21Neno+ lililomjia Yeremia kutoka kwa Yehova, wakati Mfalme Sedekia+ alipotuma kwake Pashuri+ mwana wa Malkiya na Sefania+ mwana wa Maaseya, kuhani, na kusema:
2 “Tafadhali muulize Yehova+ kwa ajili yetu, kwa sababu Nebukadreza mfalme wa Babiloni anapiga vita juu yetu.+ Labda Yehova atatutendea kulingana na kazi zake zote za ajabu, hivi kwamba yeye aondoke kwetu.”+