17 Na hakika mimi nitauweka uso wangu juu yenu, nanyi hakika mtashindwa mbele ya adui zenu;+ nao wale wanaowachukia ninyi watawakanyagia chini,+ nanyi kwa kweli mtakimbia wakati ambapo hakuna mtu yeyote anayewafuatilia.+
17 ambaye atatoka nje mbele yao na ambaye ataingia ndani mbele yao na ambaye atawatoa nje na ambaye atawaingiza ndani,+ ili kusanyiko la Yehova lisiwe kama kondoo wasio na mchungaji.”+
25 Yehova atakufanya ushindwe mbele ya adui zako.+ Utatoka nje kwa njia moja kwenda juu yao, lakini kwa njia saba utakimbia kutoka mbele yao; nawe utakuwa kitu chenye kuogopesha kwa falme zote za dunia.+
2 Kwa maana terafimu+ zimesema mambo ya uchawi; nao waaguzi wameona maono ya uwongo,+ nao huendelea kusema ndoto za bure, nao hujaribu kufariji kwa ubatili.+ Ndiyo sababu wataondoka kama kundi;+ watateseka, kwa sababu hakuna mchungaji.+