1 Wakorintho
11 Iweni waigaji wangu, kama vile mimi nilivyo mwigaji wa Kristo.+
2 Sasa nawasifu ninyi kwa sababu katika mambo yote mnanikumbuka na mnayashika sana mapokeo+ kama vile nilivyowapa ninyi. 3 Lakini nataka mjue kwamba kichwa cha kila mwanamume ni Kristo;+ nacho kichwa cha mwanamke ni mwanamume;+ nacho kichwa cha Kristo ni Mungu.+ 4 Kila mwanamume ambaye husali au kutoa unabii akiwa na kitu juu ya kichwa chake hukiaibisha kichwa chake;+ 5 lakini kila mwanamke ambaye husali au kutoa unabii+ kichwa chake kikiwa hakijafunikwa hukiaibisha kichwa chake,+ kwa maana ni kana kwamba yeye ni mwanamke mwenye kichwa kilichonyolewa.+ 6 Kwa maana ikiwa mwanamke hajifuniki, na akatwe nywele pia; lakini ikiwa inafedhehesha kwa mwanamke kukatwa nywele au kunyolewa,+ basi na afunikwe.+
7 Kwa maana mwanamume hapaswi kufunika kichwa chake, kwa kuwa yeye ni mfano+ na utukufu wa Mungu;+ lakini mwanamke ni utukufu wa mwanamume.+ 8 Kwa maana mwanamume hakutoka katika mwanamke, bali mwanamke alitoka katika mwanamume;+ 9 na, zaidi ya hayo, mwanamume hakuumbwa kwa ajili ya mwanamke, bali mwanamke kwa ajili ya mwanamume.+ 10 Ndiyo sababu mwanamke anapaswa kuwa na ishara ya mamlaka juu ya kichwa chake+ kwa sababu ya malaika.+
11 Tena, kuhusiana na Bwana mwanamke si bila mwanamume wala mwanamume si bila mwanamke.+ 12 Kwa maana kama vile mwanamke ametoka katika mwanamume,+ vivyo hivyo pia mwanamume amepitia katika mwanamke;+ lakini vitu vyote vimetoka kwa Mungu.+ 13 Hukumuni ninyi wenyewe: Je, inafaa mwanamke kusali kwa Mungu pasipo kichwa chake kufunikwa? 14 Je, maumbile yenyewe hayawafundishi ninyi kwamba mwanamume akiwa na nywele ndefu, ni aibu kwake; 15 lakini mwanamke akiwa na nywele ndefu, ni utukufu+ kwake? Kwa sababu yeye amepewa nywele zake ziwe badala ya vazi la kichwani.+ 16 Hata hivyo, mtu yeyote akiwa na mwelekeo wa kubishania+ desturi fulani nyingine,+ sisi hatuna nyingine, wala makutaniko ya Mungu.
17 Lakini, ninapoyatoa maagizo haya, siwasifu ninyi kwa sababu mnakutana pamoja, si kwa ajili ya wema, bali kwa ajili ya ubaya kabisa.+ 18 Kwa maana kwanza kabisa, mnapokuja pamoja katika kutaniko, nasikia kwamba kuna migawanyiko katikati yenu;+ nami naamini jambo hilo kwa kiasi fulani. 19 Kwa maana lazima pia yaweko madhehebu+ katikati yenu, ili watu waliokubaliwa wapate pia kufunuliwa katikati yenu.+
20 Kwa hiyo, mnapokuja pamoja mahali pamoja, haiwezekani kula mlo wa jioni wa Bwana.+ 21 Kwa maana, mnapoula, kila mtu hutangulia kula mlo wake mwenyewe wa jioni, hivi kwamba mmoja ana njaa lakini mwingine amelewa. 22 Je, hamna nyumba za kulia mlo na kunywea?+ Au je, mnalidharau kutaniko la Mungu na kuwaaibisha wale wasio na kitu?+ Nitawaambia ninyi nini? Je, nitawasifu ninyi? Katika hilo siwasifu ninyi.
23 Kwa maana nilipokea kutoka kwa Bwana kile nilichowapa ninyi pia, kwamba Bwana Yesu katika ule usiku+ aliokuwa akienda kutolewa alichukua mkate 24 na, baada ya kutoa shukrani, akaumega+ na kusema: “Huu unamaanisha mwili+ wangu ambao ni kwa ajili yenu. Endeleeni kufanya hivi kwa kunikumbuka+ mimi.” 25 Akafanya vivyo hivyo kuhusu kile kikombe+ pia, baada ya yeye kula mlo wa jioni, akisema: “Kikombe hiki kinamaanisha agano jipya+ kwa msingi wa damu+ yangu. Endeleeni kufanya hivi, kila mara mnapokinywa, kwa kunikumbuka+ mimi.” 26 Kwa maana kila mara+ mnapokula mkate huu na kunywa kikombe hiki, mnaendelea kukitangaza kifo+ cha Bwana, mpaka atakapofika.+
27 Kwa hiyo yeyote anayeula mkate au kukinywa kikombe cha Bwana isivyofaa atakuwa na hatia+ kuhusiana na mwili na damu+ ya Bwana. 28 Kwanza acheni mtu ajichunguze mwenyewe na kuona kama anafaa,+ na basi ale mkate na anywe kikombe. 29 Kwa maana yeye anayekula na kunywa anakula na kunywa hukumu+ juu yake mwenyewe ikiwa hautambui mwili. 30 Ndiyo sababu wengi katikati yenu ni dhaifu na wagonjwa-wagonjwa, na wengi wamelala+ katika kifo. 31 Lakini kama tungalitambua sisi wenyewe ni nani, hatungalihukumiwa.+ 32 Hata hivyo, tunapohukumiwa,+ Yehova+ anatutia nidhamu, ili tusihukumiwe+ pamoja na ulimwengu.+ 33 Kwa hiyo, ndugu zangu, mnapokuja pamoja kula mlo huo,+ mngojeane. 34 Ikiwa yeyote ana njaa, acheni ale nyumbani,+ ili msije pamoja kwa ajili ya kuhukumiwa.+ Lakini mambo yaliyobaki nitayarekebisha nitakapofika.