4 Na jiji likabomolewa,+ na watu wote wa vita wakakimbia wakati wa usiku kupitia njia ya lango lililo kati ya zile kuta mbili kando ya bustani ya mfalme,+ huku Wakaldayo+ wakiwa wamelizunguka jiji pande zote; naye mfalme akaanza kwenda+ kuelekea upande wa Araba.+
5 Nami nitavitoa vitu vyote vya jiji hili vilivyowekwa akiba na mazao yake yote na vitu vyake vyote vyenye thamani; na hazina zote za wafalme wa Yuda nitazitia mkononi mwa adui zao.+ Na hakika wao watavipora na kuvichukua na kuvipeleka Babiloni.+
4 ‘Yehova Mungu wa Israeli amesema hivi: “Tazama, ninazigeuza nyuma silaha za vita zilizo mkononi mwenu, mnazotumia kupigana na mfalme wa Babiloni,+ na Wakaldayo+ wanaowazingira ninyi nje ya ukuta, nami nitazikusanya katikati ya jiji hili.+