Yona
2 Ndipo, kutoka ndani ya tumbo la samaki huyo, Yona akasali kwa Yehova Mungu wake+ 2 na kusema:
“Katika taabu yangu nilimwita Yehova,+ naye akanijibu.+
Katika tumbo la Kaburi* nilililia msaada.+
Ulisikia sauti yangu.+
3 Uliponitupa kwenye vilindi, ndani ya moyo wa bahari kuu,+
Ndipo mto nao ukanizunguka.
Mashuu yako yote na mawimbi yako—yalipita juu yangu.+
4 Nami nikasema, ‘Nimefukuzwa kutoka mbele za macho yako!+
Nitapataje kuliona tena hekalu lako takatifu?’+
5 Maji yalinizunguka mpaka katika nafsi;+ kilindi cha maji nacho kikazidi kunizunguka.
Magugu yalinizunguka kichwani.
6 Nilishuka mpaka sehemu za chini kabisa za milima.
Nayo dunia, mapingo yake yalikuwa juu yangu mpaka wakati usio na kipimo.
Lakini uliinua uhai wangu toka shimoni, Ee Yehova Mungu wangu.+
7 Nafsi yangu ilipozimia ndani yangu,+ Yehova Ndiye niliyemkumbuka.+
Ndipo sala yangu ikaingia kwako, ndani ya hekalu lako takatifu.+
8 Nao wale wanaozifuata sanamu zisizo za kweli, wanaziacha fadhili zao wenyewe zenye upendo.+
9 Lakini mimi, kwa sauti ya kutoa shukrani nitakutolea dhabihu.+
10 Baadaye Yehova akamwamuru huyo samaki, akamtapika Yona kwenye nchi kavu.+