Isaya
38 Katika siku hizo Hezekia akawa mgonjwa kufikia hatua ya kufa.+ Basi Isaya+ mwana wa Amozi nabii akaingia kwake na kumwambia: “Yehova amesema hivi, ‘Wape amri watu wa nyumba yako,+ kwa maana wewe hakika utakufa wala hutaishi.’”+ 2 Ndipo Hezekia akageuza uso wake kuelekea ukuta,+ akaanza kusali kwa Yehova+ 3 na kusema: “Nakuomba, Ee Yehova, tafadhali ukumbuke+ jinsi nilivyotembea+ mbele zako kwa ukweli+ na kwa moyo mkamilifu,+ nami nimetenda yaliyokuwa mema machoni pako.” Na Hezekia akaanza kulia sana.+
4 Sasa neno+ la Yehova likamjia Isaya, kusema: 5 “Nenda, umwambie Hezekia, ‘Yehova, Mungu wa Daudi babu yako+ amesema hivi: “Nimeisikia sala yako.+ Nimeyaona machozi yako.+ Tazama, naongeza miaka kumi na mitano juu ya siku zako;+ 6 nami nitakukomboa wewe pamoja na jiji hili kutoka katika mkono wa mfalme wa Ashuru, nami nitalilinda jiji hili.+ 7 Na hii ndiyo ishara kwa ajili yako kutoka kwa Yehova kwamba Yehova atatenda neno hili ambalo amesema:+ 8 Tazama, ninafanya kivuli cha vipandio ambacho kilikuwa kimeshuka juu ya vile vipandio vya ngazi ya Ahazi kwa sababu ya jua+ kirudi nyuma vipandio kumi.”’”+ Na jua likarudi nyuma polepole vipandio kumi juu ya vipandio vya ngazi ambavyo lilikuwa limeshuka.+
9 Haya ni maandishi ya Hezekia mfalme wa Yuda, aliposhikwa na ugonjwa+ kisha akapona ugonjwa wake.+
10 Mimi nilisema: “Katikati ya siku zangu nitaingia katika malango+ ya Kaburi.*
Nitanyimwa mabaki+ ya miaka yangu.”
11 Nimesema: “Sitamwona Yah, ndiyo, Yah, katika nchi ya walio hai.+
Sitawaona wanadamu tena—pamoja na wakaaji wa nchi ya kukoma.
12 Makao yangu yameng’olewa+ na kuondolewa kwangu kama hema la wachungaji.
Nimeukunja uhai wangu kama mfumaji wa nguo;
Mtu fulani ananikatilia mbali+ kutoka kwenye nyuzi za mtande.
Tangu mapambazuko mpaka usiku unaendelea kunitoa.+
Tangu mapambazuko mpaka usiku wewe unaendelea kunitoa.+
15 Nitasema nini, na kwa kweli yeye ataniambia nini?+
Yeye ametenda pia.+
Ninaendelea kutembea kwa unyamavu miaka yangu yote katika uchungu wa nafsi yangu.+
16 ‘Ee Yehova, kwa sababu hiyo wanaendelea kuishi; na kama ilivyo kwa kila mtu, ndivyo na uhai wa roho yangu.+
Nawe utanirudishia afya na hakika kunihifadhi hai.+
17 Tazama! Kwa ajili ya amani nilipata jambo chungu, ndiyo, chungu;+
Nawe mwenyewe umeshikamana na nafsi yangu na kuizuia kutokana na shimo la uharibifu.+
Kwa maana umezitupa dhambi zangu zote nyuma ya mgongo wako.+
18 Kwa maana Kaburi* haliwezi kukusifu;+ kifo hakiwezi kukusifu.+
Wale wanaoshuka shimoni hawawezi kuutumaini ukweli wako.+
19 Aliye hai, aliye hai, ndiye anayeweza kukusifu,+
Kama vile mimi ninavyoweza leo hii.+
Baba anaweza kuwapa wanawe ujuzi+ kuhusu ukweli wako.
20 Ee Yehova, chukua hatua ya kuniokoa,+ nasi tutapiga nyimbo zangu za kinanda nilizochagua+
Siku zote za maisha yetu katika nyumba ya Yehova.’”+
21 Naye Isaya akasema: “Acha wachukue keki ya tini kavu zilizoshinikizwa na mlipake lile jipu,+ ili apone.”+ 22 Wakati huo Hezekia akasema: “Kuna ishara gani kwamba nitapanda kwenda katika nyumba ya Yehova?”+