13 Baada ya hapo Mungu akamwambia Noa: “Mwisho wa wote wenye mwili umekuja mbele zangu,+ kwa maana dunia imejaa jeuri kwa sababu yao; na tazama mimi ninawaharibu pamoja na dunia.+
16 Manase pia alimwaga kwa wingi sana damu isiyo na hatia,+ mpaka alipolijaza Yerusalemu kutoka mwisho huu mpaka mwisho ule, mbali na dhambi yake aliyosababisha Yuda kutenda dhambi kwa kufanya yaliyokuwa mabaya machoni pa Yehova.+
4 kwa sababu wameniacha+ mimi nao wamepafanya mahali hapa pasitambuliwe+ na kufukiza moshi wa dhabihu ndani yake kwa miungu mingine ambayo hawakuijua,+ wao pamoja na mababu zao na wafalme wa Yuda; nao wamepajaza mahali hapa damu ya wasio na hatia.+
9 Kwa hiyo akaniambia: “Kosa la nyumba ya Israeli na Yuda+ ni kubwa, kubwa sana,+ na nchi imejaa umwagaji wa damu+ nalo jiji limejaa upotovu;+ kwa maana wamesema, ‘Yehova ameiacha nchi hii,+ na Yehova haoni.’+