25 Yehova atakufanya ushindwe mbele ya adui zako.+ Utatoka nje kwa njia moja kwenda juu yao, lakini kwa njia saba utakimbia kutoka mbele yao; nawe utakuwa kitu chenye kuogopesha kwa falme zote za dunia.+
14 Ndipo hasira ya Yehova ikawaka juu ya Israeli,+ akawatia mikononi mwa waporaji, nao wakaanza kuwapora;+ naye akawauza mkononi mwa adui zao waliowazunguka pande zote,+ wala hawakuweza tena kusimama mbele ya adui zao.+
10 Basi Wafilisti wakapigana, na Israeli wakashindwa,+ nao wakakimbia kila mmoja kwenda katika hema lake;+ na mauaji hayo yakawa makubwa sana,+ hivi kwamba katika Israeli wakaanguka watu 30,000 wenye kwenda kwa miguu.+