Isaya
37 Na ikawa kwamba mara tu Mfalme Hezekia aliposikia, mara moja akayararua mavazi yake, akavaa nguo za magunia,+ akaingia ndani ya nyumba ya Yehova.+ 2 Na zaidi ya hayo, akamtuma Eliakimu,+ aliyekuwa juu ya hiyo nyumba, na Shebna mwandishi+ na wanaume wazee wa makuhani+ wakiwa wamevaa nguo za magunia, waende kwa Isaya+ nabii, mwana wa Amozi.+ 3 Nao wakamwambia: “Hezekia amesema hivi, ‘Leo ni siku ya taabu+ na ya kemeo na ya dharau yenye dhihaka,+ kwa maana wana wamefika mpaka kwenye mlango wa tumbo la uzazi, na hakuna nguvu za kuzaa.+ 4 Pengine Yehova Mungu wako atayasikia maneno ya Rabshake,+ ambaye mfalme wa Ashuru bwana wake alimtuma ili kumdhihaki+ Mungu aliye hai, naye kwa kweli atamtoza hesabu kwa ajili ya maneno ambayo Yehova, Mungu wako, ameyasikia.+ Nawe uinue sala+ kwa ajili ya mabaki ambao wanapatikana.’”+
5 Basi watumishi wa Mfalme Hezekia wakaingia kwa Isaya.+ 6 Ndipo Isaya akawaambia: “Mwambieni bwana wenu, ‘Yehova amesema hivi:+ “Usiogope+ kwa sababu ya maneno uliyosikia ambayo watumishi+ wa mfalme wa Ashuru wamesema vibaya kunihusu. 7 Tazama, ninatia roho+ ndani yake, naye atasikia habari+ na kurudi katika nchi yake mwenyewe; nami hakika nitamwangusha kwa upanga katika nchi yake mwenyewe.”’”+
8 Baada ya hapo Rabshake+ akarudi na kumkuta mfalme wa Ashuru akipigana na Libna,+ kwa maana alikuwa amesikia kwamba ameondoka Lakishi.+ 9 Sasa alisikia ikisemwa hivi kumhusu Tirhaka+ mfalme wa Ethiopia: “Amekuja kupigana nawe.” Aliposikia hayo, akatuma wajumbe+ mara moja kwa Hezekia, na kusema: 10 “Mwambieni hivi Hezekia mfalme wa Yuda, ‘Usiache Mungu unayemtegemea akudanganye,+ na kusema: “Yerusalemu halitatiwa mkononi mwa mfalme wa Ashuru.”+ 11 Tazama! Wewe mwenyewe umesikia yale ambayo wafalme wa Ashuru walizitendea nchi zote kwa kuziangamiza,+ na je, wewe mwenyewe utakombolewa?+ 12 Je, miungu+ ya mataifa ambayo mababu zangu waliharibu imeyakomboa,+ naam, Gozani+ na Harani+ na Resefu na wana wa Edeni+ waliokuwa katika Tel-asari? 13 Yuko wapi mfalme wa Hamathi+ na mfalme wa Arpadi+ na mfalme wa jiji la Sefarvaimu+—wa Hena na wa Iva?’”+
14 Ndipo Hezekia akaichukua ile barua kutoka mkononi mwa wale wajumbe, akaisoma,+ kisha Hezekia akaenda katika nyumba ya Yehova, akaitandaza mbele za Yehova.+ 15 Na Hezekia akaanza kusali kwa Yehova,+ akisema: 16 “Ee Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli,+ unayeketi juu ya makerubi, wewe peke yako ndiye Mungu wa kweli wa falme zote za dunia.+ Wewe mwenyewe umezifanya mbingu na dunia.+ 17 Tega sikio lako, Ee Yehova, usikie.+ Fungua macho yako,+ Ee Yehova, uone, na uyasikie maneno yote ya Senakeribu+ ambayo ametuma ili kumdhihaki Mungu aliye hai.+ 18 Ee Yehova, ni kweli kwamba wafalme wa Ashuru wameziharibu nchi zote, na nchi yao wenyewe.+ 19 Na miungu yao iliteketezwa kwa moto,+ kwa sababu hiyo haikuwa miungu,+ bali kazi ya mikono ya mwanadamu,+ miti na mawe, hivi kwamba wakaiharibu.+ 20 Na sasa, Ee Yehova Mungu wetu,+ utuokoe kutoka mkononi mwake,+ ili falme zote za dunia zijue kwamba wewe, Ee Yehova, ndiye Mungu peke yako.”+
21 Naye Isaya mwana wa Amozi akatuma habari kwa Hezekia, na kusema: “Yehova, Mungu wa Israeli, amesema hivi, ‘Kwa sababu umesali kwangu kumhusu Senakeribu mfalme wa Ashuru,+ 22 Yehova amesema neno hili juu yake:
“Bikira, binti Sayuni, amekudharau, amekudhihaki.+
Binti Yerusalemu ametikisa kichwa chake nyuma yako.+
23 Umemdhihaki+ nani na kusema vibaya+ juu yake?
Nawe umepaaza sauti+ yako juu ya nani
Na kuinua macho+ yako juu?
Ni juu ya Mtakatifu wa Israeli!+
24 Umemdhihaki Yehova kupitia watumishi wako, nawe unasema,+
‘Kwa wingi wa magari yangu ya vita, mimi mwenyewe+—
Mimi hakika nitapanda vilele vya maeneo yenye milima,+
Sehemu za mbali zaidi za Lebanoni;+
Nami nitaikata mierezi yake iliyotukuka, miberoshi yake iliyo bora.+
Nami nitaingia katika kilele chake cha mwisho, msitu wa shamba lake la matunda.+
25 Mimi hakika nitachimba na kunywa maji,
Nami nitaikausha mifereji yote ya Nile+ ya Misri kwa nyayo za miguu yangu.’+
26 Je, hujasikia?+ Tangu nyakati za zamani za kale ndilo nitakalofanya.+
Tangu siku zilizopita nimelifanya.+ Sasa nitalitimiza.+
Nawe utafanya majiji yenye ngome yawe ukiwa kama marundo ya mabomoko.+
Watakuwa kama majani ya shambani na majani mabichi yaliyo laini,+
28 Nami najua vema kuketi kwako kimya na kuondoka+ kwako na kuingia kwako,+
Na kujichochea kwako juu yangu,+
29 Kwa sababu kujichochea kwako juu yangu+ na kunguruma kwako kumepanda mpaka ndani ya masikio yangu.+
Nami hakika nitatia kulabu yangu puani mwako na lijamu yangu katikati ya midomo yako,+
Nami hakika nitakurudisha kupitia njia ile uliyoijia.”+
30 “‘Na hii itakuwa ndiyo ishara kwa ajili yako: Mimea inayochipuka kutokana na mbegu zilizoanguka+ italiwa mwaka huu, na katika mwaka wa pili nafaka inayochipuka yenyewe; lakini katika mwaka wa tatu pandeni mbegu, mvune, na mpande mashamba ya mizabibu na kula mazao yake.+ 31 Na wale watakaoponyoka wa nyumba ya Yuda, wale wanaobaki,+ hakika watatia mizizi kwenda chini na kuzaa matunda kwenda juu.+ 32 Kwa maana mabaki+ watatoka katika Yerusalemu na wale wanaoponyoka katika Mlima Sayuni.+ Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.+
33 “‘Kwa hiyo Yehova amesema hivi kumhusu mfalme wa Ashuru:+ “Hataingia katika jiji hili+ wala hatapiga mshale humo, wala kulikabili kwa ngao, wala kujenga juu yake boma la kulizingira.”’+
34 “‘Atarudi kupitia ile njia aliyoijia, naye hataingia ndani ya jiji hili,’ asema Yehova.+ 35 ‘Nami hakika nitalilinda+ jiji hili ili kuliokoa kwa ajili yangu mwenyewe+ na kwa ajili ya Daudi mtumishi wangu.’”+
36 Na malaika+ wa Yehova alitoka, akapiga na kuwaua watu 185,000 katika kambi ya Waashuru.+ Watu walipoamka asubuhi na mapema, tazama, wote walikuwa mizoga iliyokufa.+ 37 Basi Senakeribu+ mfalme wa Ashuru akaondoka, akaenda, akarudi,+ akaanza kukaa katika Ninawi.+ 38 Na ikawa kwamba alipokuwa akiinama nyumbani mwa Nisroki+ mungu wake,+ Adrameleki na Shareza, wanawe mwenyewe, wakampiga na kumuua kwa upanga,+ nao wakakimbia, wakaenda katika nchi ya Ararati.+ Na Esar-hadoni+ mwana wake akaanza kutawala mahali pake.