11 Siku hiyo hutaona aibu kwa sababu ya matendo yako yote uliyonikosea,+ kwa maana wakati huo nitaondoa katikati yako watu wako wanaofurahi kwa majivuno;+ nawe hutajivuna tena kamwe katika mlima wangu mtakatifu.+
14 Ninawaambia ninyi, Mtu huyu alishuka kwenda nyumbani kwake akiwa amethibitishwa kuwa mwadilifu+ zaidi kuliko yule mwingine; kwa sababu kila mtu anayejiinua atafedheheshwa, bali yule anayejinyenyekeza atainuliwa.”+
6 Hata hivyo, fadhili zisizostahiliwa ambazo yeye hutoa ni kubwa zaidi.+ Kwa hiyo, hilo linasema: “Mungu huwapinga wenye majivuno,+ lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.”+
5 Vivyo hivyo, enyi vijana, jitiisheni+ kwa wanaume wazee. Lakini ninyi nyote jifungeni unyenyekevu wa akili kuelekeana ninyi wenyewe,+ kwa sababu Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.+