Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Nehemia 9:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Kwa hiyo wakakataa kusikiliza,+ wala hawakuyakumbuka+ matendo yako ya ajabu ambayo ulikuwa umewafanyia, bali wakafanya shingo zao kuwa ngumu+ na kujichagulia mkuu+ ili kurudi kwenye hali yao ya utumwa katika Misri. Lakini wewe ni Mungu wa matendo ya kusamehe,+ mwenye neema+ na rehema,+ si mwepesi wa hasira+ na ni mwingi+ wa fadhili zenye upendo, nawe hukuwaacha.+

  • Mika 7:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Atatuonyesha rehema tena;+ atayatiisha makosa yetu.+ Nawe utazitupa dhambi zao zote+ katika vilindi vya bahari.

  • Luka 6:36
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 36 Endeleeni kuwa wenye rehema, kama vile Baba yenu alivyo mwenye rehema.+

  • Waefeso 4:32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Bali iweni wenye fadhili+ ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo,+ mkisameheana kwa hiari kama vile Mungu pia kupitia Kristo alivyowasamehe ninyi kwa hiari.+

  • Wakolosai 3:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari+ ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika+ juu ya mwingine. Kama vile Yehova alivyowasamehe ninyi+ kwa hiari, nanyi fanyeni vivyo hivyo pia.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki