Yona
3 Ndipo neno la Yehova likamjia Yona mara ya pili, na kusema:+ 2 “Ondoka, uende Ninawi lile jiji kubwa, ukalitangazie neno+ ninalokuambia.”
3 Basi Yona akasimama na kwenda Ninawi kulingana na neno la Yehova.+ Sasa Ninawi lilikuwa jiji kubwa kwa Mungu,+ lenye mwendo wa kutembea wa siku tatu. 4 Mwishowe Yona akaanza kuingia jijini mwendo wa kutembea wa siku moja, naye aliendelea kutangaza na kusema: “Bado siku 40 tu, na Ninawi litaangamizwa.”+
5 Nao watu wa Ninawi wakaanza kumwamini Mungu,+ ndipo wakatangaza kufunga na kuvaa nguo za magunia,+ kutoka aliye mkubwa zaidi kati yao mpaka aliye mdogo zaidi. 6 Neno hilo lilipomfikia mfalme wa Ninawi,+ ndipo akasimama kutoka kwenye kiti chake cha ufalme, akavua vazi lake rasmi na kujifunika nguo za magunia na kuketi katika majivu.+ 7 Zaidi ya hayo, akaagiza mwito utolewe, naye akaagiza utolewe katika Ninawi, kwa agizo la kisheria la mfalme na wakubwa wake, na kusema:
“Hakuna mwanadamu wala mnyama wa kufugwa, mifugo wala kundi, anayepaswa kuonja kitu chochote. Yeyote asile chakula. Hata maji wasinywe.+ 8 Nao wajifunike nguo za magunia, mwanadamu na mnyama wa kufugwa; na wamwite Mungu kwa nguvu na warudi,+ kila mmoja kutoka katika njia yake mbaya na kutoka katika jeuri iliyokuwa mikononi mwao. 9 Ni nani anayejua iwapo Mungu wa kweli hatageuka na kujuta+ na kuacha hasira yake inayowaka, tusije tukaangamia?”+
10 Naye Mungu wa kweli akaona matendo yao,+ kwamba walikuwa wamegeuka kutoka katika njia yao mbaya;+ naye Mungu wa kweli akajuta+ juu ya msiba ambao alikuwa amesema ataleta juu yao; naye hakuuleta.+