17 Na hakika mimi nitauweka uso wangu juu yenu, nanyi hakika mtashindwa mbele ya adui zenu;+ nao wale wanaowachukia ninyi watawakanyagia chini,+ nanyi kwa kweli mtakimbia wakati ambapo hakuna mtu yeyote anayewafuatilia.+
25 Yehova atakufanya ushindwe mbele ya adui zako.+ Utatoka nje kwa njia moja kwenda juu yao, lakini kwa njia saba utakimbia kutoka mbele yao; nawe utakuwa kitu chenye kuogopesha kwa falme zote za dunia.+
2 Na Wafilisti wakajipanga+ ili kukutana na Israeli, na pigano hilo likaenda vibaya, hivi kwamba Israeli wakashindwa mbele ya Wafilisti,+ ambao waliwapiga na kuwaua karibu watu elfu nne katika pigano uwanjani.