Wakolosai
3 Hata hivyo, ikiwa mlifufuliwa+ pamoja na Kristo, endeleeni kutafuta mambo yaliyo juu,+ ambako Kristo ameketi kwenye mkono wa kuume wa Mungu.+ 2 Endeleeni kukaza akili zenu juu ya mambo yaliyo juu,+ si juu ya mambo yaliyo duniani.+ 3 Kwa maana mlikufa,+ na uhai wenu+ umefichwa pamoja na Kristo katika muungano+ na Mungu. 4 Wakati Kristo, aliye uhai wetu,+ atakapofunuliwa, ndipo ninyi pia mtakapofunuliwa+ pamoja naye katika utukufu.+
5 Kwa hiyo, viueni+ viungo vya mwili+ wenu vilivyo duniani kwa habari ya uasherati, uchafu, hamu ya ngono,+ tamaa yenye madhara, na kutamani,+ ambako ni ibada ya sanamu. 6 Kwa sababu ya mambo hayo ghadhabu ya Mungu inakuja.+ 7 Ninyi, pia, mlitembea wakati mmoja katika mambo hayo, mlipokuwa mkiishi katika hayo.+ 8 Lakini sasa, kwa kweli, yaondoleeni mbali mambo haya yote kutoka kwenu,+ ghadhabu, hasira, ubaya, matukano,+ na maneno machafu+ kutoka kinywani mwenu. 9 Msiwe mkiambiana uwongo.+ Uvueni utu wa zamani+ pamoja na mazoea yake, 10 na mjivike utu mpya,+ ambao kupitia ujuzi sahihi unafanywa kuwa mpya kulingana na mfano+ wa Yule aliyeuumba, 11 ambapo hakuna Mgiriki wala Myahudi, tohara wala kutotahiriwa, mgeni, Msikithe, mtumwa, mtu huru,+ bali Kristo ni kila kitu na katika vitu vyote.+
12 Basi, kama waliochaguliwa wa Mungu,+ watakatifu na wapendwa, jivikeni upendo mwororo wenye huruma,+ fadhili, unyenyekevu wa akili,+ upole,+ na ustahimilivu.+ 13 Endeleeni kuvumiliana na kusameheana kwa hiari+ ikiwa yeyote ana sababu ya kulalamika+ juu ya mwingine. Kama vile Yehova alivyowasamehe ninyi+ kwa hiari, nanyi fanyeni vivyo hivyo pia. 14 Lakini, zaidi ya mambo haya yote, jivikeni upendo,+ kwa maana huo ni kifungo kikamilifu+ cha muungano.
15 Pia, acheni amani+ ya Kristo itawale mioyoni mwenu,+ kwa maana ninyi, kwa kweli, mliitiwa hiyo katika mwili mmoja.+ Na mjionyeshe kuwa wenye shukrani. 16 Neno la Kristo na likae ndani yenu kwa wingi katika hekima yote.+ Endeleeni kufundishana+ na kuonyana kwa zaburi,+ sifa kwa Mungu, nyimbo za kiroho+ kwa neema, mkimwimbia Yehova+ mioyoni mwenu. 17 Na lolote lile mnalofanya kwa neno au kwa tendo,+ fanyeni kila jambo katika jina la Bwana Yesu,+ mkimshukuru+ Mungu Baba kupitia yeye.
18 Enyi wake, jitiisheni+ kwa waume zenu, kwa kuwa inafaa katika Bwana. 19 Enyi waume, endeleeni kuwapenda wake zenu+ nanyi msiwakasirikie kwa uchungu.+ 20 Enyi watoto, watiini+ wazazi wenu katika kila jambo, kwa maana hilo linapendeza vema katika Bwana. 21 Enyi akina baba, msiwe mkiwakasirisha watoto wenu,+ ili wasivunjike moyo. 22 Enyi watumwa, watiini katika kila jambo wale ambao ni mabwana zenu katika maana ya kimwili,+ si kwa matendo ya utumishi wa macho, kama wenye kupendeza wanadamu,+ bali kwa unyoofu wa moyo, kwa kumwogopa Yehova.+ 23 Lolote mnalofanya, lifanyeni kwa nafsi yote+ kama kwa Yehova,+ na si kama kwa wanadamu, 24 kwa maana mnajua kwamba mtapokea kutoka kwa Yehova+ thawabu inayofaa ya urithi.+ Mtumikieni Bwana, Kristo.+ 25 Hakika yule anayetenda kosa atapokea malipo+ kwa lile kosa alilotenda, na hakuna ubaguzi wowote.+