Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 115:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Zina kinywa, lakini haziwezi kusema;+

      Zina macho, lakini haziwezi kuona;+

  • Zaburi 135:16
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 16 Zina kinywa, lakini haziwezi kusema lolote;+

      Zina macho, lakini haziwezi kuona chochote;+

  • Isaya 44:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Hawajajua,+ wala hawaelewi,+ kwa sababu macho yao yamechafuliwa ili yasione,+ moyo wao ili usiwe na ufahamu.+

  • Isaya 45:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Jikusanyeni na kuja.+ Njooni karibu pamoja, ninyi wenye kuponyoka kutoka katika mataifa.+ Wale wanaochukua miti ya sanamu yao ya kuchongwa hawajapata ujuzi wowote, wala wale wanaotoa sala kwa mungu ambaye hawezi kuokoa.+

  • Yeremia 10:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Hizo ni kama sanamu ya kufukuza ndege ya shamba la matango, nazo haziwezi kusema.+ Nazo hakika hubebwa, kwa maana haziwezi kupiga hatua zozote.+ Zisiwatie woga, kwa maana haziwezi kufanya jambo lolote lenye kuleta msiba, na zaidi ya hayo, haziwezi kufanya wema wowote.”+

  • Danieli 5:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 Bali ulijiinua juu ya Bwana wa mbingu,+ nao wakaleta mbele yako vyombo vya nyumba yake;+ na wewe pamoja na wakuu wako, masuria wako na wake zako wadogo mmekuwa mkivinywea divai. Nawe umeisifu miungu minyonge ya fedha na ya dhahabu, shaba, chuma, miti na mawe,+ ambayo haioni chochote, wala kusikia chochote, wala kujua chochote;+ lakini hukumtukuza+ Mungu ambaye pumzi yako imo mkononi mwake+ na ambaye njia zako zote ni zake.+

  • Habakuki 2:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Sanamu ya kuchongwa imekuwa na faida gani,+ wakati yeye aliyeifanya ameichonga, sanamu ya kuyeyushwa, na mfundishaji wa uwongo?+ wakati yeye aliyefanya umbo lake ameitegemea,+ kufikia hatua ya kufanya miungu isiyo na thamani ambayo haiwezi kusema?+

  • 1 Wakorintho 8:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 4 Sasa kuhusu kula+ vyakula vinavyotolewa kwa sanamu, tunajua kwamba sanamu si kitu+ katika ulimwengu, na kwamba hakuna Mungu isipokuwa mmoja.+

  • 1 Wakorintho 10:19
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Basi, niseme nini? Kwamba kile ambacho kimetolewa dhabihu kwa sanamu ni kitu, au kwamba sanamu ni kitu?+

  • 1 Wakorintho 12:2
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 2 Mnajua kwamba mlipokuwa watu wa mataifa,+ mlikuwa mkiongozwa kwenye zile sanamu+ zisizo na sauti+ kama vile mlivyoongozwa.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki