5 Kisha akainua macho yake akaona wale wanawake na wale watoto na kusema: “Hawa walio pamoja nawe ni nani?” naye akasema: “Watoto ambao Mungu amemkubalia mtumishi wako kuwa nao.”+
4 Naye akaniambia, ‘Tazama, nakufanya uzae,+ nami nitakufanya kuwa wengi na nitakufanya uwe kutaniko la vikundi vya watu,+ nami nitaupa uzao wako baada yako nchi hii iwe miliki mpaka wakati usio na kipimo.’+
21 Basi Yehova akageuza fikira zake kwa Hana,+ akachukua mimba, akazaa wana watatu na binti wawili.+ Na yule mvulana Samweli akaendelea kukua akiwa na Yehova.+
5 na kati ya wanangu wote (kwa maana wana ambao Yehova amenipa ni wengi)+ ndipo akamchagua Sulemani+ mwanangu aketi kwenye kiti cha ufalme+ wa Yehova juu ya Israeli.