Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 1 Wafalme 18:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Basi wakamchukua yule ng’ombe mchanga aliyewapa. Kisha wakamtayarisha, nao wakaendelea kuliitia jina la Baali kutoka asubuhi mpaka katikati ya mchana, wakisema: “Ee Baali, tupe jibu!” Lakini hapakuwa na sauti yoyote,+ wala hakuna yeyote aliyetoa jibu.+ Nao wakazidi kurukaruka kuizunguka madhabahu waliyokuwa wameitengeneza.

  • Isaya 37:38
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Na ikawa kwamba alipokuwa akiinama nyumbani mwa Nisroki+ mungu wake,+ Adrameleki na Shareza, wanawe mwenyewe, wakampiga na kumuua kwa upanga,+ nao wakakimbia, wakaenda katika nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.

  • Yeremia 2:28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 “Lakini iko wapi miungu yako ambayo umejifanyia?+ Na isimame ikiwa inaweza kukuokoa wakati wa msiba wako.+ Kwa maana miungu yako imekuwa kama hesabu ya majiji yako, Ee Yuda.+

  • Yona 1:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Nao wanamaji wakaanza kuogopa na kuomba msaada, kila mmoja kwa mungu wake.+ Nao wakawa wakitupa baharini vyombo vilivyokuwa ndani ya meli, ili kuipunguzia uzito wake.+ Lakini Yona alikuwa ameshuka na kuingia sehemu za ndani kabisa za chombo hicho chenye ghorofa, naye akajilaza chini, akalala usingizi mzito.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki