21 Sasa tazama! umeweka tegemeo lako katika usaidizi wa tete hili lililopondeka,+ Misri,+ ambalo, mtu akiliegemea, hakika litaingia mkononi mwake na kuuchoma. Hivyo ndivyo Farao+ mfalme wa Misri alivyo kwa wote wanaomtegemea.
3 Hata hivyo, Wamisri ni watu wa udongo,+ wala si Mungu; na farasi wao ni nyama,+ wala si roho. Na Yehova mwenyewe atanyoosha mkono wake, na yeye anayetoa usaidizi atajikwaa, na yeye anayesaidiwa ataanguka,+ nao wote watafikia mwisho wakati mmoja.
6 Tazama! Umetegemea usaidizi wa tete hili lililopondeka,+ Misri,+ ambalo, mtu akiliegemea, hakika litaingia mkononi mwake na kuuchoma. Hivyo ndivyo Farao+ mfalme wa Misri alivyo kwa wote wanaomtegemea.+
17 Na kwa jeshi kubwa na kwa kutaniko lenye watu wengi Farao hatamfanya apate mafanikio katika vita,+ kwa kujenga boma la kuzingira na kwa kujenga ukuta wa kuzingira, ili kukatilia mbali nafsi nyingi.+