1 Wakorintho
10 Basi sitaki mkose kujua, akina ndugu, kwamba mababu zetu walikuwa wote chini ya wingu+ na wote walipita katika bahari + 2 na wote walibatizwa katika Musa+ kupitia wingu na bahari; 3 na wote walikula chakula kilekile cha kiroho+ 4 na wote walikunywa maji+ yaleyale ya kiroho. Kwa maana walikuwa wakinywa kutokana na mwamba+ wa kiroho uliowafuata, na mwamba+ huo ulimaanisha Kristo.+ 5 Hata hivyo, Mungu hakuonyesha kibali+ chake juu ya walio wengi kati yao, kwa maana waliangamizwa+ nyikani.
6 Basi mambo hayo yalikuwa vielelezo kwetu sisi, ili tusiwe watu wanaotamani mambo mabaya,+ kama wao walivyoyatamani. 7 Wala tusiwe waabudu-sanamu, kama baadhi yao walivyofanya;+ kama ilivyoandikwa: “Watu wakaketi ili wale na kunywa, nao wakasimama wapate kujifurahisha.”+ 8 Wala tusifanye uasherati, kama baadhi yao walivyofanya uasherati,+ na kuanguka, 23,000 kati yao katika siku moja.+ 9 Wala tusimjaribu Yehova,+ kama baadhi yao walivyomjaribu,+ na kuangamizwa na nyoka.+ 10 Wala tusiwe wanung’unikaji, kama baadhi yao walivyonung’unika,+ na kuangamizwa na mwangamizaji.+ 11 Basi mambo hayo yaliendelea kuwapata kuwa vielelezo, nayo yaliandikwa ili kuwa onyo+ kwetu sisi ambao tumefikiwa na miisho ya mifumo ya mambo.+
12 Kwa hiyo yeye anayefikiri kuwa amesimama na ajihadhari kwamba asianguke.+ 13 Hakuna jaribu ambalo limewapata ninyi ila lile lililo kawaida kwa watu.+ Lakini Mungu ni mwaminifu,+ naye hatawaacha ninyi mjaribiwe kupita mnavyoweza kuhimili,+ bali pamoja na hilo jaribu ataifanya pia njia ya kutokea+ kusudi mweze kulivumilia.
14 Kwa hiyo, wapendwa wangu, ikimbieni+ ibada ya sanamu.+ 15 Nasema kana kwamba ni kwa watu wenye utambuzi;+ hukumuni ninyi wenyewe lile ninalosema. 16 Kikombe+ cha baraka ambacho tunabariki, je, hicho si kushiriki katika damu ya Kristo? Ule mkate ambao tunamega,+ je, huo si kushiriki katika mwili wa Kristo?+ 17 Kwa sababu kuna mkate mmoja, sisi, ingawa tuko wengi,+ ni mwili mmoja,+ kwa maana sisi sote tunakula huo mkate mmoja.+
18 Tazameni kile ambacho ni Israeli kwa njia ya kimwili:+ Je, wale wanaokula dhabihu si washiriki pamoja na madhabahu?+ 19 Basi, niseme nini? Kwamba kile ambacho kimetolewa dhabihu kwa sanamu ni kitu, au kwamba sanamu ni kitu?+ 20 Hapana; bali nasema kwamba vitu ambavyo mataifa huvitoa dhabihu wao huvitoa dhabihu kwa roho waovu,+ na si kwa Mungu; nami sitaki ninyi muwe washiriki pamoja na roho waovu.+ 21 Hamwezi kuwa mkinywa kikombe cha Yehova+ na kikombe cha roho waovu; hamwezi kuwa mkishiriki “meza ya Yehova”+ na meza ya roho waovu. 22 Au je, “tunamchochea Yehova kuwa na wivu”?+ Je, sisi tuna nguvu+ zaidi kuliko yeye?
23 Mambo yote ni halali; lakini si mambo yote yaliyo na faida.+ Mambo yote ni halali;+ lakini si mambo yote yanayojenga.+ 24 Kila mmoja na aendelee kutafuta, si faida yake mwenyewe,+ bali ile ya yule mtu mwingine.+
25 Endeleeni kula kila kitu kinachouzwa katika soko la nyama,+ bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu;+ 26 kwa maana “dunia na vyote vinavyoijaza+ ni vya Yehova.”+ 27 Yeyote kati ya wasio waamini akiwaalika nanyi mtake kwenda, kuleni kila kitu kinachowekwa mbele yenu,+ bila kuchunguza kwa sababu ya dhamiri yenu.+ 28 Lakini yeyote akiwaambia ninyi: “Hiki ni kitu kilichotolewa katika dhabihu,” msile kwa sababu ya yule aliyefunua hilo na kwa sababu ya dhamiri.+ 29 “Dhamiri,” nasema, si yako mwenyewe, bali ile ya yule mtu mwingine. Kwa maana kwa nini iwe kwamba uhuru wangu unahukumiwa na dhamiri ya mtu mwingine?+ 30 Ikiwa nakula nikiwa na shukrani, kwa nini nitukanwe juu ya kile ninachotolea shukrani?+
31 Kwa hiyo, kama mnakula au mnakunywa au mnafanya jambo lingine lolote, fanyeni mambo yote kwa utukufu wa Mungu.+ 32 Epukeni kuwa vikwazo+ kwa Wayahudi na vilevile kwa Wagiriki na kwa kutaniko la Mungu, 33 kama vile mimi ninavyowapendeza watu wote katika mambo yote,+ bila kutafuta faida yangu mwenyewe+ bali ile ya walio wengi, ili wapate kuokolewa.+