-
2 Mambo ya Nyakati 31:1Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
31 Na mara tu walipomaliza hayo yote, Waisraeli+ wote waliokuwa hapo wakaenda katika majiji ya Yuda,+ nao wakazivunja nguzo takatifu+ na kuikata miti mitakatifu+ na kupabomoa mahali pa juu+ na madhabahu+ kutoka katika Yuda+ yote na Benyamini na katika Efraimu+ na Manase+ mpaka walipomaliza; kisha wana wote wa Israeli wakarudi katika majiji yao, kila mmoja kwenye miliki yake.
-