ndoa+ na kuingia katikati yao, nao wakiingia katikati yenu,
12 Na sasa ninyi msiwape wana wao binti zenu,+ wala binti zao msiwakubali kwa ajili ya wana wenu; nanyi msiwatakie amani wala mafanikio+ mpaka wakati usio na kipimo, ili mpate nguvu+ na mle mema ya nchi na kuimiliki kwa ajili ya wana wenu mpaka wakati usio na kipimo.’+
2 Ndipo Shekania mwana wa Yehieli+ wa wana wa Elamu+ akamwambia Ezra: “Sisi—sisi tumemtendea Mungu wetu kwa njia isiyo ya uaminifu, kwa kuwapa makao wake wa kigeni kutoka kwa vikundi vya watu wa nchi hii.+ Na bado sasa kuna tumaini+ kwa Israeli kuhusu jambo hili.
14 Msifungwe nira isivyo sawa pamoja na wasio waamini.+ Kwa maana kuna ushirika gani kati ya uadilifu na uasi-sheria?+ Au nuru ina ushirika gani na giza?+