Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 6:5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Basi Yehova akaona kuwa ubaya wa mwanadamu ulikuwa mwingi duniani na kila mwelekeo+ wa fikira za moyo wake ulikuwa mbaya tu wakati wote.+

  • Mwanzo 8:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Na Yehova akaanza kunusa harufu ya kutuliza,+ na kwa hiyo Yehova akasema moyoni mwake:+ “Sitailaani nchi+ tena kamwe kwa sababu ya mwanadamu, kwani mwelekeo+ wa moyo wa mwanadamu ni mbaya tangu ujana wake na kuendelea;+ nami sitakipiga tena kamwe kila kitu chenye uhai kama vile nilivyofanya.+

  • Methali 28:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Anayetegemea moyo wake mwenyewe ni mjinga,+ lakini yeye anayetembea katika hekima ndiye atakayeponyoka.+

  • Isaya 44:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Anajilisha majivu.+ Moyo wake ambao umedanganywa umempotosha.+ Naye haikomboi nafsi yake, wala hasemi: “Je, hamna uwongo katika mkono wangu wa kuume?”+

  • Isaya 59:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Kumekuwa na ukosaji na kumkana Yehova;+ na kulikuwako kurudi nyuma kutoka kwa Mungu wetu, kusema ukandamizaji na maasi,+ kutunga na kunong’ona maneno ya uwongo kutoka moyoni.+

  • Yakobo 1:14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 14 Lakini kila mtu hujaribiwa kwa kuvutwa na kushawishiwa na tamaa yake mwenyewe.+

  • Yakobo 1:26
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 26 Ikiwa mtu yeyote anajiona kuwa mwabudu anayeshikilia vizuri namna ya ibada+ na bado hauongozi ulimi wake,+ bali anaendelea kuudanganya moyo wake mwenyewe,+ namna ya ibada ya mtu huyo ni ya ubatili.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki