26 Ee binti ya watu wangu, vaa nguo ya gunia+ na ugaegae katika majivu.+ Omboleza kama kumwombolezea mwana wa pekee, kilio cha uchungu;+ kwa sababu mporaji atakuja juu yetu kwa ghafula.+
30 Nao hakika watajiacha wasikiwe juu yako kwa sauti yao nao watapaaza kilio kwa uchungu.+ Nao watatia mavumbi juu ya vichwa vyao.+ Watagaagaa katika majivu.+
6 Neno hilo lilipomfikia mfalme wa Ninawi,+ ndipo akasimama kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, akavua vazi lake rasmi na kujifunika nguo za magunia na kuketi katika majivu.+
8 Nao wajifunike nguo za magunia, mwanadamu na mnyama wa kufugwa; na wamwite Mungu kwa nguvu na warudi,+ kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya na kutoka katika jeuri iliyokuwa mikononi mwao.